Yesu Alipokuwa Lyrics Sung by Your Voice Melody
Pre-Chorus
Yesu alipokuwa njiani kwenda Yerusalemu,
Alipoingia ndani ya kijiji kimoja,
Alikutana na watu kumi wenye ukoma
Walisimama mbali naye (--Na-ye-- Yesu),
Wakapaza sauti wakisema uturehemu
Alipowaona, aliwaambia,
‘Endeni mkajionyeshe kwa makuhani’
Na walipokuwa wakienda walitakasika.
Walipaza sauti wakisema,
‘Eeh Yesu Bwana mkubwa uturehemu.’
Chorus II
Mmoja wao alipoona kwamba amepona,
Alirudi kwa Yesu akiwa na furaha tele
Kamshukuru Bwana,
Kampa utukufu,
Mmoja wao alipoona kwamba amepona,
Alirudi kwa Yesu akiwa na furaha tele
Kamshukuru Bwana,
Kampa utukufu,
Imani yake ilimuokoa.
Verse
Watu wengi wanasahau
Wanasahau,
Yale Mungu amewatendea
Binadamu,
Binadamu hana asante,
Kwa yale Mungu ametenda
Ni mara ngapi we, Mungu amekuponya?
(----------------------------------------Amekuponya we)
Ni mara ngapi amekutoa shimoni?
(-------------------------Amekutoa shimoni?)
Tabia ya mwanadamu akiwa na shida
(--------ya mwanadamu---akiwa na shida)
Anamkumbuka Mungu akipata anamsahau,
(------------------------------akipata anamsahau)
Tabia ya wanadamu tukiwa na shida,
(--------ya wanadamu---------na shida)
Tunamkumbuka Mungu tukipata tunamsahau
(-------------------------------tukipata tunamsahau)
Shukuru Mungu kwa kila jambo,
Jifunze kusema asante ndugu yangu
Pre-Chorus
Yesu alipokuwa njiani kwenda Yerusalemu,
Alipitia Samaria na Galilaya
Alipoingia ndani ya kijiji kimoja,
Alikutana na watu kumi wenye ukoma
Walisimama mbali naye (--Na-ye-- Yesu),
Wakapaza sauti wakisema uturehemu
Alipowaona, aliwaambia,
‘Endeni mkajionyeshe kwa makuhani’
Na walipokuwa wakienda walitakasika.
Walipaza sauti wakisema,
‘Eeh Yesu Bwana mkubwa uturehemu.’
Chorus II
Mmoja wao alipoona kwamba amepona,
Alirudi kwa Yesu akiwa na furaha tele
Kamshukuru Bwana,
Kampa utukufu,
Imani yake ilimuokoa.
Mmoja wao alipoona kwamba amepona,
Alirudi kwa Yesu akiwa na furaha tele
Kamshukuru Bwana,
Kampa utukufu,
Imani yake ilimuokoa.
Your Voice Melody.
Your Voice Melody, SDA Swahili Songs, SDA Swahili Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics