Thursday, 30 January 2025

Tanzania Nakupenda Lyrics Sung by Acacia Singers, Tanzania

Tanzania Nakupenda Lyrics Sung by Acacia Singers, Tanzania


Refrain

Tanzania nakupenda nchi yangu nakupenda sana

Bara pia visiwani sisi sote tupendane sana


1. Tanzania yetu twakupenda kwa hakika

Uumbaji wake Mungu wetu ndio twausifu milele

Bahari zake alizotupa ndizo twajivunia leo

Bahari zake alizotupa ndizo twajivunia leo


2. Maziwa na vito nazo mbuga za wanyama

Mlima mrefu Kilimanjaro upitao yote Afrika

Makumbusho yetu ya taifa, ni vivutio kwa wageni

Makumbusho yetu ya taifa, ni vivutio kwa wageni


3. Taifa la amani na upendo kwa hao wote

Dumisha umoja Mungu Baba, na utuepushe na vita

Tupe ulinzi toka kwako Afrika yetu iwe moja

Tupe ulinzi toka kwako Afrika yetu iwe moja


Acacia Singers, Tz.

Mimi Ni Mungu/Mungu Wa Huruma Lyrics Sung by Acacia Singers, Tanzania

Mimi Ni Mungu/Mungu Wa Huruma Lyrics Sung by Acacia Singers, Tanzania

1. Mimi ni Mungu wenu asema Bwana
Nirudieni mimi Mungu wa kweli
Mnapotanga mbali nasikitika
Njooni wanangu sasa rudini nyumbani

Refrain
Mungu wa huruma tena mwenye na upendo
Aita wenye dhambi njooni wanangu

2. Yeye ajaye kwangu sitomtupa
Nitampa uzima ule wa milele
Kila asikiaye na aje sasa (asema)
Nyumbani mwake Baba makao ni mengi

3. Wataoshinda dhambi ‘tavikwa taji
Naye Mwokozi Yesu ‘tawakaribisha
‘Ingieni rahani mwa Baba yangu’
Mle mema ya nchi yaloandaliwa

Acacia Singers, Tz.

Sikia Neno La Bwana Yesu Lyrics Sung by Acacia Singers, Tanzania

Sikia Neno La Bwana Yesu Lyrics Sung by Acacia Singers, Tanzania

1. Sikia neno la Bwana Yesu Alivyosema kwa huzuni,
‘Mikononi mwako Baba yangu. Roho yangu uipokee’
Baada ya hayo Yesu Bwana, Alikataa roho kwa huzuni
Baada ya hayo Yesu Bwana, Alikataa roho kwa huzuni

Refrain
Aliishinda kifo Yesu (wangu) Sasa yu hai Bwana wangu
Yauja tena na Malaika Kila jicho litamuona

2. Na ilipokwisha pambazuka Siku ya kwanza ya juma
Walikwenda tazama kaburi Tazama lilikuwa tupu
Malaika wa Bwana alishuka Akaliondoa lile jiwe
Malaika wa Bwana alishuka Akaliondoa lile jiwe 

3. Ingawa walilinda kaburi askari wote walishindwa
Hofu kuu ilikuja kwao Wakatetemeka kwa uoga
Tetemeko kuu la kutisha Wakaanguka kwa nguvu hizo
Tetemeko kuu la kutisha Wakaanguka kwa nguvu hizo

Acacia Singers, Tz.

Wednesday, 22 January 2025

Siku Yake Mungu Lyrics sung by Acacia Singers

Siku Yake Mungu Lyrics sung by Acacia Singers


1. Siku yake Mungu inakuja

Kwa kila kiumbe juu ya nchi

Mungu atamwaga ghadhabu yake kuu

Wenye dhambi wote wataangamia


Mungu atamwaga ghadhabu yake kuu

Wenye dhambi wote wataangamia


Refrain

Atamwaga ghadhabu yake juu yetu

Atawasha hasira yake

Atamwaga ghadhabu yake juu yetu

Kamwe hatatoa rehema


2. Nani awezaye kusimama

Katika hukumu inayokuja

Waliokubali kumpokea Yesu

Hao ndio watakaokolewa


3. Utasimamaje ukiitwa?

Mbele ya kiti cha hukumu ya Mungu

Muda umekwisha tumrejee Yesu

Siku ile yaja kama vile mwivi


Muda umekwisha tumrejee Yesu

Siku ile yaja kama vile mwivi.


Acacia Singers, Tz.

