Sauti Yangu Lyrics sung by Kurasini SDA Choir
1. Sauti yangu bado ina nguvu, Naweza kutangaza injili
Najua wakati itafika, sitaweza imba tena.
Refrain
Najua wakati utapofika, Nitanyamaza kimya
Sauti yangu itatoweka, Nitaporudi mavumbini
Nitawezaje kunyamaza kimya? Sauti yangu bado ina nguvu.
2. Miaka yangu ni ya kukopeshwa, Naishi kwa rehema za Bwana
Hakuna jema nililotenda, Kushinda waliolala.
3. Sioni sababu ya kukaa kimya, Jeshi la Bwana liko vitani
Nitafichaje talanta yangu? Nitaulizwa na Bwana.
Kurasini SDA Choir.
Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Kurasini Vol 29, Bedi Score, Bedi Lyrics