Thursday, 12 June 2025

Tunaye Roho - Anatuombea Lyrics sung by Acacia Singers

Tunaye Roho - Anatuombea Lyrics sung by Acacia Singers

1. Tunaye roho wake Mungu, Ambaye ni msaidizi
Hutuongoza kwenye ukweli, Hata tusitende uovu
Roho wa Mungu tuliyepewa, Hutukumbusha maagizo
Roho wa Mungu tuliyepewa, Hutukumbusha maagizo

Refrain
(Na bado) Anatuombea,
Juu mbinguni
(Na bado) Anatuombea
Dhambi zetu zipate kufutika

2. Tunaye mwana Yesu Kristo, Anatuombea kwa Baba
Hutuongoza kwenye kweli, Mchunga mwema wa kondoo
Mwombezi wetu kule mbinguni, Mtetezi wa wenye dhambi
Mwombezi wetu kule mbinguni, Mtetezi wa wenye dhambi

3. Lishike neno lake Mungu, Ukadumu kwenye sala
Naye roho mtakatifu, Atakujaza nguvu tele
Roho wa Mungu tuliyepewa, Usimuache aende zake
Roho wa Mungu uliyepewa, Usimuache aende zake

4. (Solo)
Mpatanishi, Yesu Kristo, Yeye aliye na mauwa
Kuhani wetu mwenye haki, Mtakatifu wake Bwana
Mwanakondoo aliyechinjwa, Kwa ajili ya wenye dhambi
Mwanakondoo aliyechinjwa, Kwa ajili ya wenye dhambi

Refrain
(Oh, Na bado) Anatuombea
(Kule kwa Baba) Juu mbinguni
(Kweli bado) Anatuombea
Dhambi zetu zipate kufutika

Refrain
(Nasema bado) Anatuombea
(Kule kwa Baba) Juu mbinguni
(Kweli bado) Anatuombea
Dhambi zetu zipate kufutika

Outro
Dhambi zetu; zetu zipate kufutika
Dhambi zetu; zetu zipate kufutika
Dhambi zetu; zetu zipate kufutika
Dhambi zetu; zetu zipate kufutika.

Acacia Singers.

For Revision #ForRevision

?kweli/ukweli

Ewe Bwana Nenda Nasi Lyrics sung by Osingo Secondary

Ewe Bwana Nenda Nasi Lyrics sung by Osingo Secondary

Refrain
Ewe Bwana nenda nasi *2 Ooh
Tupe nguvu za kushinda majaribu za dunia
Japo ni magumu kwetu japo ni makali
Mungu wetu nenda nasi tuweze kuyashinda

1. Watoto wake Ayubu kufariki nayo
Maradhi kajawa mwili mwake
Mali kuhisha Ayubu hakukata tamaa
Kuamini Mungu mali kurudishwa mara mbili

2. Umweleze Yesu shida zako
Kimbilio yetu maishani mwako 
Atatuongoza hadi tufike kwetu mbinguni
Atatuongoza hadi tufike kwetu mbinguni.


This is from home; Crudely recorded.
Add Year Later, Post/Link the Crude Song in Bedi Score YouTube Channel, Songs from Home

Osingo Secondary SDA Choir, Songs from Home, Fillers, For Revision, Bedi Score, Bedi Lyrics

Nitasimulia Kisa Cha Yesu Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Nitasimulia Kisa Cha Yesu Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Kwa matendo makuu aliyotenda
Kwa rehema zake nitasimulia,
Amebadilisha maisha yangu
Sasa natambua kwamba anipenda,
Nitasimulia habari zake
Kamwe sitaacha kunena habari,
Habari za Yesu tamu kwangu

Pre-Chorus
Nitasimulia habari zake,
Amebadilisha maisha yangu
Nilikuwa vile leo niko hivi,
Amebadilisha maisha yangu
Nitasimulia habari zake

Chorus
Mashariki (wote) kusini, wasikie
Kaskazini (wote) magharibi, wasikie (wasikie)
Vilindini (wote) na bahari, wasikie

Sasa natambua kwamba anipenda,
Nitasimulia habari zake
Kamwe sitaacha kunena habari,
Habari za Yesu tamu kwangu.

Kurasini SDA Choir.

Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Kurasini Vol 35, First Posting, Bedi Score, Bedi Lyrics

Yote Yatapita Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Yote yatapita tuonayo,
Yote yatapita tuyapendayo
Kitakacho dumu ni uzima,
Uzima ule wa milele

Refrain
Ni kitu gani kitacho dumu kwako
Ulivyonavyo vyote ni ubatili
Vyote vyatoweka havidumu,
Tafuta uzima milele

2. Mali utajiri vyatoweka,
Maisha ya sasa yanatoweka
Yesu analeta maisha mapya,
Yote ya kale yanapita

Outro
Mambo yote yanapita yatoweka
Tarajia uzima wa milele
Nasema, kaza mwendo usichoke
Yesu aleta mambo mapya.

Kurasini SDA Choir.

Ninayaweza Mambo Yote Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Ninayaweza mambo yote,
Kwa jina la Yesu
Nimejifunza kumtumaini siku zote

Refrain
Nayaweza yote kwa jina la Yesu,
Mbele yangu (ni)naona nuru
Anaongoza mapito yangu,
Ni jibu kwa mashaka yangu
Sitapungukiwa chochote,
Anajua shida zangu

2. Furaha amani ninatapata,
Kwa jina hili
Ni mtetezi wangu nikiitwa hukumuni.

Kurasini SDA Choir.

Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Kurasini Vol 35, Bedi Score, Bedi Lyrics

Kiasi Gani (Rudi Nyumbani) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Kiasi gani watanga mbali na Bwana
Na umerushwa rushwa huku na kule
Mahangaiko taabu za maisha
Rudi nyumbani, rudi kwa Bwana
Unahangaika bure, rudi nyumbani

Refrain
Rudi nyumbani, rudi kwa Bwana,
Sasa yatosha, rudi nyumbani
Kuna mambo mazuri yanayokungojea,
Kivulini mwa Yesu kuna faraja,
Nyumba ni nyumbani utakuwa hura
Kuna sauti inakuita,
Rudi nyumbani Bwana anakuita

Wasio na huruma wala hisani
Waliotayari kukuangamiza
Watakurarua wakuangamize
Rudi nyumbani, mwanangu rudi
Unahangaika bure, rudi nyumbani.

Kurasini SDA Choir.

Safari Ya Mbinguni Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


Nitazame juu, Sing ladies;
Ninapaza sauti; ‘Yesu uniokea’

Refrain
Eeeeh; Katika mikono ya Bwana nimetia nanga,
Oooh; Katika shida nilimwita akanisikia
Mikononi mwa Bwana kivuli cha faraja,
‘Enyi nyote mliolemewa,’ Bwana, anawaita

Yesu aliniona
Akayafuta machozi yangu
Nina amani, Sing ladies;
Bila Yesu ni bure, Sasa nina amani.

Kurasini SDA Choir.

Kama Kwenye Ngazi (Mungu Akiwa Upande Wetu) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Kama Kwenye Ngazi (Mungu Akiwa Upande Wetu) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

1. Kama kwenye ngazi ya Yakobo,
Malaika walifurika
Wengi washuka, wengi wapanda
Wakimzunguka, (Zunguka!)
Wengi washuka, wengi wapanda
Wakimzunguka, (Zunguka!)

Pre-Chorus
Mungu akiwa upande wetu,
Ni nani wa kutuogofwa?
Hutuzunguka hutuinua
Mikononi mwake

Chorus
Ni kama mlima wa Zayuni
-(Kama mlima---wa Zayuni)
Hutuzunguka kote kote
-(Huzunguka---kote kote)
Najivunia jina lenye nguvu
-(Najivuna jina---lenye nguvu)
Nimetulia, tena nina nguvu
-(Natulia tena---nina nguvu)
Mungu akiwa upande wetu tumogope nani?
Mungu akiwa upande wetu tumogope nani?

2. Kama kwenye ngazi ya Yakobo,
Ngazi yangu hulindwa naye
Sina mwingine, Sina mwingine,
Yesu anitosha, (Atosha!)
Sina mwingine, Sina mwingine,
Yesu anitosha.

Kurasini SDA Choir.

Asikutaabishe Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1 Asikutaabishe maana yeye haendi
Asikutaabishe safarini hayupo
Ni ya mtu mwenyewe
Asikutaabishe, Umtazame Yesu

Refrain
Hayupo, hayupo safarini hayupo
Mwisho wa safari

2. Majina yaitwapo jina lake halipo
Alishahukumiwa sababu ya uasi
Hana nafasi juu mbinguni
Asikutaabishe
Safari ya mbinguni, Umtazame Yesu.

Kurasini SDA Choir.

Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Kurasini Vol 35Bedi Score, Bedi Lyrics

Revise Rhythm & Flow

Bwana Umenichunguza Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Bwana umenichunguza kote kote
Na we’ umenijua hata kuketi kwangu
Na we’ wajua matendo yangu yote
Nikufiche nini Bwana wangu

Refrain
Hata nikijificha katika pango la giza (nene), bado ni kazi bure
Kwa mkono hodari utanitafuta huko, kila mahali uko
Njia zako za ajabu hazichunguziki, hazichunguziki
Mimi ni kiumbe wewe ni muumba
Hata nikilala chini ya bahari
Njia zangu zote waziijua
Ninajidanganya naja kwako Bwana

2. Tunajifunza somo hili kwa Yona
Alipotaka kwenda kujificha Tarshishi
Bila kujua akakutana nawe
Alipotoroka uso wako.

Kurasini SDA Choir.

Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Kurasini Vol 35, For Revision, Bedi Score, Bedi Lyrics

Revise Rhythm & Flow


Kati Ya Waloachwa Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Kati Ya Waloachwa Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

1. Kati ya wal’oachwa humu
Kati ya wal’opewa msamaha
Na mimi nilikuwa mmoja wao
Na mimi, Nasema; na mimi
Nikapewa msamaha

Refrain
Nikajiuliza kwa nini mimi? (kwa ni---‘mi-mi’4)
Mimi, kwa nini mimi?
Neema za Mungu ziwe juu yangu
Ni upendo wa ajabu

2. Gereza likafunguliwa
Wafungwa tuka-achwa huru
Na wote tukatoka gerezani
Na wewe, Nasema; na mimi
Nikapata msamaha.

Kurasini SDA Choir.

Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Kurasini Vol 35, For Revision, Bedi Score, Bedi Lyrics

Waloachwa; Wal’oachwa; Walioachwa

Nani Kati Yenu Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Nani kati yenu mtoto akimwomba mkate,
Yeye kama mzazi---atampa jiwe?
(Hum*3) Nani kati yenu mtoto akimwomba samaki,
Yeye kama mzazi---atampa nyoka?
(Hum*3) Baba wa mbinguni ni Baba anayetupenda
Mahitaji yetu---ajua ya kesho
(Hum*3) Anasema bisha malango ya mbinguni wazi,
Kila abishaye---atafunguliwa

Pre Chorus
Ameahidi baraka tele, Na ahadi zake ni za kweli
Msiwaze mambo ya kesho, yeye ayajua
Njooni kwake kwa ujasiri, Na enyi nyote mliolemewa
Msiwaze mambo ya kesho, yeye ayajua

Chorus
Tunajivunia Yesu, nani kama wewe?
Baba anayejua kutunza, analea
Mahitaji yetu yote mikononi mwake,
Hakika, (na) atupenda
Ni lini ‘tafika kwake nimwone uso kwa uso?
Yesu (Yesu), atupendaaa…

2. Ninajivunia jina la Yesu la thamani,
Kwake ninapata---uzima milele
(Hum*3) Ninajivunia simba wa kabila la Yuda,
Kivulini mwake---napata faraja
(Hum*3) Kila nikimwita yu tayari kunisikia,
Yuko ndani yangu---nami ndani yake
(Hum*3) Anasema bisha malango ya mbinguni wazi,
Kila abishae---atafunguliwa.

Kurasini SDA Choir.

Kitu Gani Kitachokutenganisha (Chagua Hivi Leo) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Kitu Gani Kitachokutenganisha (Chagua Hivi Leo) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Kitu gani kitachokutenganisha,

Na upendo wa Yesu ukajitenga naye

Tangu umjue Mwokozi wako,

Amekuwa ngao kimbilio


Refrain

Chagua chagua hivi leo ni nani utakayemtumikia

Utasita kati ya njia mbili hatarini (wewe)

Chagua utakayemtumikia


Chagua chagua, chagua chagua,

Chagua chagua, utakayemtumikia


Lakini mimi, mimi na nyumba yangu tutamtumikia Mungu wetu

Lakini mimi, mimi na nyumba yangu tutamtumikia Mungu wetu


2. Ni wakati wa kufanya uamuzi,

Acha kutangatanga kati ya njia mbili

Msimamo wako una mashaka,

Utangatanga hata lini?


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Kurasini Vol 35, Bedi Score, Bedi Lyrics

Fungua Fahamu Zangu Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


Fahamu zangu ni mali yako, Fungua fahamu zangu nione.

