Siku Moja/Watoto Walia Lyrics sung by The Gospel Train

Siku Moja/Watoto Walia Lyrics sung by The Gospel Train

1. Siku moja niliondoka kutembelea rafiki yangu

Rafiki yangu kaniuliza "Umekuja kunicheka?

Kwamba mimi masikini, Mama mjane tena fukara

Mimi sioni haja tena ya ushirika,

Mungu amenitenga mbona nimuabudu?"


Refrain

Watoto walia, "Mama ako wapi, baba?"

Wajane wanauliza, "Yesu tumefanya nini?"

"Mbona tupitie haya? Mbona tusumbuke hivi?

Na sala sisi twatoa?"


2. "Mungu huyu mnayemwabudu, Ni Mungu wa aina gani?

Ni Mungu yule anayenyamaza tunapodhoofika,

Miaka mingi tumemwabudu, Kwa hali hata na mali

Jamani nielezeni sababu ya ushirika?

Mungu amenitenga mbona nimuabudu?"


Outro

Yesu anajibu "Mimi Baba ya mayatimu wote

Bwana, wa wajane wote, msiogope."


"Nitawalinda nitawachunga Mimi Mungu mwaminifu

Nilivyolinda mababu zenu Isaka kina Yakobo."


The Gospel Train, Kenya.


Heb 13:5 I will never leave thee, nor forsake thee.

Ps 34:18 The Lord is near to the broken hearted, and saves the CRUSHED in spirit.[bold is mine]

Zaburi 34:18 Mwenyezi-Mungu yu karibu na waliokufa moyo; huwaokoa wote waliokata tamaa kabisa.

Comments

Popular posts from this blog

Tanzania Nakupenda Lyrics Sung by Acacia Singers, Tanzania

Damu Yake Lyrics sung by The Golden Gate Choir

Nyosha Mkono Wako Lyrics sung by Nyandema SDA Choir