Posts

Nenda Ninawi Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Nenda Ninawi Lyrics sung by Kurasini SDA Choir Verse 1 Nenda Ninawi , Peleka ujumbe (peleka ujumbe) Peleka ujumbe (peleka ujumbe) Nenda Ninawi Yona , Peleka ujumbe wangu Kwamba uovu wao umefika mbele yangu Verse 2 Kawaambie watubu (Kawaambie watubu) Nitangaamiza Ninawi (Nitangaamiza Ninawi) Kaipaze sauti (Kaipaze sauti) Watu wote wanapaswa kutubu, Wanadamu na wanyama Na vyote vilivyoumbwa na Mungu, Vyote vimlilie Mungu muumbaji Verse 3 Yona hakutaka kwenda Ninawi Kapanda merikebu ya Tarshishi Akijua anamkimbia Mungu Masikini Yona mtumishi wa Mungu hakujua, Mungu yuko pande zote Verse 4 Wakiwa baharini tufani ikavuma Upepo ukaipiga ile merikebu Meli ikatikiswa (ikatikiswa) Karibu ya kupasuka vipande vipande (vipande vipande) Yona hana habari (hana habari) Amefichiwa na usingizi (usingizi) ‘Amka! Wewe, Amka! Wewe, Usilale usingizi, Muombe Mungu wako atuokoe’ Verse 5 Yona alipoamka na kuona tufani, Akagundua kosa lake kwa Mungu Kamwambia nahodha, ‘Ili ninyi mpone…, Nitupeeni mimi baharin...

Upendo wa Yesu Lyrics sung by Light Group Ministry

Upendo wa Yesu Lyrics sung by Light Group Ministry 1. Upendo wa Yesu kwangu Upendo usiokipimo Japo dunia iishe ndugu Upendo wa Yesu waninitosha Chorus Upendo wa Yesu kwangu watosha Hakuna cha kulinganishwa na dunia hii Nimetafuta kote Hakuna upendo mwingine kama wa Yesu 2. Upendo ulimfanya Muumba wa mbingu na nchi Ashuke chini kutufilia Kutuokoa kwa dhambi zetu 3. Aliuwawa Bwana Yesu Kifo hicho cha msalaba Upendo wake kwa wenye dhambi Ulimpa kifo cha aibu. Light Group Ministry. Light Group Ministry, Bedi Score, Bedi Lyrics

Sikia Sauti Ya Bwana Lyrics sung by Light Group Ministry

Sikia Sauti Ya Bwana Lyrics sung by Light Group Ministry 1. Sikia sauti ya Bwana Inenayo moyoni Subira inanijia Kwa maneno hayo Giza litatoweka Majaribu yakome Subiri nuru ijayo Mvua itapokoma Chorus Manemo matamu Yanayonipa nguvu Yanituliza moyo Nipitapo shidani 2. Hata katika dhiki Nipitapo bondeni Hatari zinikumbapo Yeye huniongoza Huzuni zinikumbapo Kamwe sitachoka Subiri nuru ijayo Mvua itakapokoma. Light Group Ministry. Light Group Ministry, Bedi Score , Bedi Lyrics Whispering Hope / Soft as the Voice of an Angel

Panapo Pendo Lyrics sung by Light Group Ministry

Panapo Pendo Lyrics sung by Light Group Ministry 1. Vitu vyote ni sawa, Panapo pendo Kila sauti tamu, Panapo pendo Pana amani pale, Na furaha nyumbani Siku zote salama, Panapo pendo Chorus Panapo upendo , Siku zote salama, Panapo pendo. 2. Furaha i nyumbani, Panapo pendo Hapana machukizo, Panapo pendo Chakula ni kitamu, Mashamba ya sitawi Maisha ni kamili, Panapo pendo 3. Hata mbinguni juu, Pana furaha Wakiona upendo, Nyumbani mwetu Macho yanapendezwa, Na viumbe vya Mungu Naye Mungu huona, Panapo pendo 4. Ee Yesu niwe wako, Wako kabisa Ndipo patakuwako, Pendo nyumbani Nitakaa salama, Sitaifanya dhambi Nitabarikiwa tu, Panapo pendo. Light Group Ministry. Light Group Ministry, Bedi Score, Bedi Lyrics Nyimbo za Kristo No 184 . ( There Is Beauty All Around )

Pana Mahali Pazuri Mno Lyrics sung by Light Group Ministry

Pana Mahali Pazuri Mno Lyrics sung by Light Group Ministry 1. Pana mahali pazuri mno Twapaona kwa mbali sasa Baba yetu angoja pale Amepanga makao yetu Refrain Kitambo tu bado Tutakutana ng’ambo pale Kitambo tu bado Tutakutana ng’ambo pale 2. Tutaimba pale kwa moyo Nyimbo tamu za wenye heri Na rohoni hatutaona Tena haja ya kupumzika 3. Kwa Baba yetu mkarimu Tutatoa shukrani sana Kwa kipaji cha pendo lake Na baraka anazotupa. Light Group Ministry. Light Group Ministry, Bedi Score , Bedi Lyrics Nyimbo za Kristo No. 180 ( In the Sweet By and By / There’s a Land )

Nipe Neno Lyrics sung by Light Group Ministry

Nipe Neno Lyrics sung by Light Group Ministry 1. Nipe neno niweze kusema Itakayo mbingu kwa wanadamu Walioasi warejeshwe zizini mwako Chorus  Umetupa mamlaka duniani kote Tulihubiri neno lako Tukawaletee walopotea Warejee kwako 2. Kwa imani kamwe sihofu Neno lako faraja kwa waloasi Wasikiapo warejee zizini mwako. Light Group Ministry. Light Group Ministry, Bedi Score, Bedi Lyrics

