Tuesday, 2 June 2026

Ndoa Ilibarikiwa Lyrics sung by Diana Gesare

Ndoa Ilibarikiwa Lyrics sung by Diana Gesare


1. Ndoa ilibarikiwa na Mungu,

Ilianza pale Edeni

Kwani Mungu aliona, si vyema Adamu,

Awe pekee yake msaidizi.


Refrain

Waliounganishwa naye Muumba

Mwanadamu yeyote asiwatenganishe

Kwani siku ya leo ni siku ya raha,

Mnapozifunga pingu za maisha.


2. Ndoa inatuonyesha pendo la Mungu,

Wanandoa mpendane

Katika mambo yote, mmyapitiayo,

Huku mkimtanguliza Muumba.


Diana Gesare.


Diana Gesare, Bedi Score, Bedi Lyrics

Ndugu Unaposema (Ubatizo) Lyrics sung by Diana Gesare

Ndugu Unaposema (Ubatizo) Lyrics sung by Diana Gesare


1. Ndugu unaposema kwamba umebatizwa,

Imekupasa kuyachunguza sana maneno yako

Kwani ubatizo una maana ya kuzamisha,

Alivyozamishwa Mwokozi wetu Yesu mtoni Yorodani

Alivyozamishwa Mwokozi wetu Yesu mtoni Yorodani.


Refrain I

Uzamishwa ndani ya maji, maji yalo mengi

Ni ishara ionyesha kufa na kufufuka.


Refrain II

Ndiyo ubatizo ulio wa kweli,

Hebu na tufuate nyayo za Bwana Yesu.


2. Tuna Baba mmoja, Biblia ni moja, Imani moja

Na njia nayo ni moja, ambayo ni Yesu

Mbona tusizifuate nyayo zake Mwokozi?

Kwa kubatizwa alivyobatizwa Bwana Yesu mtoni Yorodani

Kwa kubatizwa alivyobatizwa Bwana Yesu mtoni Yorodani.


3. Ubatizwapo ndugu, kumbuka ni ishara,

Ya kuyazikwa mambo yale ya zamani yalo ya giza

Ebu mwamini leo ufanye uamuzi

Ili uzaliwe mara ya pili uwe kiumbe kipya

Ili uzaliwe mara ya pili uwe kiumbe kipya.


Diana Gesare.


Diana Gesare, Bedi Score, Bedi Lyrics

Kisa Cha Msalaba Lyrics sung by Diana Gesare

Kisa Cha Msalaba Lyrics sung by Diana Gesare


1. Kisa cha Msalaba chagusa moyo wangu,

Alivyoteseka kwa ajili yangu

Taji ya miba alivikwa Bwana wangu,

Ili mi' na wewe tupate kuokoka.


Refrain

Machozi ya Mwokozi yazidi kutiririka,

Anapotuona tukipotea dhambini,

Anatuita leo kwa sauti ya upole

Fungua moyo aingie.


2. Njiani Goligotha alitembea Bwana

Msalaba mzito ukamlea,

Mkuki ubavuni alichomwa Bwana wangu

Mikononi, miguuni kachomwa misumari.


3. Leo Yesu Mwokozi yu mlangoni mwako,

Akusihi ndugu umpokee maishani

Kwani gharama yetu ya Wokovu alilipa,

Njoo nami leo hii tumfuate Mkombozi.


Diana Gesare.


Diana Gesare, Bedi Score, Bedi Lyrics

Thy Word Lyrics sung by Diana Gesare

Thy Word Lyrics sung by Diana Gesare


1. Thy word is a lamp unto my feet,

And the light unto my path

I'll ever follow you, wherever you take me

Oh Lord, be my own guide.


Refrain

You sent your Son to carry all my burdens,

To die for me that I can be saved.

Lord, give me the strength, to serve thee to the end,

You are one that can help me.


2. Life here on earth,

Is full of trials which come day in day out

People come and go, Seasons come and go,

But your word will forever remain.


3. Your plan-? in me a new soul to serve thee,

To endure all the trials

In all I believe, that by faith,

I won’t have to cross Jordan alone.


For Revision: Stanza Line, Line 4; Your plan to me; Your plan-?: Your plan into me...