Refrain
Fungua fahamu za moyo wangu, Nikuone Yesu ndani yangu

2. Fungua fahamu zangu Bwana, Niitambue sauti yako
Niwe mtiifu (Na) mnyenyekevu, Fungua fahamu zangu nione
Niwe mtiifu (Na) mnyenyekevu, Fungua fahamu zangu nione.

Kurasini SDA Choir.

Wednesday, 11 June 2025

Umeshupalia Kibanzi - Toa Boriti Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Umeshupalia Kibanzi - Toa Boriti Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

1. Umeshupalia kibanzi kwenye jicho la nduguyo
Fanya matengenezo msaidie
Sote tumepungukiwa na utukufu wake Mungu
Ebu fanya matengenezo

Refrain
Toa boriti kwenye jicho lako kwanza
Ukamsaidia nduguyo
Sote tu wasafiri Kwenda Kanaani
Sote twarejea kwa Mwokozi

2. Umekuwa hakimu wa kuhukumu dhambi za nduguyo
Fanya matengenezo msaidie
Ndugu yako akikosa njia muonye kwa upole
Ebu fanya matengenezo.

Kurasini SDA Choir.

Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Neema Iliyoshuka Album, Bedi Score, Bedi Lyrics

Shupalia - To affirm with urgency, To Insist.
Definition Source; https://swahili-dictionary.com/swahili-english/shupalia_shupalia

Tulipofika (Kila Goti Litapigwa) - Wastahili Heshima Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Tulipofika kwenye miamba ya kutisha,
Yesu akawa ni mwamba wa kale
Tulipovuka bahari (bahari), Yesu maji ya uzima
Kwenye wanyama wakali (wakali), Kaitwa simba wa Yuda
Alipofika kwa wenye wadhambi,
Wakamwita Imanueli Mungu pamoja nasi

Refrain
Kila goti litapigwa litapigwa
Hakika mchana kweupe
Kila ndimi litakiri likisema,
Wazi wewe mwana wa Mungu
Wastahili heshima leo,
Hata milele milele

2. Tutakapofika mbinguni tutamuona,
Itakuwa ni furaha ajabu
Kufumba na kufumbua (fumbua), Makovu yataponyeshwa
Majeruhi watapona ('tapona), Hakuna maombolezo
Tutakapofika kwenye meza ya fahari,
Imanueli atakuwa wa kwanza.

Kurasini SDA Choir.

Inueni Mioyo (Roho Mtakatifu) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Inueni Mioyo (Roho Mtakatifu) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

1. Inueni mioyo mtazame juu 
Pokeeni roho mtakatifu
Ndiye msaada wetu mfariji
Inueni mioyo mtazame juu

Refrain
Kiongozi amini kwa wakati
Fungue mioyo yenu mjazwe roho
Ndiye roho wa kweli si wa machafuko
Atawaongoza awape amani
Njoo roho mtakatifu utushike mkono

2. Roho mtakatifu ni msaada
Hupatikanao kwa wakati
Fungueni mioyo aingie
Roho mtakatifu njoo kwangu.

Kurasini SDA Choir.

Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Neema Iliyoshuka Album, Bedi Score, Bedi Lyrics

Tazama Upendo (Mikoni Mwa Yesu) sung by Kurasini SDA Choir

Tazama Upendo (Mikoni Mwa Yesu) sung by Kurasini SDA Choir

1. Tazama upendo wa Mwokozi Yesu
Alivyotupenda hapo mwanzoni
Ahitaji wote watangao mbali
Wamrudie Mungu waokolewe
Atafuta waliokata tamaa
Waliochoshwa na dhambi Yesu anawaita
Waliolemewa na mizigo moyoni
Watakuwa huru atawapumzisha

Refrain
Hata sasa amini (wote) uwe huru
Tazama utazame Kalwari
Wanaomtumaini watabarikiwa
Ufalme u tayari kwa ajili yao

2. Mungu wa mbinguni awapenda wote
Ni mchunga mwema wakati wote
Ujapopita bondeni mwa mauti
Atakulinda ubaki salama
Miguuni pa Yesu kuna amani
Mbele yangu kuna ulinzi ulio imara
Awaita wote waje waokolewe
Watapata raha atawapumzisha

Outro
Wito wa Yesu kwa wote waliolemewa
Mikononi mwa Yesu watakuwa huru
Mikononi mwa Yesu, (Mikononi mwa Yesu)
Waliao watafutwa machozi, njoo kwa Yesu.

Kurasini SDA Choir.

Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Neema Iliyoshuka Album, Bedi Score, Bedi Lyrics

Fungueni Malango Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


Leo ni siku ya furaha tulioingoja
Ni siku kuu ya wateule toka kila pembe
Nisikie furaha
Marafiki waliotengana kufumba na kufumbua
Watakutana tena
Safari hii hakuna kifo wala kutengana
Nisikie furaha

Refrain
Furaha! Furaha! Furaha! Ni furaha
Siku yenye iko karibu

2. Shangwe tele na vigelegele
Vitasikika kutoka vinywa vya wateule
Itakuwa furaha
Yaliyopita yameshapita
Hakuna sababu kukumbuka yaliyopita
Twatazamia mambo mapya na maisha mapya
Itakuwa furaha.

Kurasini SDA Choir.

Wanaisraeli (Una Nini Mkononi) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Wanaisraeli (Una Nini Mkononi) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Chorus
Wanaisraeli wamekwama jangwani
Wameyasahau maajabu ya Mungu
'Musa una nini mkononi?
Piga mwamba watu wapate maji'
Jeshi la Farao linakuja
Nyosha fimbo yako juu ya bahari
Wakashuhudia maajabu ya Mungu
Wakapita kati ya bahari

Verse 1
Bahari ikagawanyika maajabu ya Mungu
 (Hum! Hum! Hum! Hum!...aaahaa)
Wakapita kuvuka kati ya maji ya bahari
 (Hum! Hum! Hum! Hum!...aaahaa)
Na jeshi ya Farao walipofika wakazama
 (Hum! Hum! Hum! Hum!...aaahaa)
Wakashangilia wakamsifu Mungu
Maajabu ya Mungu

Chorus
Wanaisraeli wamekwama jangwani
Wameyasahau maajabu ya Mungu
'Musa una nini mkononi?
Piga mwamba watu wapate maji'
Jeshi la Farao linakuja
Nyosha fimbo yako juu ya bahari
Wakashuhudia maajabu ya Mungu
Wakapita kati ya bahari

Verse 2
Nasi leo kama wanaisraeli wasafiri
 (Hum! Hum! Hum! Hum!...aaahaa)
Tumetangatanga jangwani tumekosa imani
 (Hum! Hum! Hum! Hum!...aaahaa)
Amini! Amini! Amini! Bwana atatimiza
 (Hum! Hum! Hum! Hum!...aaahaa)
Alivyoahidi, atakuwa nasi katika safari.

Chorus; Outro
Wanaisraeli wamekwama jangwani (wote)
Wameyasahau maajabu ya Mungu
'Musa una nini mkononi?
Piga mwamba watu wapate maji'
Jeshi la Farao linakuja
Nyosha fimbo yako juu ya bahari
Wakashuhudia maajabu ya Mungu
Wakapita kati ya bahari

Wanaisraeli wamekwama jangwani (wote)
Wameyasahau maajabu ya Mungu
'Musa una nini mkononi?
Piga mwamba watu wapate maji'
Jeshi la Farao linakuja
Nyosha fimbo yako juu ya bahari
Wakashuhudia maajabu ya Mungu
Wakapita kati ya bahari.

Kurasini SDA Choir.

Tunataka Kumuona Yesu Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. 'Tunataka kumuona Yesu, Yesu
Eh, Bwana tunataka kumuona Yesu
Sisi tunataka kumwona Yesu,'
Walikuwa wayunani
Miongoni mwa waliopanda kwenda kuabudu
Walimwendea Filipo wakisema;

Refrain
'Bwana, Eh Bwana tunataka kumwona Yesu,
Tumesikia habari zake, Tunataka kumuona Yesu, Ooh,
Bwana, Eh Bwana tunataka kumuona Yesu,'
Walimwomba Filipo naye akawasikia

2. Mara ngapi wewe umeomba kumwona Yesu
Ili aseme na wewe, Akupe chakula cha mbingu
Waweka moyo wako mbali
Wafunga milango ya moyo
Fungua leo, uwe kama wale (kama wale) wayunani wa kale
Waliamua kumwomba Filipo kwa moyo

Outro
Bwana Yesu kafungua milango ya mbingu
Ameinyosha mikono yake
Angoja uitike ukichukua hatua kumuita
Mwite leo akungoja...
Atakusikiliza...

Kurasini SDA Choir.

Gharama Ya Wito Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Gharama ya wito wa Yesu, Je waitambua?
Alikwisha itamka mapema
Uza vyote gawa vyote kisha unifuate
Tutapataje kupona tusipojali?

Sikia! Sikia! Sauti, Sikia!
Inayokuita leo
Dunia na yote yanapita yanatoweka
Tutapataje kupona tusipojali?