Niimbe Pendo Lake Lyrics sung by Light Group Ministry

Niimbe Pendo Lake Lyrics sung by Light Group Ministry 1. Niimbe (Niimbe) pendo lake, Pendo la (Pendo la) Yesu Bwana ; Sababu (Sababu) alitoka Kwa Baba, akafa Chorus Niimbe (Niimbe) pendo lake; Sifa kuu (Sifa kuu) nitatoa; Akafa (Akafa) niwe hai, Niimbe pendo lake 2. Machozi (Machozi) alitoa  Ijapo (Ijapo) sijalia; Maombi (Aaombi) yangu bado, Aniombeapo 3. Upendo (Upendo) kubwa huo! Dunia (Dunia) haijui Samaha (Samaha) kwa makosa Kubwa kama yangu 4. Hapana (Hapana) tendo jema Ambalo (Ambalo) nilitenda, Nataka (Nataka) toka leo  Nimwonyeshe pendo. Light Group Ministry. Light Group Ministry, Bedi Score, Bedi Lyrics Nyimbo za Kristo No. 031 ( I Will Sing of Jesus Love )

Ni Yeye Lyrics sung by Light Group Ministry

Ni Yeye Lyrics sung by Light Group Ministry 1. Ni yeye anayejua shida zetu, Kwani ndiye aliyetufilia Aliacha enzi yake kule juu, Wewe nami tuokolewe Refrain Ndiye Yesu Mwokozi Anatutakasa  Ajua shida zetu Nani kama yeye? 2. Ni yeye anayejua shida zetu, Majaribu tunayoyapitia Hata pale tunapokata tamaa Bado yu mwaminifu kwetu. Light Group Ministry. Light Group Ministry, Bedi Score , Bedi Lyrics

Mlangoni Pa Moyo Lyrics sung by Light Group Ministry

Mlangoni Pa Moyo Lyrics sung by Light Group Ministry 1. Mlangoni pa moyo ; Mgeni! (Amesimama) Amesimama pale, Mgeni! (Amesimama) Umkaribishe sasa, Umkaribishe Mwana Wa Baba wa upendo: Mgeni! (Umkaribishe) 2. Moyo wako kwa Bwana, Fungua (Fungulieni) Asikuache mbali, Fungua (Fungulieni) Umkubali Rafiki, Roho atafariji Naye atakutunza: Fungua (Fungulieni)  3. Usikie sauti Ya Bwana (Uisikie) Uyachague mambo Ya Bwana (Mambo ya Bwana) Ufungue mlango, Usimwambie bado Jina lake tumai; Yu Bwana (Jina la Bwana) 4. Na ufungue moyo, Kwa Bwana (Fungulieni) Utapewa msaada, Wa Bwana (Msaada wetu) Uzuri utavikwa Dhambi ataondoa, Ukifungua moyo. Kwa Bwana (Fungulieni) Light Group Ministry. Light Group Ministry, Bedi Score , Bedi Lyrics Nyimbo za Kristo No. 157 ( There's a Stranger at the Door )

Ombi Langu Lyrics sung by Light Group Ministry

Ombi Langu Lyrics sung by Light Group Ministry 1. Mara nyingi nimezama katika mawazo Hata lini shida za dunia zitakoma Lakini najua siku itafika Haya yote yatapita Siku ile Yesu arudipo Refrain Majina yaitwapo Jina langu na liwepo Watakatifu wasimamapo Nami niwe kati yao Wakivikwa taji (Taji yangu mimi nayo) Taji yangu na iwepo Ombi langu Bwana (Ewe Yesu) Nikuone katika utukufu wako Ombi langu Bwana (Ewe Yesu) Nikuone katika utukufu wako 2. Wengi wameacha nuru iliyo ya kweli Wamezamia mambo ya dunia yapitayo  Lakini najua siku itafika  Haya yote yatapita siku ile Yesu arudipo. Light Group Ministry. Light Group Ministry, Bedi Score , Bedi Lyrics

Ikumbukeni Sabato Lyrics sung by Light Group Ministry

Ikumbukeni Sabato Lyrics sung by Light Group Ministry 1. Ikumbukeni Sabato Sabato ya Bwana Siku nzuri yenye raha Kupita siku zote Siku nzuri yenye raha Kupita siku zote Chorus Ni mpango wa Mungu Kwa kupanga siku sita Kutana siku ya saba Sabato takatifu Kutana siku ya saba Sabato takatifu 2. Moyo wangu wanivuta Niingie Sabato Ili kujifurahisha Kwa mambo ya Mungu. Light Group Ministry. Light Group Ministry, Bedi Score , Bedi Lyrics Adapted from Nyimbo za Kristo No. 084 ( Don’t Forget the Sabbath

Hatujui Saa Lyrics sung by Light Group Ministry

Hatujui Saa Lyrics sung by Light Group Ministry 1. Hatujui saa ya kuja kwwa Bwana, Lakini dalili zasema karibu Atakaporudi, lakini kwa kweli Hatujui saa Chorus Atakuja, kwa vile tukeshe; Atakuja Mwokozi, Aleluya! Atakuja kwa fahari ya Baba yake, Hatujui saa 2. Pana nuru kwao wapendao haki, Pana kweli katika chuo cha Mungu; Unabii hufundisha kuja kwake, Hatujui saa 3. Tutakesha na tutaomba daima, Tutafanya kazi mpaka akija, Tutaimba na tutasoma ishara, Hatujui saa. Light Group Ministry. Light Group Ministry, Bedi Score, Bedi Lyrics Nyimbo za Kristo No. 173 ( We Know Not the Hour )