Nitakufanya Kuta/Acacia Singers Lyrics sung by Acacia Singers

Nitakufanya Kuta/Acacia Singers Lyrics sung by Acacia Singers


1. Nitakufanya kuta wa boma la shaba

Hauta bomoshwa milele milele

Adui zako wote wapiganapo nawe

Hawatakushinda asema Mungu wetu (Hata)


Refrain

Hata juu mbinguni kwake

Tutapokutana naye

Acacia Singers wote

Tutaimba milele(Hata)


2. Mungu yu na uwezo mkuu ajabu

Hatoshindwa kamwe daima milele

Tatufanya imara kama mti mshita

Acacia kundi ndogo twaimba sifa zake


3. Kama mti mgumo ule wa mshita

Uloota wa amani* (kandokando) kando ya kijito

Akiwa kati yetu hatutayumbishwa

Twaomba Mungu wetu utufanye imara.


Acacia Singers, Tz.

Nitakwenda Pekee Yangu Lyrics sung by Acacia Singers

Nitakwenda Pekee Yangu Lyrics sung by Acacia Singers


1. Nitakwenda kwake mimi pekee yangu

Nasikia aniita “Njoo kwangu

Wewe utaabikaye Pekee yako itakoma,”

Asema Bwana “Mimi ndiye chakula ya uzima

Yeye alaye hataona njaa

Yeye alaye hataona njaa


Refrain

Yesu asema, "Njooni nyote kwangu

Furaha amani mtapata mbinguni."


2. Niambie u tayari kumwandama

Uende naye mbinguni

Je una shaka na hutaki kumwamini?

Au bado watamani raha za dunia?

Hatujui yatakayo jiri kesho

Mfuata Yesu upate uzima

Mfuata Yesu upate uzima


3. Wateule watakwenda naye Bwana

Kuishi huko mbinguni

Kwa furaha wamwimbie nyimbo tamu 

Za utukufu kwa shangwe wakiwa juu

Utukufu wake Mungu utang’aa

Walotakaswa wataishi humo.


Acacia Singers, Tz.

Ondoka Uangaze Lyrics sung by Acacia Singers

Ondoka Uangaze Lyrics sung by Acacia Singers


1. Ondoka uangaze kwa kuwa nuru ya Bwana imekuja

Na utukufu wa Bwana umekuzukia 

Ondoka peleke neno utangaze kwa wote 


Refrain

Wajulishe habari kwamba yu mlangoni

Anarejea upesi Mwokozi

Wajulishe wote kwamba yuko karibu


2. Amka harakishe usisubiri kwani muda waisha

Mavuno ni tayari wavuni wachache

Ondoka peleke neno utangaze kwa wote.


Acacia Singers, Tz.

Ungeniambia Nilipokosea Lyrics sung by Acacia Singers

Ungeniambia Nilipokosea Lyrics sung by Acacia Singers


1. Ungeniambia nilipokosea

Nikalijua kosa langu

Uenda ningebadilika

Nikajirekebisha

Umeifanya dhambi yangu

Kunuka mbele za watu

Mdahalo wote juu yangu

Kwa kosa nisilojua


Iiii Iiii Maneno haya yanahuruma

Ungeniambia nilipokosea

Nami nikabadilika


2. Maneno yanayonenwa juu yangu

Yanaumiza roho yangu

Laiti kama ungenijulisha

Nikajua ubaya wangu

Ungeniita kwa upole

Ukanieleza kwa pendo

Ungeiokoa nafsi yangu

Kwa haya yatokeayo 


3. Leo* uamue uje kwa Yesu

Aliye msaada wetu

Hakika Bwana wetu atupenda

Yeye ana huruma nyingi

Hutuonya kwa upole,

"Msitende dhambi wanangu,"

Yeye husamehe, husahau

Wala hakumbuki tena


Outro

Yesu utusaidie tuvishe

*Tufike mbele sote

Tufike mbinguni.


Acacia Singers, Tz.

Ninakushukuru Kwa Wema Wako Lyrics sung by Acacia Singers

Ninakushukuru Kwa Wema Wako Lyrics sung by Acacia Singers


1. Ninakushukuru kwa wema wako

Mungu mtukufu wa kuabudiwa

Wewe ndiwe mponya na hakuna mwingine

Umenishindia yaliyo makuu


Wewe ndiwe mponya na hakuna mwingine

Umenishindia yaliyo makuu


Refrain

Ni wewe tu Bwana Mungu wangu

Wala hakuna yeyote kama wewe

Ni wewe tu Bwana Mungu wangu

Ndiwe mfariji wangu hakuna mwingine


2. Uweza na nguvu (Yote) na mamlaka

Yashinda wakuu wote wa dunia

Nionapo milima, jua, mwezi na nyota

Wewe ni mkuu haulinganishwi


Nionapo milima, jua, mwezi na nyota

Wewe ni mkuu haulinganishwi


3. Nikifika kwako huko mbinguni

Nitakusujudu we mtakatifu

Sifa na heshima viwe nawe milele

Watu maelufu kukusujudia


Sifa na heshima viwe nawe milele

Watu maelufu kukusujudia.


Acacia Singers, Tz.

Ninakushukuru Kwa Wema Wako Lyrics sung by Acacia Singers

Ninakushukuru Kwa Wema Wako Lyrics sung by Acacia Singers


1. Ninakushukuru kwa wema wako

Mungu mtukufu wa kuabudiwa

Wewe ndiwe mponya na hakuna mwingine

Umenishindia yaliyo makuu


Wewe ndiwe mponya na hakuna mwingine

Umenishindia yaliyo makuu


Refrain

Ni wewe tu Bwana Mungu wangu

Wala hakuna yeyote kama wewe

Ni wewe tu Bwana Mungu wangu

Ndiwe mfariji wangu hakuna mwingine


2. Uweza na nguvu (Yote) na mamlaka

Yashinda wakuu wote wa dunia

Nionapo milima, jua, mwezi na nyota

Wewe ni mkuu haulinganishwi


Nionapo milima, jua, mwezi na nyota

Wewe ni mkuu haulinganishwi


3. Nikifika kwako huko mbinguni

Nitakusujudu we mtakatifu

Sifa na heshima viwe nawe milele

Watu maelufu kukusujudia


Sifa na heshima viwe nawe milele

Watu maelufu kukusujudia.


Acacia Singers, Tz.

Nguvu Zangu Pekee Lyrics sung by Acacia Singers

Nguvu Zangu Pekee Lyrics sung by Acacia Singers

1. Nguvu zangu pekee hazitoweza
Kupambana naye Ibilisi
Jeshi lake kubwa huniandama
Kote niendako hunitisha

Refrain
Nakuita mchungaji mwema (Yesu)
Yesu mwana wa Mungu (Kweli)
Nipitapo kati ya nyika
Bwana nisiogope

2. Ewe Mungu wangu nisaidie
Ona nasumbuka na mateso
Mzigo mzito niliobeba
Tautua kwako nipumzike

3. Masumbuko haya mpaka lini?
Bwana wangu Yesu niahidi
Tutapokutana makao mapya
Baba mama wote niwaone

Refrain
Nakuita mchungaji mwema (Yesu)
Yesu mwana wa Mungu (Kweli)
Nipitapo kati ya nyika
Bwana nisiogope

4. Ninapotazama juu mbinguni
Naiona nyota ile tukufu
Tukufu kwa wale wasafirio
Kwa machozi mengi Bwana Yesu

Refrain
Nakuita mchungaji mwema (Yesu)
Yesu mwana wa Mungu (Kweli)
Nipitapo kati ya nyika
Bwana nisiogope.

Acacia Singers, Tz.

Sisi Tu Wasafiri Lyrics sung by Acacia Singers

Sisi Tu Wasafiri Lyrics sung by Acacia Singers

1. Sisi tu wasafiri wa kwenda mbinguni
Dunia si kwetu, kwetu ni mbinguni

Muda u mbele yetu umeamuliwa juu
Na dunia hii kukomesha dhambi

2. Maisha ya dunia yamejaa mashaka
Mambo ya dunia yote yanapita

Yapaswa tujihoji tumeanguka wapi
Tumrudie Yesu yeye ndiye njia.

Acacia Singers, Tz.

Sina Hofu Wala Mashaka Lyrics sung by Acacia Singers

Sina Hofu Wala Mashaka Lyrics sung by Acacia Singers

1. Sina hofu wala mashaka
Kwani Yesu yu ndani yangu
Aongoza hatua zangu
Popote nitembeapo

Refrain
Nakaza mwendo Nasonga mbele
Japo njia ni ndefu
Dhiki taabu Nayo mateso
Kwa imani mimi nitafika 

2. Japo njia ina mabonde
Yote hayo mi' sitahofu
Ninajua niko salama
Mwendo nitaumaliza.

Acacia Singers, Tz.

Naamani Shujaa Wa Jeshi Lyrics sung by Acacia Singers

Naamani Shujaa Wa Jeshi Lyrics sung by Acacia Singers

1. Shujaa wa jeshi lile la washami
Mtu mkubwa jemedari mkuu wa vita
Muheshimiwa alishinda vita nyingi
Ni Naamani lakini alikuwa mkoma

Refrain
Mara saba ukaoge Yorodani
Utakaswe ngozi yako utapona 

2. Binti yule mfungwa mfanyakazi
Mu-Isiraeli aliyejawa huruma
Alitamka laiti angekuwepo
Nabii yule wa Msamaria angepona

3. Sasa tazama najua yote hakika
Hakuna Mungu humu duniani mwote
Ila katika Israeli pekee
Alitamka Naamani alipoponywa

Outro 1
Huyu Mungu muumbaji
Ndiye Mungu Bwana wetu
Anayeponya magonjwa
Na kutenda maajabu 

Outro 2
Njoo utakaswe dhambi zako
Usafishwe naye (na Yesu) kwa damu yake.

