Sunday, 19 October 2025

Panapo Pendo Lyrics sung by Light Group Ministry

Panapo Pendo Lyrics sung by Light Group Ministry


1. Vitu vyote ni sawa, Panapo pendo

Kila sauti tamu, Panapo pendo

Pana amani pale, Na furaha nyumbani

Siku zote salama, Panapo pendo


Chorus

Panapo upendo,

Siku zote salama,

Panapo pendo.


2. Furaha i nyumbani, Panapo pendo

Hapana machukizo, Panapo pendo

Chakula ni kitamu, Mashamba ya sitawi

Maisha ni kamili, Panapo pendo


3. Hata mbinguni juu, Pana furaha

Wakiona upendo, Nyumbani mwetu

Macho yanapendezwa, Na viumbe vya Mungu

Naye Mungu huona, Panapo pendo


4. Ee Yesu niwe wako, Wako kabisa

Ndipo patakuwako, Pendo nyumbani

Nitakaa salama, Sitaifanya dhambi

Nitabarikiwa tu, Panapo pendo.


From: Nyimbo za Kristo No 184.

Writer: John Hugh McNaughton.


Light Group Ministry.


Light Group Ministry, Bedi Score, Bedi Lyrics

Wewe Ni Baba (Jenga Boma) Lyrics sung by Majaoni AY Kilifi, Kenya

Wewe Ni Baba (Jenga Boma) Lyrics sung by Majaoni AY Kilifi, Kenya 1. Wewe ni Baba wa kinilinda We ndiye shina anipendaye Marafiki wataponia...