Msiwape Mbwa Lyrics sung by Grace and Glory Singers

Msiwape Mbwa Lyrics sung by Grace and Glory Singers


1. Msiwape mbwa kilicho kitakatifu

Wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe

Wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao

Wakageuka na kuwararua

Omba tafuta bisha, Kwa maana


Kila aombaye hupokea, Naye atafutaye huona

Abishaaye atafunguliwa, Mambo yatakuwa shwari


Kila aombaye hupokea, Naye atafutaye huona

Abishaaye atafunguliwa, Mambo yatakuwa shwari


Chorus

Basi ninyi salini hivi,


Baba yetu uliye mbinguni jina lako litukuzwe, ufalme,

Ufalme wako uje

Mapenzi yako yatimizwe hapa duniani, Kama mbinguni

Utupe leo riziki yetu,

Utusamehe deni zetu,

Kama sisi tuwasameavyo wadeni wetu

Usitutie majaribuni


2. Basi msalipo msiwe kama wanafiki

Kwa maana wao wapenda kusali

Hali wamesimama masinagogi na katika pembe za njia

Ili waonekane na watu


Bali wewe usalipo ingia katika chumba chako

Usali mbele ya Baba yako aliye sirini,

Na Baba yako aonaye sirini, Atakujali


Bali wewe usalipo ingia katika chumba chako

Usali mbele ya Baba yako aliye sirini,

Na Baba yako aonaye sirini, Atakujali.


Grace and Glory Singers.

Comments

Popular posts from this blog

Tanzania Nakupenda Lyrics Sung by Acacia Singers, Tanzania

Muumbaji Mfalme Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Bwana wa mabwana Lyrics sung by Cherubim Singers, Nairobi South SDA