Hebu Tumheshimu Bwana Lyrics sung by The Gospel Train
Hebu Tumheshimu Bwana Lyrics sung by The Gospel Train
1. Hebu tumheshimu Bwana muumba wa vitu vyote
Uwezo wake ni mkuu kwa watu wake, eeeh
Tangu utotoni mwetu ametulinda muumba
Nitamshukuru, nitamshukuru Mungu wangu
Refrain
Anastahili heshima Mungu wetu
Yeye ni Mungu, ni Mungu wa Baba zetu
Tunapaswa kutangaza Mungu wetu
Hatuwezi kunyamaza, Mungu ni mkuu
2. Najua mimi mnyonge, mwili wangu ni dhaifu
Bila Mungu sina nguvu wala uwezo (wala uwezo)
Ninajitoa mhanga kwake aliye muweza
Naegemea kwake mwenyezi Mungu wangu.
The Gospel Train, Kenya.
Comments
Post a Comment