Acacia Singers, Tz.

Punda Mwana Punda Lyrics sung by Acacia Singers

Punda Mwana Punda Lyrics sung by Acacia Singers


Chorus

Endendeni katika kile kijiji kile kinachowakabili (Ndipo)

Mtamwona punda kafungwa na mwanapunda

Pamoja naye wafungueni nanyi mnilete

Mkiulizwa semeni Bwana anawahitaji

Mkiulizwa semeni Bwana anawahitaji


1. Wakaenda zao wale wanafunzi

Wakafanya vile alivyowaamuru

Shangwe furaha tele mji wote

Waliimba Hosana ajaye kwa jina la Bwana

Waliimba Hosana ajaye kwa jina la Bwana (Sasa)


2. Sababu ya furaha walokuwa nayo

Walitandika nguo zao njia yote

Wakiwa na matawi mikononi

Waliimba Hosana ajaye kwa jina la Bwan

Waliimba Hosana ajaye kwa jina la Bwana (Sasa)


3. Njooni tumwimbie Yesu Bwana wetu

Kwa ushindi mkuu natumtukuze

Njooni tumsifu mkombozi

Huyu ndiye Yesu Mwokozi wa maisha yetu (Haleluya)

Huyu ndiye Yesu Mwokozi wa maisha yetu.


Acacia Singers, Tz.


Mtafuteni Bwana/Wajane Lyrics sung by Acacia Singers

Mtafuteni Bwana/Wajane Lyrics sung by Acacia Singers

Uuuh, Uuuh, Uuuh
1. Mtafuteni Bwana kwani anapatikana
Mwombeni wakati wote yeye yu karibu
Hujibu maombi kwa wote wamwitao
Ikiwa usiku mchana hata asubuhi
Ikiwa usiku mchana hata asubuhi

Refrain
Ooh Baba (Baba), Ooh Mungu wangu
Uwasikie wote waliao Nawe uwape usingizi
Ooh Yesu (Yesu), Ooh Mungu wetu
Wajane wote uwape amani
Uwarehemu na yatima 


Aaah, Aaah, Aaah, Aaah

2. Ni ahadi yake yeye aliyoitoa
Yeyote ajaye kwangu sitamtupa kamwe
Na wimbi la shida lijapokuandama
Muite Bwana Yesu useme naye kwa upole
Muite Bwana Yesu useme naye kwa upole

Acacia Singers, Tz.

Sunday, 5 January 2025

When the Rich and the Poor Get Together Lyrics sung by The Gospel Train

When the Rich and the Poor Get Together Lyrics sung by The Gospel Train

(When We All Get Together With The Lord Lyrics)

(Now) When the rich and the poor get together with the Lord
Get together, get together with the Lord
They will treat each other like sister and brother
When they all get together with the Lord

Refrain
(Now) When we all get together (Hallelujah)
When they all get together with the Lord
They will treat each other like sister and brother
When they all get together with the Lord

(Now) When the tall and the short get together with the Lord
Get together, get together with the Lord
They will treat each other like sister and brother
When they all get together with the Lord

(Now) When the big and the small get together with the Lord
Get together, get together with the Lord
They will treat each other like sister and brother
When they all get together with the Lord

The Gospel Train.

This version has a wording variation to the one done by The Gaither's Band.

Twaja Mbele Zako Lyrics sung by Acacia Singers

Twaja Mbele Zako Lyrics sung by Acacia Singers

1. Twaja mbele zako,
Tu wanyonge kabisa
Twaleta dhambi zetu,
Ili utukomboe
Tunakuja jinsi tulivyo,
Utuoshe kwa damu yako

Refrain
Pekee yangu sitaweza 
Kuvumilia mateso 
Njoo Yesu mkombozi wangu

2. Pekee sitaweza,
Kuumshinda Shetani
Kama utaniacha,
Sitaweza Mkombozi
U mlinzi na ngome yangu,
Msaada ulokaribu.

Acacia Singers, Tz.

Ps 55:22 Cast thy burden upon the LORD, and he shall sustain thee: he shall never suffer the righteous to be moved.

Matthew 11:29-30 Take my yoke upon you, and learn of me; for I am meek and lowly in heart: and ye shall find rest unto your souls. For my yoke is easy, and my burden is light.

