Najuta Lyrics sung by Kurasini SDA Choir
1. Najuta, Najuta
Nikiwaza ya kale, najuta
Kwa kupoteza wakati, Kwa kupenda dunia
Yalikuwa ya kale, najuta
Kwa kupoteza wakati, Kwa kupenda dunia
Yalikuwa ya kale, najuta.
Refrain
Pasipo Yesu kunitafuta,
Kwa kifo cha aibu
Ni nani, angebeba dhamana?
Ya kutoa maisha, juu yangu.
2. Mwokozi, Mwokozi
Ulitoa uhai, juu yangu
Ukalipa deni langu, Na kutoa aibu yangu
Ukaniweka huru milele
Ukalipa deni langu, Na kutoa aibu yangu
Ukaniweka huru milele.
Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Kurasini Vol 29, Bedi Score, Bedi Lyrics