Kaa Nami Lyrics sung by Springs Of Hope Kenya
1. Kaa nami ni usiku tena; usiniache gizani, Bwana,
Msaada wako haukomi; Nili peke yangu, kaa nami.
2. Siku zetu hazikawi kwisha; Sioni la kunifurahisha;
Hakuna ambacho hakikomi, Usiye na mwisho kaa nami.
3. Nina haja nawe kila saa; sina mwingine wa kunifaa
Mimi nitaongozwa na nani ila wewe? Bwana kaa nami.
4. Sichi neno uwapo karibu; Nipatalo lote, si taabu;
Kifo na kaburi havikumi; Nitashinda kwako, kaa nami.
5. Nilalapo nikuone wewe; Gizani mote nimulikiwe;
Nuru za mbinguni hazikomi, siku zangu zote; kaa nami.
Texts | Exo 33:14-15, Ps 61
From: Nyimbo Za Kristo No. 091.
Writer: Henry Francis Lyte
Composer: EVENTIDE (William H Monk)
Springs Of Hope Kenya.
Springs Of Hope Kenya, Swahili Hymns, Bedi Score, Bedi Lyrics