Psalms 68:19-20 Blessed be the Lord, who daily loadeth us with benefits, even the God of our salvation. Selah. He that is our God is the God of salvation;
and unto GOD the Lord belong the issues from death.

1 Peter 5:6-7 Humble yourselves therefore under the mighty hand of God, that he may exalt you in due time: Casting all your care upon him; for he careth for you.

Makaoni Mwake Lyrics sung by Acacia Singers

Makaoni Mwake Lyrics sung by Acacia Singers

1. Makaoni mwake Bwana nitaketi
Nile naye, nizungumze naye
Furahani mwake Bwana nitaketi
Nimwimbie wimbo mutamu
Nikiwa na amani na furaha moyoni mwangu
Nikiwa na amani na furaha moyoni mwangu

Refrain
Furaha yangu nifike juu
Yesu Mwokozi anipokee
Nitaimba na Malaika
Nyimbo nzuri nikimsifu Bwana

2. Mji wake Mungu niutamanio
Kuna raha isiyo kifani, aah
Wote walochoka watapumzishwa
Yesu Kristo atawafariji (kweli)
Kwenye mji wa Mungu ‘taishi naye Bwana wangu
Kwenye mji wa Mungu ‘taishi naye Bwana wangu

3. Tutakusanyika toka kila pembe
Kulitukuza jina la Yesu
Malango ya lulu yatafunguliwa
Naye Yesu Mkombozi wetu
Sikia nikueleze kuna raha kule kwa Baba
Sikia nikueleze kuna raha kule kwa Baba

Acacia Singers, Tz.

Huyu Yesu Mnazorayo Lyrics Sung by Acacia Singers, Tanzania

Huyu Yesu Mnazorayo Lyrics Sung by Acacia Singers, Tanzania

Verse 1
Huyu Yesu, ataitwa mnazorayo
Huyu Yesu, ataitwa mnazorayo
Twakueleza habari zake Yesu
Aliyeishi kama maskini
Akalelewa Yesu mjini Nazareti
Wakaazi wa mji huo
Wakamwita mnazorayo

Ata akakuwa akihubiri kote
Neno la uzima katika miji yote
Ata akakuwa akihubiri kote
Neno la uzima katika miji yote

Aliitwa mnazorayo
Aliitwa mnazorayo

Verse 2
Alikamatwa Yesu mnazorayo
Akapelekwa mbele ya makuhani
Akaeleza Yesu, “Nalikuwa nanyi,
Siku zote hekaluni nikiwafundisha nyote
Lipi nililotenda kwenu watu wangu
lililobaya kwenu nanyi mwanikamata?
Lipi nililotenda kwenu watu wangu
lililobaya kwenu nanyi mwanikamata?”

Break
Aaa-uuh, Aaah-Aaah
Aaa-aah, Aaah-Uuuh-Aliteswa!

Verse 3
Aliteswa Yesu mnazorayo
Aliteswa Yesu mnazorayo

Akaangikwa pale juu Goligotha
Yesu kalia Eloi, Eloi, Lama Sabakthani?"
Yaani "Mungu wangu,
Mbona sasa waniacha,"
Alilia Yesu masikini

Taji ya miba kawekewa kichwani
Wale Wayahudi hawakumfahamu
Taji ya miba kawekewa kichwani
Wale Wayahudi hawakumfahamu

Verse 4 Outro
Isingekuwa kifo chake Yesu
Nani angetoa uhai wake?
Isingekuwa kifo chake Yesu
Nani angetoa uhai wake?

Verse 5 Outro
Nani mwenye huruma kama Mungu wetu
Kumtoa mwana kubeba laana yangu *4

Acacia Singers, Tz.

Miaka Yangu Ni Michache/Neema Yako Lyrics sung by Acacia Singers

Miaka Yangu Ni Michache/Neema Yako Lyrics sung by Acacia Singers

1. Miaka yangu ni michache
Maisha yangu yamejaaa taabu
Sijaona furaha maishani mwangu
Yakiwa mafupi kamwe sitahuzunika

Refrain
Neema yako Eeh Bwana
Ndiyo twaitumaini
Yote chini yakiisha
Mwokozi atanitosha

2. Mara nyingi shetani hunisongaa
Hunionyesha shida, njaa, vita,
Magonjwa na mauti watu wakisumbuka
Kusudi nimwache Yesu Mkombozi wangu

Acacia Singers, Tz.