2. Tambua sauti ya Yesu inayokuita
Ya nyuma usifikiri njoo leo
Moyoni kata shauri la kufuata Yesu
Tutapataje kupona tusipojali?

Kurasini SDA Choir.

Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Neema Iliyoshuka Album, Bedi Score, Bedi Lyrics

Karibu Tutaona Jiji (Ni shangwe) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Karibu tutaona jiji tulioahidiwa
Msifadhaike mioyoni mwenu Yesu alitamka
Jicho halijapata kuona mazuri ya mbinguni
Kaza mwendo tuingie pale (pale) katika jiji.

Refrain
Nuru yake yaongoza kuingia kwenye jiji
Itakuwa jubilii ni shangwe juu mbinguni
Ndugu kaza mwendo tuingie (pale) katika jiji

Ni kunyatanyata mwendo wa pole, mwendo wa maharusi
Wakaaji wa jiji lile wamejawa na upendo
Wenye chuki hawatakuwepo (pale) katika jiji.

Kurasini SDA Choir.

Tulia Kwa Yesu Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Tulia kwa Yesu usitoke kamwe
Teseka naye ufikie mwisho
Ukazikwe na Yesu, Ufufuke naye
Ndiye msaada wako, Alpha na Omega
Tulia kwake usitoke

Refrain
Tulia kwa Bwana, Usitoke kamwe
Tulia! Tulia! Tulia! Tu
Usitoke kamwe uwe salama
Tulia, Usitoke kamwe

2. Tufani zivume usitoke kamwe
Ngome imara nyakati za taabu
Muite ataitika kwenye taabu zako
Yesu ndiye jibu
Ni mwanzo na mwisho
Tulia kwake usitoke.

Kurasini SDA Choir.

Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Neema Iliyoshuka Album, Bedi Score, Bedi Lyrics

Nashangaa (Kina Cha Pendo) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Nashangaa (Kina Cha Pendo) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

1. Nashangaa nashangaa, Kina cha upendo wa Mungu wanizunguka
Nashangaa tena nashangaa, Alivyo mwema kwangu siku zote
Kwa mapana marefu ya pendo, Nauona waziwazi
Pande zote amenizunguka, Naburudika kwenye pendo lako
Natembea bila wasiwasi, Katika pendo la Yesu

Refrain
Kina cha pendo la Yesu, Chazidi kina cha bahari
Hangaiko la machozi, Kwa Yesu ni furaha
Subiri ngoja uone Yesu, Atatenda kwa wakati
Kina cha upendo wa Yesu, Ni pendo lisilo kipimo

2. Nashangaa nashangaa, Maajabu ya pendo lake yanishangaza
Wema wake unadumu kwangu,Pendo lake linazidi kipimo
Nimeona marafiki wengi, Sijaona kama Yesu
Marafiki wa dunia hii, Wamejawa na pendo la herosi
Yesu ndiye rafiki wa kweli, Pendo lake linadumu.

Kurasini SDA Choir.

Kurasini SDA Choir - Kisha Nikaona Mbingu Nchi Mpya Lyrics

Kurasini SDA Choir - Kisha Nikaona Mbingu Nchi Mpya Lyrics


1. Kisha nikaona Mbingu Nchi mpya

Ikishuka hapo juu angani

Jeshi la Malaika wanapiga vinumbi

Wakimleta Bwana Harusi


Refrain

Kisha nikaona jiji Jerusalemi

Umepambwa unameta mji ni mzuri

Na wenyeji wake wapendeza

Si mbali kaza mwendo ufike pale.


2. Sauti za tarumbeta zasikika

Ni ishara Yesu anarudi

Jeshi la Malaika likishuka angani

Wakimleta Bwana Harusi.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Kurasini Neema Iliyoshuka Album, Bedi Score, Bedi Lyrics

Ni Habari Njema Kwangu (Neema Iliyoshuka) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Ni Habari Njema Kwangu (Neema Iliyoshuka) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Ni habari njema kwangu, Ni habari njema kwangu,

Habari njema kwako, Sikiliza kwa makini

Neema ni bure ni bure

Ilitolewa kwa wote, Ilitolewa kwa wote

Tulipotanga mbali, Kama kondoo bila mchunga

Kwa neema yake akatuokoa.


Refrain

Neema iliyoshuka, Ilisafisha njia ya wokovu

Ilitolewa na Mungu Baba, Kwa wenye dhambi

Neema ya bure juu yangu, Neema ya bure juu yako

Ilitolewa kwa ajili yangu, Na ilitolewa kwa ajili yako

Pokea neema bure, Toka kwa Mungu Baba.


2. Yesu alilipa bei, Yesu alilipa bei

Neema bure kwangu, Niliyestahili kifo

Kabeba msalaba wangu

Anachohitaji kwangu, Anachohitaji kwangu

Nimpe moyo wangu, Apate nafasi ndani yangu

Kwa neema yake ataniokoa.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Kurasini Neema Iliyoshuka Album, Bedi Score, Bedi Lyrics

Tuesday, 10 June 2025

Muumbaji Mfalme Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Muumbaji mfalme vitu vyote vyako,
Moyo wangu ni mali yako
Ndani yangu weka neno la uzima,
Nisimame kwenye neno lako

Refrain
Nitangaze sifa zako Bwana
Kati ya mataifa
Watu wakuone fungua njia,
Kaa nami Bwana

2. Nipe ujasiri mwingi nisimame,
Ndani yangu fanya kituo
Nisimame kama mitume wa kale,
Unifiche kwenye mbawa zako.


Kurasini SDA Choir.

Umepimwa Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Umepimwa Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Umepimwa kwenye mizani Mizani ya Bwana

Na umeonekana ndugu umepungua

Mizani ya Bwana umeonekana

Ya kwamba umepungua, Haleluya!


Refrain

Fanya matengenezo haraka

Umepimwa kwenye mizani Mizani ya Bwana

Umeonekana ndugu umepungua

Tafakari ndugu mwenendo wako, Haleluya!


2. Ajidhaniye amesimama ataanguka

Mizani ya Bwana itasimama daima

Ikisema kweli kwa matendo yako

Dhambi zitawekwa wazi, Haleluya!


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Injili Kwanza Album, Bedi Score, Bedi Lyrics

Nimesikia Wito Wako Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Nimesikia Wito Wako Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Nimesikia wito wako, Nami sitaghairi kuja kwako

Nimetambua kosa langu, Bado una makusudi juu yangu

Nimetambua kosa langu, La kutanga mbali na uso wako


Refrain

Ulisema tukibisha tutafunguliwa, Na mimi leo ninabisha kwako

Nifungulie lango la rehema, Najuta nimepoteza wakati

Nimetanga mbali na we’, Sasa yatosha najuta nisamehe

Wewe ni Bwana mwingi wa rehema, Nifungulie lango la rehema


2. Niite nikaseme nawe, Nikueleze haja za moyoni

Ninatubu maovu yangu, Kilio changu nikusamehewa

Nitamke kwa lugha gani, Nimechafuka najuta nipokee.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Injili Kwanza Album, Bedi Score, Bedi Lyrics

Sogea Karibu Nami Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Sogea Karibu Nami Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Sogea karibu nami Bwana

Unikumbushe mapito yako

Mimi ni dhaifu nasahau

Unikumbushe uwe karibu


Refrain

Ninaanguka ninasimama

Kama mtoto mchanga nakosa nguvu

Sogea karibu unishike mkono

Nina haja nawe kila saa


2. Uwe kando yangu safarini

Msaada wangu ni katika Bwana

Mimi ni dhaifu nasahau

Unikumbushe uwe karibu.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Injili Kwanza Album, Bedi Score, Bedi Lyrics

Sielewi Ni Kwa Nini Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Sielewi Ni Kwa Nini Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


Refrain

Sielewi, Sielewi ni kwa nini, Kila siku majaribu juu yangu

Leo nikisema ninatubu Kesho ninarudi palepale

Ni -? hili kesho nina lile, Nahitaji msaada toka juu

Nimechoka natamani nipumzike, Roho iko radhi mwili ni dhaifu


1. Nagundua ni Shetani Shetani hajalala usingizi

Kama simba awindaye Ndivyo anavyoniwinda

Ninafika mbali kuwaza Kwamba Yesu ameshaniacha – Oooh;

Kwani ninaposimama, Ndipo ninapoanguka (Sielewi!)


2. Napata faraja ninapotambua kwamba Yesu yuko nami

Hajalala usingizi Ndipo ninapata nguvu

Na katika hayo ndipo natambua kwamba Yesu anipenda – Oooh;

Nami ninapoanguka, Yesu ananiinua (Sielewi!)


Sielewi! Sielewi! Ni kwa nini?