Diana Gesare.


Diana Gesare, Bedi Score, For Revision, Bedi Lyrics

Bwana Mungu Muumbaji (Sabato) Lyrics sung by Diana Gesare

Bwana Mungu Muumbaji (Sabato) Lyrics sung by Diana Gesare


1. Bwana Mungu Muumbaji, aliumba vya dunia

Na vya mbingu vyote yeye aliviumba

Kakamilisha kazi yake, baada ya siku sita

Akapumzika Sabato takatifu.


Refrain

Tumshukuru Bwana, Tumwinua Mungu wetu

Kwa uumbaji wa ajabu, tena tukumbuke kwamba

Siku ya Sabato, ndio siku kuu ya ibada.


2. Katika siku hii, usitende kazi yoyote

Kwani ni siku kuu ya mapumziko

We’ pamoja na nyumba yako, hata na watumishi wako

Pia mali yako mkapumzike.


Diana Gesare.


Diana Gesare, Bedi Score, Bedi Lyrics

Usiniache Bwana Lyrics sung by Diana Gesare

Usiniache Bwana Lyrics sung by Diana Gesare


1. Usiniache Bwana mimi ninakuhitaji,

Kwenye safari yangu ya kwenda Mbinguni,

Iliyojawa na mabonde pamoja na milima, usiniache.


Refrain

Wewe ni taa yangu; --We ni taa yangu, We ni taa yangu--

Naomba nimulikie; --Baba nimulikie--

Wewe ni ngome yangu; -- Wewe ni ngome yangu--

Bwana nishike mkono; --Tembea nami Bwana--

Tembea nami Bwana; --Tembea nami Bwana—

Kamwe usiniache; --Tembea nami Bwana—

Tembea nami Bwana –Kamwe/Usiniache--


2. Kwenye safari hii, wengi wakataa tamaa

Wengi wanaiacha imani ya Bwana Yesu

Leo tunakuomba utushike mkono, usituache.


For Revision: Review the the Refrain. Add the vatiation

Diana Gesare.


Diana Gesare, For Revision, Bedi Score, Bedi Lyrics

Bwana Wangu (Nakushukuru) Lyrics sung by Diana Gesare

Bwana Wangu (Nakushukuru) Lyrics sung by Diana Gesare


1. Bwana wangu sijui, Na sina cha kukupa kwa upendo wako

Ulikonitoa hakuna mwanadamu yeyote awezaye kueleza

Lakini kwa upendo wako ulo mkuu, sasa nashukuru.


Refrain

Wakati ule wa giza nene, Moyoni mwangu uliniona eh Bwana

Mimi sikuzitambua njia zako za siri, Nakushukuru Bwana wangu.


2. Sasa nina sababu, ya kulitukuza na kuliinua jina lako eh Bwana

Wakati wa shida u rafiki wa kweli, ambaye namtumainia.


Diana Gesare.


Diana Gesare, Bedi Score, Bedi Lyrics

Ni Machungu Yasononeshayo Lyrics sung by Diana Gesare

Ni Machungu Yasononeshayo Lyrics sung by Diana Gesare


1. Ni machungu yasononeshayo, yatukumbayo ndugu

Tupitiayo humu duniani, kweli yanatisha

Wana wa Mungu wateseka, kila aina ya machungu

Lakini jambo moja linipalo faraja kwamba atarudi

Lakini jambo moja linipalo faraja kwamba atarudi.


Refrain

Bwana wangu ninajua atarudi,

Huu mwili unaoteseka sasa utaisha

Nitavikwa mwili mpya,

Nikiingia Yerusalemi mpya pasipo na mateso

Nikiingia Yerusalemi mpya pasipo na mateso.


2. Wengi wajifanya marafiki, lakini yale watutendeayo,

Kweli yanatisha, Tunaye rafiki wa kweli,

Ambaye ni Yesu Mkombozi

Ameshatuahidi ya kwamba, kamwe yeye hawezi kutuacha

Ameshatuahidi ya kwamba, kamwe yeye hawezi kutuacha.


Refrain

Bwana wangu ninajua atarudi,

Huu mwili unaoteseka sasa utaisha

Nitavikwa mwili mpya,

Nikiingia Yerusalemi mpya pasipo na mateso

Nikiingia Yerusalemi mpya pasipo na mateso.


Outro

Tuwakumbuke Meshaka, Shadrak and Abednego,

Waliporushwa motoni, Bwana aliwashindia

Na sisi leo kweli, tukimwamini Bwana

Atatupa nguvu za kuweza kuyakabili.


Usifadhaike tena, moyoni mwako ndugu

Umwamini Bwana atakushindia,

Yale yote upitiayo yeye anaweza

Atakupa nguvu za kuyakabili kuyakabili

Atakupa nguvu za kuyakabili kuyakabili.


Diana Gesare.


Diana Gesare, Bedi Score, Bedi Lyrics

Haya Tunayoyaona Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Haya Tunayoyaona Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Haya tunayoyaona, Yanayotupendeza

Yanayotuhangaisha, Yote yatapita, Yote yatapita.


Refrain

Tafuta uzima kwanza, Ya dunia yanapita

Heri maskini wa roho, Watamuona Bwana.


2. Ndio ahadi ya Bwana, Kwa wanaomwamini

Leo watafadhaika, Kesho ni furaha, Kesho ni furaha.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 28, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Kama Nilivyotumwa Duniani Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Kama Nilivyotumwa Duniani Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


Refrain

Kama nilivyotumwa duniani, Nami pia ninawatuma ninyi

Enendeni ulimwenguni mwote, Wahubirini waokoke

Ulimwenguni mtaona dhiki (Jipe moyo), Nipo nanyi siku zote

Nani ataweza kusimama,

Pasipo ‘tegemea Bwana Yesu? Jipeni moyo.


1. Ushindi na Yesu ni hakika, alisema mwenyewe

Niite wakati wa taabu, nami nitaitika

Yale magumu msiyoyaweza nitawafunulia.


2. Mimi nimeshinda ulimwengu, Nimepewa mamlaka

Nitawapa roho mtakatifu, -? Msaidizi

Mbinguni wanasifu ukombozi, U mikono ni mwake.


For Revision: Stanza 2, Line 2; Nitawapa roho mtakatifu, -? Msaidizi'; Kama msaidizi, Omba msaidizi


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 28, For Revision, Bedi Score, Bedi Lyrics

Aliacha Utukufu Wake Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Aliacha Utukufu Wake Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Aliacha utukufu wake, Kwa ajili yangu mdhambi

Akaitwa Imanueli, Mungu pamoja na wanadamu.


Refrain

Akashuka duniani, Akashuka kaburini

Simba wa Yuda ni jina lake, Mungu pamoja na wanadamu.


2. Ni msaada ulio karibu, Ni yote katika yote

Yeye kwetu ndiye kimbilio, Mungu pamoja na wanadamu.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 28, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Ninaye Rafiki Wa Thamani Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Ninaye Rafiki Wa Thamani Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Ninaye rafiki wa thamani, Anipendaye tena mlinzi mwema

Japo mwovu anitenge naye, Hunirejesha kwa upole mwingi

Huniwezesha kutafakari, Nafsi yangu itangapo mbali naye.


Refrain

Je nani wa kunitenganisha na Mwokozi wangu? (Kwa kweli)

Hunitunza vyema hunipa furaha moyoni.


2. Ninaye rafiki wa thamani, Mlinzi wangu bondeni mwa mauti

Adui ajapo mbele yangu, Hunilinda niwapo mashakani

Hunihuhisha huniongoza Nimtegemeapo ninafarijika.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 28, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Umemgusa Bwana Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Umemgusa Bwana Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Umemgusa Bwana maishani mwako

Umeketi naye mezani

Yaliyo magumu amekuonyesha

Umekuwa kiumbe kipya

Umekuwa kiumbe kipya.


Refrain

Umemgusa Bwana umebadilika

Maisha ya kale yamebadilika

Umemgusa Bwana, umeona nuru

Umekuwa kiumbe kipya

Umekuwa kiumbe kipya.


2. Wanaheri wale walomgusa Yesu

Wameponywa mioyo kwa damu

Mawimbi yakija hawatatikiswa

Wamejenga juu ya mwamba mwamba

Wamejenga juu ya mwamba mwamba.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 28, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Pale kaburini (Yu Hai) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Pale kaburini (Yu Hai) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Pale kaburini, Yesu kalala

Neno litimiye, Kafufuka!


