Nimeona Nikimbilie Kwako Lyrics sung by Kurasini SDA Choir
1. Nimeona nikimbilie kwako Bwana,
Nipate msaada wako Bwana
Nimesongwa na majaribu njia zote,
Nishike mkono uniongoze.
Refrain
Safari imezidi kuwa ngumu kwangu,
Wewe ndiwe tumaini langu
Usinifiche uso wako niitapo
U tayari kuniokoa,
Bwana nakuhitaji, Kwangu.
2. Pekee yangu sitaweza kuvuka ng'ambo,
Njia ya injili ni ya shida
Pamoja na wewe nitakwenda popote,
Nishike mkono uniongoze.
Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Kurasini Vol 24, Bedi Score, Bedi Lyrics