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Injili Kwanza Album, For Revision, Bedi Score, Bedi Lyrics


*-?; Shinda, Ni ishi na

*Revise the Rhythm

Nina Rafiki Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Nina Rafiki Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Nina rafiki wa maisha, Asiyechoshwa nami

Amechukua shida zangu, Anipenda upeo


Refrain

Ananipenda (Ananipenda), Nampenda!

Ooh Ooh Yesu, Mkombozi wangu

Aliacha enzi yake, Akaja kanikomboa


Mkombozi wangu, Akashuka kwangu

Toka utumwani, Kaniweka huru


2. Kifo kaburi havivumi, Najua iko siku

Hata nikifa, atafufuka Yesu anaporudi.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Injili Kwanza Album, Kurasini Acapella, For Revision, Bedi Score, Bedi Lyrics


Stanza 2; Hata nikifa, *atafufuka; Hata nikifa atanifufua.

Bwana Ameahidi (Mikaeli) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


Akutane na shida zako akupe heri
Atatengeneza njia pasipo njia waja wapite
Ndiye Mungu wa yale yasiyowezekana

Refrain
Ataonyesha njia kwako katikati ya giza nene
Kati ya tanuru la moto liwakalo
Mikaeli atasimama upande wako utashinda

2. Ni Mungu anayetamka na ikawa amini leo
Fadhili na neema yake iwe juu yako
Akuinulie uso wake popote akurehemu
Ndiye Mungu wa yale yasiyowezekana.

Kurasini SDA Choir.

Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Injili Kwanza Album, Bedi Score, Bedi Lyrics

Njooni Kwenye Kisima Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Njooni kwenye kisima cha Bwana, Kuna maji ya uzima tele
Nyote mliojawa na kiu, Njooni kwenye kisima cha Bwana
Atakayekunywa maji ya kisima, Kisima cha Mwokozi
Hataona kiu, milele milele

Refrain
Usikiapo sauti ya Bwana, Fanya hima uje leo kwenye kisima
Upate maji ya uzima bure bure-bure, Yanayotolewa na Yesu bure
Na wale wanaotaka kuoga, Watakuwa wasafi wana wa Mungu
Njooni nyote katika kisima, Muoge na kunywa bure (Na)

2. Wito wa Yesu ni kwa watu wote, ‘Njooni kwangu mliochoka
Na mliolemewa na dhambi, Nira yangu ni laini njooni
Tena mzigo wangu kwenu ni mwepesi, Njooni mpumzike,
Nitakuwa nanyi, mwisho wa dahari.’

Kurasini SDA Choir.

Fuata Nyayo Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Fuata nyayo za Mwokozi kule Gethsemani
Utakuta alama alipo omba
Na jasho likawa damu Yesu akiomba
Fuata nyayo za Mwokozi kule Gethsemani

Refrain
Nyayo za Mwokozi zaongoza uzimani
Matone ya damu yaliyomwagika
Yesu anaomba usipotee
Fuata nyayo zake Gethsemani

2. Fuata nyayo za Mwokozi mlimani Golgotha
Utakuta alama za misumari
Elekea kaburini utaona jiwe
Limekwisha ondolewa Yesu kafufuka.


Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Injili Kwanza Album, Bedi Score, Bedi Lyrics

Sitaionea Haya (Injili Kwanza) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Sitaionea Haya (Injili Kwanza) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Sitaionea haya injili ya Yesu, Kwa maana ni uweza wake Mungu

Uweza unaoleta Wokovu, Kwa yeye anayeamini

Kwa maana waliosikia wito ni wengi, Ni nani aliyetayari?

Wote walotayari waende kwa imani, Uweza uwe juu yao.


Refrain

Injili kwanza ajenda ya moyoni, Uweza unaoleta Wokovu

Kwanza wajue habari njema, Mambo mengine mwachie Mungu

Najua vikwazo vinavyokuja, Vitazidi kuniimarisha.


2. Utayasikia mambo mengi utazame mbele, Majeraha yake ni ya kitambo

Hakuna kitu kitamshinda Yesu, Ukiwa mikononi mwake

Shetani hawezi kumshinda Simba wa Yuda, Kumbuka pigo la jangwani

Wote walotayari waende kwa imani, Uweza uwe juu yao.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Kurasini Injili Kwanza Album, Bedi Score, Bedi Lyrics

Wewe Ni Baba (Jenga Boma) Lyrics sung by Majaoni AY Kilifi, Kenya

Wewe Ni Baba (Jenga Boma) Lyrics sung by Majaoni AY Kilifi, Kenya 1. Wewe ni Baba wa kinilinda We ndiye shina anipendaye Marafiki wataponia...