Refrain

Neno likatimia hayupo kaburini tena (Hayupo!)

Ameketi juu na malaika

Ameshinda mauti ni mfalme

Yu hai! Yu hai! Ameshinda mauti!


2. Askari wakesha, Kwenye kaburi

Wanakesha bure, Kaburini!


NZK NO. 246 Mle Kaburini, Yesu Mwokozi.


1. Mle kaburini, Yesu Mwokozi!

Alilazwa chini, Bwana wangu!


Refrain

Bwana! Amefufuka, Kifo kimeshindwa kabisa!

Gizani mle alitoka chini, Sasa atawala huko Mbinguni!

Yu hai! Yu hai! Bwana Yesu yu hai!


2. Aungoja huo, Yesu Mwokozi!

Mchana ujao, Bwana wangu!


3.Walinda kaburi, Yesu Mwokozi!

Bure ni muhuri, Bwana wangu!


4.Kifo kimeshindwa, Yesu mwokozi!

Pingu zimevunjwa, Bwana wangu!


NOTES

1 Wakorintho 15:55 "Kuko wapi Ewe mauti kushinda kwako? Uko wapi Ewe mauti uchungu wako?"


This version is done by Kurasini and could be picked from other Kiswahili Hymnal Books.


From: Nyimbo Za Kristo No. 246, Pale Kaburini

English Version: Songs For Worship (SFW) No. 741, Christ Arose

Writer: Robert Lowry

Composer: Emily D. Wilson (1898), TUNE Name: HEAVEN


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 28, Swahili Hymns, Bedi Score, Bedi Lyrics

Imbeni Pendo (Tukifika Mbinguni) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Imbeni Pendo (Tukifika Mbinguni) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Imbeni pendo lake Yesu upendo wa ajabu,

Katika makao mapya tutaishi milele.


Refrain

Tukifika mbinguni, Ni siku kuu yenye furaha

Tukimwona Yesu, Tutakuwa ni washindi.


2. Shangwe kuu vigelegele vitapigwa angani (Kweli)

Hakuna huzuni tena kutawala na Yesu.


Php 3.

From: SDAH No. 663, When We All Get to Heaven; Tukifika Mbinguni.

Writer: Eliza Edmunds Hewitt.

Composer: Emily D. Wilson (1898), TUNE Name: HEAVEN


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 28, Swahili Hymns, Bedi Score, Bedi Lyrics

Kazi Ni Yako Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Kazi Ni Yako Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Kazi ni yako tunayoifanya,

Hakuna awezaye kuizuiya

Tumeisikia sauti yako,

Hakuna awezaye kuizuiya.


Refrain

Kwa machozi mengi shambani mwa Bwana

Watumishi wako wapanda juani

Mawimbi makali kwenye mapambano

Nyosha mkono utushike.


2. Tupe ujasiri shambani mwako,

Wapandao juani wape nguvu

Wasirudi nyuma shambani mwako,

Taji zinawangoja muda kitambo.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 28, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Namwandama Bwana Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Namwandama Bwana Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Namwandama Bwana kila siku,

Yapitayo naacha nasafiri

Kwa muda kitambo,

Nimuone Yesu, kwenye utukufu.


Refrain

Siku ikifika nimuone Yesu,

Kwenye utukufu

Ulimwengu huu hautakumbukwa,

Kwenye utukufu.


2. Namwandama Bwana angali juu,

Nione utukufu sitachoka

Katika makao,

Nami niwepo, kwenye utukufu.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 28, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Siwezi Pekee Yangu Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Siwezi Pekee Yangu Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Siwezi pekee yangu kuibeba,

Mizigo yangu hadi nyumbani

Ninaye Yesu rafiki mwema,

Mizigo yangu ataibeba.


Refrain

Ndiye mwamba ngome yangu,

Yeye ni faraja yangu, siku zote

Kwake ninasimama,

Ndiye mwamba ni salama

Ndiye mwamba ni salama,

Yesu ndiye mwamba ni salama.


