Fungueni Malango Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Fungueni Malango Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

1. Fungueni malango ya mbingu
Leo ni siku ya furaha tulioingoja
Ni siku kuu ya wateule toka kila pembe
Nisikie furaha
Marafiki waliotengana kufumba na kufumbua
Watakutana tena
Safari hii hakuna kifo wala kutengana
Nisikie furaha

Refrain
Watu wataruka wataruka kama ndama
Furaha! Furaha! Furaha! Ni furaha
Wakizunguka zunguka kiti cha enzi
Wameshinda mauti
Mungu ataketi kati ya wageni wake
Siku yenye iko karibu

2. Shangwe tele na vigelegele
Vitasikika kutoka vinywa vya wateule
Wakiimba wimbo wa Musa na Mwanakondoo
Itakuwa furaha
Yaliyopita yameshapita
Hakuna sababu kukumbuka yaliyopita
Twatazamia mambo mapya na maisha mapya
Itakuwa furaha.

Kurasini SDA Choir.

Popular posts from this blog

Tanzania Nakupenda Lyrics Sung by Acacia Singers, Tanzania

Damu Yake Lyrics sung by The Golden Gate Choir

Nyosha Mkono Wako Lyrics sung by Nyandema SDA Choir