Nenda Ninawi Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Nenda Ninawi Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


Verse 1

Nenda Ninawi,

Peleka ujumbe (peleka ujumbe)

Peleka ujumbe (peleka ujumbe)

Nenda Ninawi Yona, Peleka ujumbe wangu

Kwamba uovu wao umefika mbele yangu


Verse 2

Kawaambie watubu (Kawaambie watubu)

Nitangaamiza Ninawi (Nitangaamiza Ninawi)

Kaipaze sauti (Kaipaze sauti)

Watu wote wanapaswa kutubu,

Wanadamu na wanyama

Na vyote vilivyoumbwa na Mungu,

Vyote vimlilie Mungu muumbaji


Verse 3

Yona hakutaka kwenda Ninawi

Kapanda merikebu ya Tarshishi

Akijua anamkimbia Mungu

Masikini Yona mtumishi wa Mungu hakujua,

Mungu yuko pande zote


Verse 4

Wakiwa baharini tufani ikavuma

Upepo ukaipiga ile merikebu

Meli ikatikiswa (ikatikiswa)

Karibu ya kupasuka vipande vipande (vipande vipande)

Yona hana habari (hana habari)

Amefichiwa na usingizi (usingizi)

‘Amka! Wewe, Amka! Wewe,

Usilale usingizi,

Muombe Mungu wako atuokoe’


Verse 5

Yona alipoamka na kuona tufani,

Akagundua kosa lake kwa Mungu

Kamwambia nahodha,

‘Ili ninyi mpone…,

Nitupeeni mimi baharini’


Verse 6

Mimi na wewe rafiki,

Tumetumwa mara ngapi na Mungu?

Hatupeleki ujumbe tuliotumwa na Baba

Kwa ujinga tunadhani twajificha

Hebu leo tuwe kama Yona

Tugeuke na kwenda kufanya kazi

Bwana anatutuma…


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Kurasini Vol 35, Kurasini Acapella, Bedi Score, Bedi Lyrics

Comments

Popular posts from this blog

Tanzania Nakupenda Lyrics Sung by Acacia Singers, Tanzania

Muumbaji Mfalme Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Bwana wa mabwana Lyrics sung by Cherubim Singers, Nairobi South SDA