Posts

Tunaye Roho - Anatuombea Lyrics sung by Acacia Singers

Tunaye Roho - Anatuombea Lyrics sung by Acacia Singers 1. Tunaye roho wake Mungu, Ambaye ni msaidizi Hutuongoza kwenye ukweli, Hata tusitende uovu Roho wa Mungu tuliyepewa, Hutukumbusha maagizo Roho wa Mungu tuliyepewa, Hutukumbusha maagizo Refrain (Na bado) Anatuombea, Juu mbinguni (Na bado) Anatuombea Dhambi zetu zipate kufutika 2. Tunaye mwana Yesu Kristo, Anatuombea kwa Baba Hutuongoza kwenye kweli, Mchunga mwema wa kondoo Mwombezi wetu kule mbinguni, Mtetezi wa wenye dhambi Mwombezi wetu kule mbinguni, Mtetezi wa wenye dhambi 3. Lishike neno lake Mungu, Ukadumu kwenye sala Naye roho mtakatifu, Atakujaza nguvu tele Roho wa Mungu tuliyepewa, Usimuache aende zake Roho wa Mungu uliyepewa, Usimuache aende zake 4. (Solo) Mpatanishi, Yesu Kristo, Yeye aliye na mauwa Kuhani wetu mwenye haki, Mtakatifu wake Bwana Mwanakondoo aliyechinjwa, Kwa ajili ya wenye dhambi Mwanakondoo aliyechinjwa, Kwa ajili ya wenye dhambi Refrain (Oh, Na bado) Anatuombea (Kule kwa Baba) Juu mbinguni (Kweli bado) ...

Ewe Bwana Nenda Nasi Lyrics sung by Osingo Secondary

Ewe Bwana Nenda Nasi Lyrics sung by Osingo Secondary Refrain Ewe Bwana nenda nasi *2 Ooh Tupe nguvu za kushinda majaribu za dunia Japo ni magumu kwetu japo ni makali Mungu wetu nenda nasi tuweze kuyashinda 1. Watoto wake Ayubu kufariki nayo Maradhi kajawa mwili mwake Mali kuhisha Ayubu hakukata tamaa Kuamini Mungu mali kurudishwa mara mbili 2. Umweleze Yesu shida zako Kimbilio yetu maishani mwako  Atatuongoza hadi tufike kwetu mbinguni Atatuongoza hadi tufike kwetu mbinguni. Songs from Home As sung by Osingo Secondary.

Nitasimulia Kisa Cha Yesu Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Nitasimulia Kisa Cha Yesu Lyrics sung by Kurasini SDA Choir 1. Nitasimulia kisa cha Yesu, Kwa matendo makuu aliyotenda Kwa rehema zake nitasimulia, Amebadilisha maisha yangu Sasa natambua kwamba anipenda, Nitasimulia habari zake Kamwe sitaacha kunena habari, Habari za Yesu tamu kwangu Pre-Chorus Nitasimulia habari zake, Amebadilisha maisha yangu Nilikuwa vile leo niko hivi, Amebadilisha maisha yangu Nitasimulia habari zake Chorus Mashariki (wote) kusini, wasikie Kaskazini (wote) magharibi, wasikie (wasikie) Vilindini (wote) na bahari, wasikie Juu angani viumbe viseme ya kwamba Yesu; Mfalme wa utukufu 2. Katika tanuru amenilinda, Tunduni mwa simba kashuka kwangu Amenikingia mauti juu yangu, Hukumu ya kifo aliibeba Sasa natambua kwamba anipenda, Nitasimulia habari zake Kamwe sitaacha kunena habari, Habari za Yesu tamu kwangu. Kurasini SDA Choir. For Revision; Vilindini (wote) na bahari, wasikie

Yote Yatapita Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Yote Yatapita Lyrics sung by Kurasini SDA Choir 1. Yote yatapita tuonayo, Yote yatapita tuyapendayo Kitakacho dumu ni uzima, Uzima ule wa milele Refrain Ni kitu gani kitacho dumu kwako Ulivyonavyo vyote ni ubatili Vyote vyatoweka havidumu, Tafuta uzima milele 2. Mali utajiri vyatoweka, Maisha ya sasa yanatoweka Yesu analeta maisha mapya, Yote ya kale yanapita Outro Mambo yote yanapita yatoweka Tarajia uzima wa milele Nasema, kaza mwendo usichoke Yesu aleta mambo mapya. Kurasini SDA Choir.