2. Njiani hurahisisha safari,

Mbele yangu ni matumaini

Niwezeshe kuona wema wako,

Daima nisione huzuni.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 28, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Najuta Kwa Kuwazia (Nimeamua Kumfuata Yesu) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


Najuta Kwa Kuwazia (Nimeamua Kumfuata Yesu) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Najuta kwa kuwazia,

Maumivu na matatizo ya maisha

Nimepoteza wakati, Kwa kung'ang'ania,

Mambo nisiyoweza.


Refrain

Nimeamua kumfuata Yesu,

Sitamani mambo ya zamani

Rehema zake kwangu zimenipa furaha

Nasonga mbele naye Yesu yuko nami.


2. Naacha kuwalaumu,

Na kuwachukia watu na matukio

Mzigo wa hatia,

Nimeutua na Yesu kanipa furaha.


3. Nakubali badiliko,

La maisha yangu na mimi natambua

Bwana Yesu amefanya makao,

Ndani yangu, Nimeumbwa upya.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir, Kurasini Vol 28, Bedi Score, Bedi Lyrics

Wengi Walio Dhambini Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Wengi Walio Dhambini Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Wengi walio dhambini, Wamekata tamaa

Nani atakaye waokoa, Wapate nuru ya Bwana

Wamuone Yesu, warudi kumdhili waokolewe

Wajulisheni habari za Yesu, warejee.


Refrain

Wainueni Bwana yuaja (Wainue),

Wapate nuru toka mbinguni (Juu)

Walioao wawe watulivu,

Wamrudie Mungu Mwokozi yupo huwangojea.


2. Tulipotanga dhambini Mungu alitupenda

Kwa nguvu zetu tusingeweza, Gharama ya ukombozi

Damu ya Yesu, Goligotha Mwokozi aliteswa

Gethsemani dhambi zilimlemea, tuwe huru.


NOTES/For Revision

Stanza 1, Line 3; Add context and meaning of kumdhili as used here and even in Isaiah 9:6.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 28, Kurasini Classics, For Revision, Bedi Score, Bedi Lyrics

Usiku Wakaribia Lyrics Sung by Kurasini SDA Choir

Usiku Wakaribia Lyrics Sung by Kurasini SDA Choir


1. Usiku wakaribia, giza limesogea

Hakuna matumaini moyoni

Imani imetoweka, umekosa faraja

Inua uso wake juu kwake Yesu.


Refrain

Sio mbali (Sio mbali),

Kwapambazuka, Giza itatoweka,

Nuru njema (Nuru njema), toka kwa Yesu,

Itaondoa giza hili.


2. Mazito uyaonayo kuna msaada kwa Yesu

Fungua moyo wako aingie

Sumbuko la moyo wako Yesu ataondoa

Inua uso wake juu kwake Yesu.


NOTES

Sio mbali (Sio mbali), Kwapambazuka, Giza itatoweka; It's not long before dawn. (Kwapambazuka)

Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 27, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Hukumu Ikapita (Usiku Ule Wa Huzuni) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Hukumu Ikapita (Usiku Ule Wa Huzuni) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Hukumu ikapita, Hukumu ya kifo

Watu washangilia, Sauti ya Mwokozi

Ikawashangaza, ‘Baba, uwasamehe.’


Refrain

Usiku ule wa huzuni, Nyota zikatiwa giza

Nao mwezi angani, Ukawa giza,

Yesu akabili kifo.


2. Pilato akasema, ‘Sioni hatia,

Juu ya mtu huyu,’ Kelele kasikika

‘Damu ya mtu huyu, Na iwe juu yetu.’


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 27, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Umekwisha Sikia Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Umekwisha Sikia Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Umekwisha sikia kisa cha Musa,

Habari za Daudi na Kombeo,

Kisa cha Yusufu na ndoto zake,

Na Yona ndani ya tumbo la samaki,

Pamoja na wengi wa siku za kale

Ninatamani kuonana nao,

Kwa uwezo wa Bwana nitawaona, siku ile ajapo.


Refrain

Kutakuwa na mkutano juu angani, Bwana anaporudi

Tutakutana kule pamoja nyumbani juu angani

Tutaimba wimbo wa Musa na Mwanakondoo,

Siku ile ya utukufu

Naye Yesu atatuongoza, tukikutana sote.


