Punda Mwana Punda Lyrics sung by Acacia Singers
Punda Mwana Punda Lyrics sung by Acacia Singers
Chorus
Endendeni katika kile kijiji kile kinachowakabili (Ndipo)
Mtamwona punda kafungwa na mwanapunda
Pamoja naye wafungueni nanyi mnilete
Mkiulizwa semeni Bwana anawahitaji
Mkiulizwa semeni Bwana anawahitaji
1. Wakaenda zao wale wanafunzi
Wakafanya vile alivyowaamuru
Shangwe furaha tele mji wote
Waliimba Hosana ajaye kwa jina la Bwana
Waliimba Hosana ajaye kwa jina la Bwana (Sasa)
2. Sababu ya furaha walokuwa nayo
Walitandika nguo zao njia yote
Wakiwa na matawi mikononi
Waliimba Hosana ajaye kwa jina la Bwan
Waliimba Hosana ajaye kwa jina la Bwana (Sasa)
3. Njooni tumwimbie Yesu Bwana wetu
Kwa ushindi mkuu natumtukuze
Njooni tumsifu mkombozi
Huyu ndiye Yesu Mwokozi wa maisha yetu (Haleluya)
Huyu ndiye Yesu Mwokozi wa maisha yetu.
Acacia Singers, Tz.
Comments
Post a Comment