Wednesday, 22 January 2025

Ninakushukuru Kwa Wema Wako Lyrics sung by Acacia Singers

Ninakushukuru Kwa Wema Wako Lyrics sung by Acacia Singers


1. Ninakushukuru kwa wema wako

Mungu mtukufu wa kuabudiwa

Wewe ndiwe mponya na hakuna mwingine

Umenishindia yaliyo makuu


Wewe ndiwe mponya na hakuna mwingine

Umenishindia yaliyo makuu


Refrain

Ni wewe tu Bwana Mungu wangu

Wala hakuna yeyote kama wewe

Ni wewe tu Bwana Mungu wangu

Ndiwe mfariji wangu hakuna mwingine


2. Uweza na nguvu (Yote) na mamlaka

Yashinda wakuu wote wa dunia

Nionapo milima, jua, mwezi na nyota

Wewe ni mkuu haulinganishwi


Nionapo milima, jua, mwezi na nyota

Wewe ni mkuu haulinganishwi


3. Nikifika kwako huko mbinguni

Nitakusujudu we mtakatifu

Sifa na heshima viwe nawe milele

Watu maelufu kukusujudia


Sifa na heshima viwe nawe milele

Watu maelufu kukusujudia.


Acacia Singers, Tz.

Wewe Ni Baba (Jenga Boma) Lyrics sung by Majaoni AY Kilifi, Kenya

Wewe Ni Baba (Jenga Boma) Lyrics sung by Majaoni AY Kilifi, Kenya 1. Wewe ni Baba wa kinilinda We ndiye shina anipendaye Marafiki wataponia...