Punda Mwana Punda Lyrics sung by Acacia Singers

Punda Mwana Punda Lyrics sung by Acacia Singers


Chorus

Endendeni katika kile kijiji kile kinachowakabili (Ndipo)

Mtamwona punda kafungwa na mwanapunda

Pamoja naye wafungueni nanyi mnilete

Mkiulizwa semeni Bwana anawahitaji

Mkiulizwa semeni Bwana anawahitaji


1. Wakaenda zao wale wanafunzi

Wakafanya vile alivyowaamuru

Shangwe furaha tele mji wote

Waliimba Hosana ajaye kwa jina la Bwana

Waliimba Hosana ajaye kwa jina la Bwana (Sasa)


2. Sababu ya furaha walokuwa nayo

Walitandika nguo zao njia yote

Wakiwa na matawi mikononi

Waliimba Hosana ajaye kwa jina la Bwan

Waliimba Hosana ajaye kwa jina la Bwana (Sasa)


3. Njooni tumwimbie Yesu Bwana wetu

Kwa ushindi mkuu natumtukuze

Njooni tumsifu mkombozi

Huyu ndiye Yesu Mwokozi wa maisha yetu (Haleluya)

Huyu ndiye Yesu Mwokozi wa maisha yetu.


Acacia Singers, Tz.

Comments

Popular posts from this blog

Tanzania Nakupenda Lyrics Sung by Acacia Singers, Tanzania

Damu Yake Lyrics sung by The Golden Gate Choir

Nyosha Mkono Wako Lyrics sung by Nyandema SDA Choir