Kama Wanaisiraeli Lyrics sung by Grace and Glory Singers

Kama Wanaisiraeli Lyrics sung by Grace and Glory Singers

1. Kama Wanaisiraeli Katika safari yao
Safari ya siku chache jangwani
Ikawa ya miaka mingi
Wengi walikata tamaa Wengi walifia njiani
Ni wachache walifika Nchi ya ahadi
Ni wachache walifika Nchi ya ahadi

Refrain
Tutembee kwa ujasiri
Kwenye safari ya Kaanani
Yesu nahodha wetu ‘tatuvusha salama
Bila mwongozo wake
Hatuwezi vuka mto Yordani
Tujipe moyo tutafika

2. Nasi tunapiga hatua Moja mbele mbili nyuma
Katika safari yetu ya mbingu
Tupatapo majaribu
Tukazeni mioyo yetu sasa Tufikie ng'ambo ya pili
Kwani Pwani sio mbali Mwisho tutafika
Kwani Pwani sio mbali Mwisho tutafika.

Grace and Glory Singers.

Comments

Popular posts from this blog

Tanzania Nakupenda Lyrics Sung by Acacia Singers, Tanzania

Muumbaji Mfalme Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Bwana wa mabwana Lyrics sung by Cherubim Singers, Nairobi South SDA