Ninayaweza Mambo Yote Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Ninayaweza Mambo Yote Lyrics sung by Kurasini SDA Choir 1. Ninayaweza mambo yote, Kwa jina la Yesu Nimejifunza kumtumaini siku zote Refrain Nayaweza yote kwa jina la Yesu, Mbele yangu (ni)naona nuru Anaongoza mapito yangu, Ni jibu kwa mashaka yangu Sitapungukiwa chochote, Anajua shida zangu 2. Furaha amani ninatapata, Kwa jina hili Ni mtetezi wangu nikiitwa hukumuni. Kurasini SDA Choir.

Kiasi Gani - Rudi Nyumbani Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Kiasi Gani - Rudi Nyumbani Lyrics sung by Kurasini SDA Choir 1. Kiasi gani watanga mbali na Bwana Na umerushwa rushwa huku na kule Dunia imejaa mahangaiko, Mahangaiko taabu za maisha Rudi nyumbani, rudi kwa Bwana Unahangaika bure, rudi nyumbani Refrain Rudi nyumbani, rudi kwa Bwana, Sasa yatosha, rudi nyumbani Kuna mambo mazuri yanayokungojea, Kivulini mwa Yesu kuna faraja, Nyumba ni nyumbani utakuwa hura Kuna sauti inakuita, Rudi nyumbani Bwana anakuita 2. Duniani kuna mbwa mwitu wakali Wasio na huruma wala hisani Waliotayari kukuangamiza Watakurarua wakuangamize Rudi nyumbani, mwanangu rudi Unahangaika bure, rudi nyumbani. Kurasini SDA Choir.

Safari Ya Mbinguni Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Safari Ya Mbinguni Lyrics sung by Kurasini SDA Choir 1. Safari ya mbinguni; Kwenye njia nyembamba Tumaini linapotoweka Nainua uso wangu Nitazame juu, Sing ladies; Ninapaza sauti; ‘Yesu uniokea’ Refrain Eeeeh; Katika mikono ya Bwana nimetia nanga, Oooh; Katika shida nilimwita akanisikia Mikononi mwa Bwana kivuli cha faraja, ‘Enyi nyote mliolemewa,’ Bwana, anawaita 2. Katika giza hili; Yesu aliniona Akayafuta machozi yangu Nikawa mtumwa huru Nina amani, Sing ladies; Bila Yesu ni bure, Sasa nina amani. Kurasini SDA Choir.

Kama Kwenye Ngazi - Mungu Akiwa Upande Wetu Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Kama Kwenye Ngazi - Mungu Akiwa Upande Wetu Lyrics sung by Kurasini SDA Choir 1. Kama kwenye ngazi ya Yakobo, Malaika walifurika Wengi washuka, wengi wapanda Wakimzunguka, (Zunguka!) Wengi washuka, wengi wapanda Wakimzunguka, (Zunguka!) Pre-Chorus Mungu akiwa upande wetu, Ni nani wa kutuogofwa? Hutuzunguka hutuinua Mikononi mwake Chorus Ni kama mlima wa Zayuni -(Kama mlima---wa Zayuni) Hutuzunguka kote kote -(Huzunguka---kote kote) Najivunia jina lenye nguvu -(Najivuna jina---lenye nguvu) Nimetulia, tena nina nguvu -(Natulia tena---nina nguvu) Mungu akiwa upande wetu tumogope nani? Mungu akiwa upande wetu tumogope nani? 2. Kama kwenye ngazi ya Yakobo, Ngazi yangu hulindwa naye Sina mwingine, Sina mwingine, Yesu anitosha, (Atosha!) Sina mwingine, Sina mwingine, Yesu anitosha. Kurasini SDA Choir.

