Monday, 22 September 2025

Kila Mtu Awapotezea Lyrics sung by Grace and Glory Singers

Kila Mtu Awapotezea Lyrics sung by Grace and Glory Singers


1. Kila mtu awapotezea wenye haki

Katika njia mbaya ataanguka

Katika rima lake yeye mwenyewe

Bali wakamilifu wataridhi mema

Yeye aligeuzaye sikio lake

Asisikie sheria ya Mungu

Hata sala yake ni chukizo,

Chukizo kwa Mungu


Chorus

Basi simameni katika njia kuu, Mkaone,

Mkaulize mapito ya zamani

Iwapo njia iliyo njema,

Mkaenende katika njia, Njia hiyo nzuri

Mkatubu dhambi zenu, Mkawe safi

Naye ninyi basi-ii, Mtajipatia raha katika nafsi zenu


2. Afichaye dhambi zake Hatafanikiwa

Bali yeye aziungamae na kuziacha atapata rehema

Aendaye kwa unyofu ataokolewa

Ila mkaidi wa njia zake Ataanguka mara.


Grace and Glory Singers.

Wewe Ni Baba (Jenga Boma) Lyrics sung by Majaoni AY Kilifi, Kenya

Wewe Ni Baba (Jenga Boma) Lyrics sung by Majaoni AY Kilifi, Kenya 1. Wewe ni Baba wa kinilinda We ndiye shina anipendaye Marafiki wataponia...