Watu wanahangaika (Amani) Lyrics, Songs from the Radio
1. Watu wanahangaika, wakitafuta amani
kila sehemu ni vita, pia maombolezo
Wamekwenda kwa waganga, na hata kwao wasomi
Lakini wameikosa, amani iko wapi?
Stanza 1 With articulation/2nd Augmenting voice
Watu wanahangaika (Wahangaika), wakitafuta amani (Amani)
kila sehemu ni vita (Ni vita), pia maombolezo (Maombolezo)
Wamekwenda kwa waganga (Waganga), na hata kwao wasomi (Wasomi)
Lakini wameikosa, amani iko wapi? (Amani iko wapi?)
Refrain
Yesu ndiye kimbilio, lenye amani
Tumtafute Mwokozi, tuweze pata amani
Yeye pekee anaweza, kushinda yote
Tukimbilie kwa Yesu tutapata amani.
2. Na katika familia, amani imetoweka
migongano haiishi, watu wanafarakana
Shetani ametowesha, amani kati ya ndugu,
Ndugu umkaribishe, yeye mwenye amani.
Stanza 2 With articulation/2nd Augmenting voice
Na katika familia (Familia), amani imetoweka (Ooh kweli)
migongano haiishi (Haiishi), watu wanafarakana (Wafarakana)
Shetani ametowesha (ametowesha), amani kati ya ndugu (Amani)
Ndugu umkaribishe yeye mwenye amani (Yeye mwenye amani)
This is from the Radio; Singers not attributed. Attribution could be done later.
2017, Morning Star Radio Tz
Songs from the Radio, Fillers, Attribution Needed, Bedi Score, Bedi Lyrics