Wawili Wawili Lyrics sung by Kurasini SDA Choir
1. Wawili wawili Mungu aliviumba viumbe vyake vyote
Akaona ni vyema kwa utukufu wake
Katika safina Nuhu aliwaita wawili wawili waje
Kwa agizo la Mungu kwa utukufu wake.
Refrain
Wawili wawili (Wawili) Mungu aliumba,
Katika shida katika raha,
Wawili wawili ndoa iheshimiwe,
Na watu wote.
2. Wawili wawili msiachane kamwe ni agizo la Mungu
Dumuni siku zote katika pendo lake
Wakati wa shida Bwana yuko karibu kulinda nyumba yenu
Dumuni siku zote katika pendo lake.
Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Kurasini Vol 24, Bedi Score, Bedi Lyrics