Sunday, 14 September 2025

Kati Ya Vyote (Aliniumba Kwa Mfano Wake) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Kati Ya Vyote (Aliniumba Kwa Mfano Wake) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Kati ya vyote vilivyoumbwa,

Niliumbwa kwa mfano wa Mungu

Ni kwa sababu alinifinyanga

Kwa mfano wake, Eeeh-Eeeh-Eeeh

Nilitoka mikononi mwake,

Inapendeza kurudi kwake

Aliniumba kwa mfano wake,

Kwa mapenzi ya Mungu


Refrain

Aliniumba kwa mfano wake,

Inapendeza nilitoka kwake

Ingawa dhambi ilitia waa,

Aliniosha nikawa safi

Ingawa dhambi ilitia waa,

Aliniosha nikawa safi, Safi-ii safi-ii

Aliniosha nikawa safi, Safi-ii safi-ii,

Aliniosha nikawa safi


2. Kanipulizia pumzi yake,

Nipate kuwa kiumbe hai

Ni kwa sababu alinifinyanga

Kwa mkono wake, Ooh-Ooh-Ooh

Ndio sababu ninapendeza,

Kuliko vyote vilivyoumbwa

Aliniumba kwa mfano wake,

Kwa mapenzi ya Mungu.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Ukuta Wa Jeriko Album, Bedi Score, Bedi Lyrics

Wewe Ni Baba (Jenga Boma) Lyrics sung by Majaoni AY Kilifi, Kenya

Wewe Ni Baba (Jenga Boma) Lyrics sung by Majaoni AY Kilifi, Kenya 1. Wewe ni Baba wa kinilinda We ndiye shina anipendaye Marafiki wataponia...