Ps 90:10 The days of our years are threescore years and ten; and if by reason of strength they be fourscore years, yet is their strength labour and sorrow; for it is soon cut off, and we fly away

Psalm 39:4-6 “Lord, make me to know my end And what is the extent of my days; Let me know how transient I am. “Behold, You have made my days as handbreadths, And my lifetime as nothing in Your sight; Surely every man at his best is a mere breath. Selah.
“Surely every man walks about as a phantom; Surely they make an uproar for nothing; He amasses riches and does not know who will gather them.

Psalm 39:4-7 NLT
4 “Lord, remind me how brief my time on earth will be. Remind me that my days are numbered — how fleeting my life is. 5 You have made my life no longer than the width of my hand. My entire lifetime is just a moment to you; at best, each of us is but a breath.” Interlude 6 We are merely moving shadows, and all our busy rushing ends in nothing. We heap up wealth, not knowing who will spend it. 7 And so, Lord, where do I put my hope? My only hope is in you.

Psalms 89:47 NLT Remember how short my life is, how empty and futile this human existence!

Zaburi 89:47 Ukumbuke jinsi mimi nisivyo wa kudumu; Kwa ubatili gani umeiumba jamii ya wanadamu!

Yesu Uje Kwangu Lyrics sung by Acacia Singers

Yesu Uje Kwangu Lyrics sung by Acacia Singers

1. Yesu uje kwangu,
Ukae kwangu moyoni
Unipe badiliko la pekee,
unifanye niwe nuru kote
Nauamini uwezo wako,
Yesu haushindwi jambo lolote

Refrain
Yote yawezekana
Kwa jina lake Yesu
Kila anayemwendea
Yesu atampokea

2. Bwana nakumbuka, 
Huruma zako za ajabu
Ulimsamehe Mariamu,
Aliposhitakiwa kwako
Hivyo ulitenda kwa Rahabu,
Alipokufuata kwa imani

3. Damu yake Yesu,
Husafisha makosa yetu
Aliangikwa msalabani, 
Akawa kafara ya aibu 
Hebu sikieni wito huu, 
Njooni tumsifu Mwokozi wetu.

Acacia Singers, Tz.

Ps 51:10 Create in me a clean heart, O God; and renew a right spirit within me.
Zaburi 51:10 Ee Mungu, uniumbie moyo safi, uifanye upya roho ya uthabiti ndani yangu.

1Jo 1:9 If we confess our sins, he is faithful and just to forgive us our sins, and to cleanse us from all unrighteousness.

1Yohana 1:9 Kama tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki, atatusamehe dhambi zetu na kutusafisha toka kwenye udhalimu wote.

Mr 9:23 Jesus said unto him, If thou canst believe, all things are possible to him that believeth.

Waebrania 11:1 Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni udhahiri wa mambo yasiyoonekana.

Tawala Ndani Yangu Lyrics sung by Acacia Singers

Tawala Ndani Yangu Lyrics sung by Acacia Singers

Verse 1
Tawala ndani yangu Muumbaji Mfalme
Unilinde na dhoruba zinazonizunguka
Kama mawimbi ya bahari yavumayo kwa nguvu
Ndivyo shetani na jeshi lake anavyonitafuta
Ndivyo shetani na jeshi lake anavyonitafuta

Verse 2
Ukae ndani yangu wakati ni mfupi
Popote nitembeapo uniongoze Yesu
Ata mwisho wa safari hii nikuone karibu
Uliyetoa uhai wako kwa wote wenye dhambi
Uliyetoa uhai wako kwa wote wenye dhambi

Verse 3
Tazameni ramani bandari ii karibu
Wala usichoke ndugu Mwokozi angojea
Tutapofika Yerusalemu tutamuona Yesu
Ndipo atafuta kila chozi huzuni zitakwisha
Ndipo atafuta kila chozi huzuni zitakwisha

Outro
Utawale ndani yangu, utawale, tawala ndani
Utawale ndani yangu, utawale, Bwana wangu tawala(*4)

Acacia Singers, Tz.

Habari Za Kuzaliwa Lyrics sung by Acacia Singers

Habari Za Kuzaliwa Lyrics sung by Acacia Singers

1. Habari za kuzaliwa kwake Bwana Yesu
Zilienea mjini Bethlehemu
[Ma-] Majusi toka mashariki walifika
Kuja kumuona Mwokozi wa dunia hii

Refrain
Waliiona nyota ya mashariki (ndipo)
Wakaondoka wote kwa furaha kuu
Walipofika kule Bethlehemu
Walimsujudia Yesu (wote)

2. Uwezo toka kwake Roho mtakatifu
Alizaliwa katika hori la ng'ombe
Imanueli yaani Mungu yu pamoja nasi
Tuziimbe sifa Mwokozi amezaliwa

3. Na Herode alipoupata ujumbe 
Kazaliwa mfalume wa Uyahudi
Alighadhabika ndipo kaua watoto
Wa kiume wote katika mji ule.

