Nena Mungu sung by Cherubim Singers, Nairobi South SDA
Nena Mungu sung by Cherubim Singers, Nairobi South SDA
1. Nena rohoni Yesu, Nena kwa upole
Sema kwangu kwa pendo, “Huachwi upweke.”
Fungua moyo wangu, Nisikie mara;
Jaza roho na sifa, Sifa zako Bwana.
Kila siku unene, Vile kwa upole.
Nong’oneza [kwa pole] wa upendo:
“Daima utashinda, Uhuru ni wako.”
Nisikie maneno: “Huachwi upweke.”
2. Nena kwa wana wako, Waonyeshe njia,
Wajaze kwa furaha, Fundisha kuomba;
Wajifunze kutoa, Maisha kamili,
Wahimize ufalme, Tumwone Mwokozi.
3. Nena kama zamani, Ulipoitoa
Sheria takatifu: Niiweke pia;
Nipate kutukuza Wewe Mungu wangu,
Mapenzi yako tena, Daima kusifu.
Cherubim Singers, Nairobi South SDA.
F. Campana as Writer, Adapted by Leander Lycurgus.
From Nyimbo Za kristo 013
Comments
Post a Comment