Tunaye Roho - Anatuombea Lyrics sung by Acacia Singers
Tunaye Roho - Anatuombea Lyrics sung by Acacia Singers 1. Tunaye roho wake Mungu, Ambaye ni msaidizi Hutuongoza kwenye ukweli, Hata tusitende uovu Roho wa Mungu tuliyepewa, Hutukumbusha maagizo Roho wa Mungu tuliyepewa, Hutukumbusha maagizo Refrain (Na bado) Anatuombea, Juu mbinguni (Na bado) Anatuombea Dhambi zetu zipate kufutika 2. Tunaye mwana Yesu Kristo, Anatuombea kwa Baba Hutuongoza kwenye kweli, Mchunga mwema wa kondoo Mwombezi wetu kule mbinguni, Mtetezi wa wenye dhambi Mwombezi wetu kule mbinguni, Mtetezi wa wenye dhambi 3. Lishike neno lake Mungu, Ukadumu kwenye sala Naye roho mtakatifu, Atakujaza nguvu tele Roho wa Mungu tuliyepewa, Usimuache aende zake Roho wa Mungu uliyepewa, Usimuache aende zake 4. (Solo) Mpatanishi, Yesu Kristo, Yeye aliye na mauwa Kuhani wetu mwenye haki, Mtakatifu wake Bwana Mwanakondoo aliyechinjwa, Kwa ajili ya wenye dhambi Mwanakondoo aliyechinjwa, Kwa ajili ya wenye dhambi Refrain (Oh, Na bado) Anatuombea (Kule kwa Baba) Juu mbinguni (Kweli bado) ...