Acacia Singers, Tz.

Lu 1:14 And thou shalt have joy and gladness; and many shall rejoice at his birth.

1 Samuel 1:27–28 NIV "I prayed for this child, and the LORD has granted me what I asked of him. So now I give him to the LORD. For his whole life he will be given over to the LORD."

Psalm 8:1-2 NIV Lord, our Lord, how majestic is your name in all the earth! You have set your glory in the heavens. Through the praise of children and infants you have established a stronghold against your enemies, to silence the foe and the avenger.

Psalm 127:3 ESV Behold, children are a heritage from the Lord, the fruit of the womb a reward. Like arrows in the hand of a warrior are the children
of one’s youth. Blessed is the man who fills his quiver with them!

Yohana 3:16 Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee,
bali awe na uzima wa milele.

Bwana Utakaporudi Lyrics sung by Acacia Singers

Bwana Utakaporudi Lyrics sung by Acacia Singers

1. Bwana utakaporudi
Kama jinsi ulivyoahidi
Shida taabu za dunia hii
Zitakoma nikiwa nawe

Refrain
Ombi langu ujapo unikumbuke
Katika uzima wa milele
Utapoita wateule wako
Jina langu unikumbuke

2. Nilitanga mbali nawe (na)
Tena nilipotea gizani
Kama kondoo nilipotea
Ukanirejesha zizini

3. E mwamba na ngome yangu
Unisikie ninapokwita
Niokoe katika hatari
Na mateso yake Shetani.

Acacia Singers, Tz.

Psalms 25:7 “Remember not the sins of my youth, nor my transgressions: according to thy mercy remember thou me for thy goodness' sake, O LORD.”
Luke 23:42 And he said unto Jesus, Lord, remember me when thou comest into thy kingdom.
Psalm 136:23 He remembered us in our weakness. His faithful love endures forever.

Tutangaze Habari Lyrics sung by The Gospel Train

Tutangaze Habari Lyrics sung by The Gospel Train

1. Tutangaze habari zake Bwana
Tuendeni muda umekwisha (waisha)
Wapo wengi waliolala humu
Tuendeni tumtangaze Bwana

Refrain
Nuru yake Bwana iangaze
Waliopotea tuwatafute
Tutangazeni neno hili la Bwana
Muda kitambo Bwana a'rejea

2. Neno hili la ufalme wa Mungu
Tulieneze duniani kote
Mtu asijelia hakujua
Tuendeni tumtangaze Bwana 

Outro
Dada twende, twende
Twende tuhubiri neno lake Bwana Mwokozi
Tusambaze kote twende tuhubiri
Ndugu twende, twende
Twende tuhubiri neno lake Bwana Mwokozi
Tusambaze kote twende tuhubiri

Ewe twende, twende
Twende tuhubiri neno lake Bwana Mwokozi
Tusambaze kote twende tuhubiri

Kijana twende, twende
Twende tuhubiri neno lake Bwana Mwokozi
Tusambaze kote twende tuhubiri

Dada twende, twende
Twende tuhubiri neno lake Bwana Mwokozi
Tusambaze kote twende tuhubiri

Dada twende...

The Gospel Train, Kenya.

Japokuwa Safari ni Ndefu Lyrics sung by The Gospel Train

Japokuwa Safari ni Ndefu Lyrics sung by The Gospel Train

1.Japokuwa safari ni ndefu
Pande zote dhoruba mawimbi
Nina ujasiri Yesu yuko mbele
Mimi siogopi namwamini Yesu

Refrain 1
Shetani aniwinde ili animalize
Mimi simwogopi namwamini Yesu
Anifanye mgonjwa ili animalize
Mimi siogopi namwamini Yesu

Safarini anitege ili animalize
Ajali siogopi namwamini Yesu
Usiku akitisha ninaye mkombozi
Mungu mwenye upendo nimemwamini Yesu

2. Kwa hakika ndugu una mengi
Moyo wako unao uzito
Kuna jina moja ukiliita leo
U’tapata pumziko jina hilo ni Yesu

Refrain 2
Shetani atakuwinda ili akumalize
Mimi nakushauri ita jina la Yesu
Akufanye mgonjwa ili akumalize
Bado nakushauri ita jina la Yesu

Akikutega njiani ili akumalize
Tena nakushauri ita jina la Yesu
Usiku akitisha unae mkombozi
Mungu mwenye upendo ita jina lake

Outro
Na sisi hatutishwi
Tunaye mkombozi
Mungu mwenye upendo
Tumemwamini Yesu


The Gospel Train.

