Kama Wanaisiraeli Lyrics sung by Grace and Glory Singers
Kama Wanaisiraeli Lyrics sung by Grace and Glory Singers
1. Kama Wanaisiraeli Katika safari yao
Safari ya siku chache jangwani
Ikawa ya miaka mingi
Wengi walikata tamaa Wengi walifia njiani
Ni wachache walifika Nchi ya ahadi
Ni wachache walifika Nchi ya ahadi
Refrain
Tutembee kwa ujasiri
Kwenye safari ya Kaanani
Yesu nahodha wetu ‘tatuvusha salama
Bila mwongozo wake
Hatuwezi vuka mto Yordani
Tujipe moyo tutafika
2. Nasi tunapiga hatua Moja mbele mbili nyuma
Katika safari yetu ya mbingu
Tupatapo majaribu
Tukazeni mioyo yetu sasa Tufikie ng'ambo ya pili
Kwani Pwani sio mbali Mwisho tutafika
Kwani Pwani sio mbali Mwisho tutafika.
Grace and Glory Singers.
Comments