2. Mambo mengi yatakosekana pale,

Hakutakuwepo maombolezo,

Hakuna tena Wokovu kwa wadhambi,

Wito wa Yesu waliukataa

Hakuna huzuni hakuna upweke

Hakuna mizigo tena mioyoni

Hayo yote Bwana Yesu atafuta, siku ile ajapo.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 27, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Zamani Watoto (Soma Soma) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Zamani Watoto (Soma Soma) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


Pre-Verse

Zamani watoto walikwenda kwa Yesu,

Yesu kawabariki

Wanafunzi walitaka kuwazuia,

Yesu kawakemea.


1. Tafuta elimu usiiachi, Itakuacha mbali ndugu

Elimu ni chanzo cha kumjua Mungu,

Wapee watoto elimu, wamjue Mungu

‘Waache waje kwangu,’ asema Bwana.


Refrain

Tafuta elimu ndugu,

---Soma, soma, soma

Upate kumjua Mungu,

---Soma, soma, soma

Utapeleka injili,

Nenda watu waangamia kwa kukosa maarifa.


2. Elimu ufunguo wa maisha, Tuwape watoto elimu,

Leeni watoto kwa njia ipasayo,

Nao hawatasahau, wamjue Mungu

‘Waache waje kwangu,’ asema Bwana.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 27, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Alfajiri, Shangwe Zasikika Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Alfajiri, Shangwe Zasikika Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Alfajiri, Shangwe zasikika,

Toka kaburini, Haleluya!

Alfajiri, Yesu kafufuka,

Kristo ameshinda mauti.


Refrain

(Shangilia, Shangilia,

Shangilia, Shangilia,

Mwokozi amefufuka) x4


Kristo ameshinda mauti.


2. Alfajiri, Panda italia

Tumlaki Mwokozi, Haleluya

Makaburi, yatafunguliwa,

-? Wafu watafufuka.


Refrain

Refrain

(Shangilia, Shangilia,

Shangilia, Shangilia,

Mwokozi amefufuka) x4


Kristo ameshinda mauti.


Refrain

(Shangilia, Shangilia,

Shangilia, Shangilia,

Mwokozi amefufuka) x4


Kristo ameshinda mauti.


For Revision: Stanza 2, Line 4; -? Wafu watafufuka.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 27, Kurasini Classics, For Revision, Bedi Score, Bedi Lyrics

Nipe Neno Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Nipe Neno Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Nipe neno lenye uzima,

Liwe ni ngao msaada kwangu

Neno lile la Manabi,

Liwe ni nuru ya njia yangu.


Refrain

Neno la uzima Faraja kwangu

Nipe neno lenye uzima

Neno la Mitume na Manabi,

Liwe ni nuru ya njia yangu.


2. Neno hili tangu zamani,

Halitabadilika milele

Yesu yule, yule wa jana,

Ndiye wa leo, ndiye ajaaye.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 27, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Nikaona Jeshi Kubwa Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Nikaona Jeshi Kubwa Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Nikaona jeshi kubwa la ajabu,

Wateule, wakikaribishwa kwa furaha,

Wameshinda, ushindi ni wake Bwana Yesu

Angaza, angaza kote uone,

Ushindi u mikononi mwake,

Anatuita leo twende tuokolewe,

Kuolewa ni wito kwako.


2. Ni mnyenyekevu tena mpole

Atakaye enda aje, awe mshindi

Matumaini yako yataonekana wazi

Nani ajuaye ya kesho ila Mwokozi

Huko Mbinguni wangoja,

Wanaomtumaini watauridhi ufalme

Utakuwepo pale,

Ufalme wenye nguvu, Umewekwa tayari.


3. Matumaini Ufalme usio na mwisho

Utakuwepo pale,

Ufalme wenye nguvu, Umewekwa tayari

Matumaini ufalme usio na mwisho

Utakuwepo pale,

Ufalme wenye nguvu, Umewekwa tayari.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 27, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Nenda Useme Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Nenda Useme  Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Nenda useme; Kwa wote

Useme; Wasikie

Habari njema; Ya Wokovu

Useme; Wasikia

Usinyamanze; Wapo wengi wamezama dhambini,

Sema wote wasikie, wote wasikie Habari njema.


