Sunday, 12 October 2025

Tule Nini Lyrics sung by Hope Voice Group

Tule Nini Lyrics sung by Hope Voice Group


1 ‘Tule nini? Tuvae nini?’ Tumwachie Bwana


Tunahangaika usiku na mchana

Kwamba tule nini, Tuvae nini

Hata twamsahau Bwana

Hapa duniani sote tuwapitaji

Hata muda wetu ni mfupi

Twapita kama maua


Refrain

Bwana asema, ‘Tazameni ndege wa angani

Hata maua ya kondeni yanavyochanua

Nyinyi je si bora, kuliko wao?

Tafuteni ufalme wa Mungu wetu

Nayo, Mahitaji mtazidishiwa’


2. Kwa kuhangaika twadhani twaongeza

Hata kimo chetu, Maisha yetu

Pasipo na Bwana Mungu,

Tunajidanganya tunapotegemea

Hasa nguvu zetu akili zetu,

Na kumsahau Bwana.


Hope Voice Group.


Hope Voice Group, Bedi Score, Bedi Lyrics

Wewe Ni Baba (Jenga Boma) Lyrics sung by Majaoni AY Kilifi, Kenya

Wewe Ni Baba (Jenga Boma) Lyrics sung by Majaoni AY Kilifi, Kenya 1. Wewe ni Baba wa kinilinda We ndiye shina anipendaye Marafiki wataponia...