Asikutaabishe Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Asikutaabishe Lyrics sung by Kurasini SDA Choir 1 Asikutaabishe maana yeye haendi Asikutaabishe safarini hayupo Safari ya kwenda mbinguni Ni ya mtu mwenyewe Asikutaabishe, Umtazame Yesu Refrain Hayupo, hayupo safarini hayupo Yesu arudipo mwovu hana nafasi Asikuguze Shetani Mwisho wa safari 2. Majina yaitwapo jina lake halipo Alishahukumiwa sababu ya uasi Hana nafasi juu mbinguni Asikutaabishe Safari ya mbinguni, Umtazame Yesu. Kurasini SDA Choir.

Bwana Umenichunguza Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Bwana Umenichunguza Lyrics sung by Kurasini SDA Choir 1. Bwana umenichunguza kote kote Na we’ umenijua hata kuketi kwangu Na we’ wajua matendo yangu yote Nikufiche nini Bwana wangu Refrain Hata nikijificha katika pango la giza (nene), bado ni kazi bure Kwa mkono hodari utanitafuta huko, kila mahali uko Njia zako za ajabu hazichunguziki, hazichunguziki Mimi ni kiumbe wewe ni muumba Hata nikilala chini ya bahari Njia zangu zote waziijua Ninajidanganya naja kwako Bwana 2. Tunajifunza somo hili kwa Yona Alipotaka kwenda kujificha Tarshishi Bila kujua akakutana nawe Alipotoroka uso wako. Kurasini SDA Choir.

Kati Ya Waloachwa Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Kati Ya Waloachwa Lyrics sung by Kurasini SDA Choir 1. Kati ya wal’oachwa humu Kati ya wal’opewa msamaha Na mimi nilikuwa mmoja wao Na mimi, Nasema; na mimi Nikapewa msamaha Refrain Nikajiuliza kwa nini mimi? (kwa ni---‘mi-mi’4) Mimi, kwa nini mimi? Neema za Mungu ziwe juu yangu Ni upendo wa ajabu 2. Gereza likafunguliwa Wafungwa tuka-achwa huru Na wote tukatoka gerezani Na wewe, Nasema; na mimi Nikapata msamaha. Kurasini SDA Choir. Waloachwa; Wal’oachwa; Walioachwa

Nani Kati Yenu Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Nani Kati Yenu Lyrics sung by Kurasini SDA Choir 1. Nani kati yenu mtoto akimwomba mkate, Yeye kama mzazi---atampa jiwe? (Hum*3) Nani kati yenu mtoto akimwomba samaki, Yeye kama mzazi---atampa nyoka? (Hum*3) Baba wa mbinguni ni Baba anayetupenda Mahitaji yetu---ajua ya kesho (Hum*3) Anasema bisha malango ya mbinguni wazi, Kila abishaye---atafunguliwa Pre Chorus Ameahidi baraka tele, Na ahadi zake ni za kweli Msiwaze mambo ya kesho, yeye ayajua Njooni kwake kwa ujasiri, Na enyi nyote mliolemewa Msiwaze mambo ya kesho, yeye ayajua Chorus Tunajivunia Yesu, nani kama wewe? Baba anayejua kutunza, analea Mahitaji yetu yote mikononi mwake, Hakika, (na) atupenda Ni lini ‘tafika kwake nimwone uso kwa uso? Yesu (Yesu), atupendaaa… 2. Ninajivunia jina la Yesu la thamani, Kwake ninapata---uzima milele (Hum*3) Ninajivunia simba wa kabila la Yuda, Kivulini mwake---napata faraja (Hum*3) Kila nikimwita yu tayari kunisikia, Yuko ndani yangu---nami ndani yake (Hum*3) Anasema bisha malango ya mbinguni wa...