Naamani Shujaa Wa Jeshi Lyrics sung by Acacia Singers
Naamani Shujaa Wa Jeshi Lyrics sung by Acacia Singers
1. Shujaa wa jeshi lile la washami
Mtu mkubwa jemedari mkuu wa vita
Muheshimiwa alishinda vita nyingi
Ni Naamani lakini alikuwa mkoma
Refrain
Mara saba ukaoge Yorodani
Utakaswe ngozi yako utapona
2. Binti yule mfungwa mfanyakazi
Mu-Isiraeli aliyejawa huruma
Alitamka laiti angekuwepo
Nabii yule wa Msamaria angepona
3. Sasa tazama najua yote hakika
Hakuna Mungu humu duniani mwote
Ila katika Israeli pekee
Alitamka Naamani alipoponywa
Outro 1
Huyu Mungu muumbaji
Ndiye Mungu Bwana wetu
Anayeponya magonjwa
Na kutenda maajabu
Outro 2
Njoo utakaswe dhambi zako
Usafishwe naye (na Yesu) kwa damu yake.
Acacia Singers, Tz.
Comments
Post a Comment