Sitaionea Haya (Injili Kwanza) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir
1. Sitaionea haya injili ya Yesu, Kwa maana ni uweza wake Mungu
Uweza unaoleta Wokovu, Kwa yeye anayeamini
Kwa maana waliosikia wito ni wengi, Ni nani aliyetayari?
Wote walotayari waende kwa imani, Uweza uwe juu yao.
Refrain
Injili kwanza ajenda ya moyoni, Uweza unaoleta Wokovu
Kwanza wajue habari njema, Mambo mengine mwachie Mungu
Najua vikwazo vinavyokuja, Vitazidi kuniimarisha.
2. Utayasikia mambo mengi utazame mbele, Majeraha yake ni ya kitambo
Hakuna kitu kitamshinda Yesu, Ukiwa mikononi mwake
Shetani hawezi kumshinda Simba wa Yuda, Kumbuka pigo la jangwani
Wote walotayari waende kwa imani, Uweza uwe juu yao.
Kurasini SDA Choir.
Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Kurasini Injili Kwanza Album, Bedi Score, Bedi Lyrics