Wednesday, 24 September 2025

Kama Ilivyo Kwenye Safari Lyrics sung by Saro's Family

Kama Ilivyo Kwenye Safari Lyrics sung by Saro's Family


Eh-le lele-lele-lele-lele le-le-leh


1. Kama ilivyo kwenye safari

Kuna shida na matatizo

Kuna vikwazo dhoruba kali

Na majaribu mbalimbali

Safari yetu kwenda mbinguni

Mambo mengi huvunja moyo

Wasafiri hukataa tamaa


Refrain 1

Farao yuaja nyuma yetu (Nyuma yetu)

Bahari ya Shamu mbele yetu

Kunayo milima kandokando yetu

Bwana fungua njia (Farao)


Eh-le lele-lele-lele-lele le-eh


2. Kama ilivyo kule vitani

Jemedari yu mbele yetu

Mara jangwani, mara msalaba

Mwisho kaburi li wazi

Nasi nyumaye twasonga mbele 

Twazifuata nyayo zake tu

Tusichoke mwisho tutashinda


Refrain 2

Farao yuaja nyuma yetu (Nyuma yetu)

Bahari ya Shamu mbele yetu

Japo kuna shida na majaribu mengi

Njia atafungua. (Farao)


Saro's Family.


Saro’s Family, Bedi Score, Bedi Lyrics

Wewe Ni Baba (Jenga Boma) Lyrics sung by Majaoni AY Kilifi, Kenya

Wewe Ni Baba (Jenga Boma) Lyrics sung by Majaoni AY Kilifi, Kenya 1. Wewe ni Baba wa kinilinda We ndiye shina anipendaye Marafiki wataponia...