Nira ya Bwana Lyrics sung by Kurasini SDA Choir
1. Nira ya Bwana ni laini, Njooni nyote msumbukao
Fungueni mioyo yenu, Mjitwishe nira ya Bwana
Nira ya Bwana ni laini, Fungueni mioyo yenu
Naye atawaweka huru, Rahani mwake.
Refrain
Unahangaika bure, Dunia yakurusharusha
Bwana akuita ndugu, Upumzike.
Unahangaika bure, Dunia yakurusharusha
Bwana akuita ndugu, Upumzike.
Yeye ajaye sitamtupa, Ataiona raha milele
Yeye ajaye sitamtupa, Atavikwa vazi vazi la kifalme.
2. Bisheni mtafunguliwa, Ombeni nanyi mtapewa
Malango ya mbingu ni wazi, Ni kwa ajili yenu nyote
Sauti yake ya upole, Mtwishe msalaba wako
Naye atawaweka huru, Rahani wake.
Kurasini SDA Choir.
Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Kurasini Vol 25, Bedi Score, Bedi Lyrics