Thursday, 30 January 2025

Tanzania Nakupenda Lyrics Sung by Acacia Singers, Tanzania

Tanzania Nakupenda Lyrics Sung by Acacia Singers, Tanzania


Refrain

Tanzania nakupenda nchi yangu nakupenda sana

Bara pia visiwani sisi sote tupendane sana


1. Tanzania yetu twakupenda kwa hakika

Uumbaji wake Mungu wetu ndio twausifu milele

Bahari zake alizotupa ndizo twajivunia leo

Bahari zake alizotupa ndizo twajivunia leo


2. Maziwa na vito nazo mbuga za wanyama

Mlima mrefu Kilimanjaro upitao yote Afrika

Makumbusho yetu ya taifa, ni vivutio kwa wageni

Makumbusho yetu ya taifa, ni vivutio kwa wageni


3. Taifa la amani na upendo kwa hao wote

Dumisha umoja Mungu Baba, na utuepushe na vita

Tupe ulinzi toka kwako Afrika yetu iwe moja

Tupe ulinzi toka kwako Afrika yetu iwe moja


Acacia Singers, Tz.

Wewe Ni Baba (Jenga Boma) Lyrics sung by Majaoni AY Kilifi, Kenya

Wewe Ni Baba (Jenga Boma) Lyrics sung by Majaoni AY Kilifi, Kenya 1. Wewe ni Baba wa kinilinda We ndiye shina anipendaye Marafiki wataponia...