Namkaribisha Yesu Lyrics Sung by The Gospel Train

Namkaribisha Yesu Lyrics Sung by The Gospel Train

Refrain
Namkaribisha Yesu atawale ndani yangu
Dunia imechafuka, shida nyingi na majonzi
Najitoa kwake atawale ndani yangu
Hivyo ataniwezesha kuihama dunia hii

1. Nilikuwa mdogo sana kule tumboni mwa mama
Lakini akanilinda mpaka nilivyozaliwa
Wakati nikiwa mdogo akanilinda kanitunza
Maisha yake nimeipata namkaribisha Yesu (Huyu Yesu)

2. Nilikuwa mwovu sana mdanganyifu mwenye dhambi
Lakini kwa uwezo wake akanigeuza niwe mwema
Nikasikia sauti yake Yesu nikaitika
Nikapata utakatifu nimekaribisha Yesu (Huyu Yesu)

The Gospel Train, Kenya.

Hebu Tumheshimu Bwana Lyrics sung by The Gospel Train

Hebu Tumheshimu Bwana Lyrics sung by The Gospel Train

1. Hebu tumheshimu Bwana muumba wa vitu vyote
Uwezo wake ni mkuu kwa watu wake, eeeh
Tangu utotoni mwetu ametulinda muumba
Nitamshukuru, nitamshukuru Mungu wangu

Refrain
Anastahili heshima Mungu wetu
Yeye ni Mungu, ni Mungu wa Baba zetu
Tunapaswa kutangaza Mungu wetu
Hatuwezi kunyamaza, Mungu ni mkuu

2. Najua mimi mnyonge, mwili wangu ni dhaifu
Bila Mungu sina nguvu wala uwezo (wala uwezo)
Ninajitoa mhanga kwake aliye muweza
Naegemea kwake mwenyezi Mungu wangu.

The Gospel Train, Kenya.

Bwana Wangu Yesu Aliteseka Lyrics sung by The Gospel Train

Bwana Wangu Yesu Aliteseka Lyrics sung by The Gospel Train

1. Bwana wangu Yesu aliteseka
Msalabani kwa ajili yangu
Ili anikomboe kwa dhambi zangu
Moyo wangu unaburudika (Kweli)

Refrain
Nina furaha moyoni mwangu
Nitakusifu maishani yangu yote (ewe Bwana)
Ulikomboa kwa damu yako
Ili niwe mwana wako kamili (Baba)

2. Mungu wa Ibrahimu,Mungu wa Isaka
Nakumbuka maajabu uliyotenda
Katika maisha yangu miujiza uliyotenda
Inadhihirisha ukuu wako kwangu (Bwana)

3. Sasa imebakia kuona uso wako
Kwa kuja kwako mara ya pili
Unitayarishe kwa siku hiyo
Ili niwe kati ya wa'o waendao (Bwana).

The Gospel Train, Kenya.

Zamani Nilikuwa Lyrics sung by The Gospel Train

Zamani Nilikuwa Lyrics sung by The Gospel Train

1. Zamani nilikuwa mdhambi mpotevu
Nilizama dhambini bila matumaini
Nilikuwa katikati ya misitu mwenzangu
Shetani alinitega na mitego yake

Refrain
Asante Yesu kwa pendo lako
Ulonionyesha pale msalabani
Ulinitafuta mimi mdhambi
Kwa kifo chako Bwana nimekuwa huru

2. Mara ngapi umejikuta katika shimo la dhambi
Je wakumbuka pendo lake Yesu Bwana wa upendo
Alitufia kasulubiwa sote tupate wokovu
Nitaimba pendo lake na nitamuinua

The Gospel Train.

One Day Jesus Will Call My Name Lyrics sung by The Gospel Train

One Day Jesus Will Call My Name Lyrics sung by The Gospel Train


Refrain

One day Jesus will call my name

As days go by, Hope I don’t stay the same

I wanna get so close to Him there's no big change

On that day that Jesus calls my name


1. Some days drag and Some days fly

Some days I think of the day I’ll die

Some days fill me and some days drain

But one day Jesus will call my name


2. Now most days I pray but some days I curse

A number of days I put myself first

But it’s not what I do, the cross made that plain

And one day Jesus will call my name.


The Gospel Train.

This song also sung by Lynda Randle. This version is slightly different in wording from the original from lyrics.

Wewe Ni Baba (Jenga Boma) Lyrics sung by Majaoni AY Kilifi, Kenya

Wewe Ni Baba (Jenga Boma) Lyrics sung by Majaoni AY Kilifi, Kenya 1. Wewe ni Baba wa kinilinda We ndiye shina anipendaye Marafiki wataponia...