Refrain

Enendeni mhubiri injili, Enendeni bado kuna nafasi

(Sema), Siku zaja mtakosa nafasi

Sema wote wasikie, wote wasikie Habari njema.


2. Paza sauti; Useme

Kwa wote; Wasikie

Kwa kila lugha; Na jamaa

Watubu; Warejee

Liseme tele; Mbinguni pamoja arejeapo

Sema wote wasikie, wote wasikie Habari njema.


Refrain

Enendeni mhubiri injili, Enendeni bado kuna nafasi

(Sema), Siku zaja mtakosa nafasi

Sema wote wasikie, wote wasikie Habari njema.


Refrain (Outro)

Enendeni mhubiri injili, Enendeni bado kuna nafasi

(Sema), Siku zaja mtakosa nafasi

Sema wote wasikie, wote wasikie

Wote wasikie, wote wasikie Habari njema.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 27, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Karibu Nawe Bwana Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Karibu Nawe Bwana Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


Pre-Verse

Karibu nawe Bwana,

Huzuni zangu zitakoma,

Moyoni nina raha


1. Nimesongwa na dhambi,

Unionyeshe wema wako

Ulipo nami niwepo,

Nakuhitaji; Yesu.


Refrain

Mikononi mwako nina-?,

Dhoruba kali zikinilemelea,

Nayaweza yote mimi mdhambi,

Unaponitia nguvu; Yesu.


Pre-Verse

Karibu nawe Bwana,

Huzuni zangu zitakoma,

Moyoni nina raha


2. Nimezama dhambini,

Wewe tu pekee wanitosha

Unioshe niwe safi,

Nakuhitaji; Yesu.


For Revision: Mikononi mwako nina-?; Where I find shelter; kimbilio. Not clear. Nina-Amani?


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 27, Kurasini Classics, For Revision, Bedi Score, Bedi Lyrics

Kando Kando Ya Bahari Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Kando Kando Ya Bahari Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Kando kando ya bahari ya kioo, tutakaa siku zote

Hakuna huzuni ni furaha tele, Kutawala na Bwana.


Refrain

Shangwe tele kando kando ya Bahari,

Kwenye bustani nzuri ya Mungu

Ni furaha, furaha isiyo mwisho,

Kutawala Bwana.


2. Siku ikifika kuaga dunia, Furaha na shangwe tele

Mambo ya zamani, Tutayasahau kutawala na Bwana.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 27, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Kamwe Sitaacha Kumtumikia Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Kamwe Sitaacha Kumtumikia Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Kamwe sitaacha kumtumikia, Nimeona baraka zake

Amenifichia aibu yangu, Kati ya watesi wangu

Hata sasa sijapungukiwa, Mezani nabarikiwa

Ajua mavazi nivaayo, Viatu miguuni.


Refrain

Majumba, Umetupa,

Magari, Umetupa

Watoto, Umeshatupa,

Haleluya! Twakusifu,

Eeh Bwana, Tubariki.


2. Dunia na vyote viijaavyo, Vyote ni mali yako Bwana

Umekubali viwe milki yetu, Upendo wa jinsi gani

Kikombe changu kinafurika, Watesi wanishangaa

Umenikumbatia mkononi, Rahani napumzika.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 27, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Ee Moyo Wangu Tulia Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Ee Moyo Wangu Tulia Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


Refrain

Ee moyo wangu tulia kwa Bwana,

Tulia kwa Bwana moyo wangu

Kwa kuwa siku zote Kristo ngome yangu,

Kimbilio wakati wa taabu.


1. Nimechoka kutanga dhambini (Oh dhambini)

Sasa narudi, narudi nyumbani

Nimeona nuru ya Yesu

Nimechoka kutanga dhambini.


2. Nimekuwa mtumwa dhambini (Oh dhambini)

Nimesikia habari za Yesu

Mjoli wangu ameniita

Nimechoka kutanga dhambini.


NOTES

Mjoli wangu ameniita; Mjoli means a fellow worker, a partner, or someone who shares the exact same task, calling, or mission as you. Christ is a fellow worker in the service to search fellow workers.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 27, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Bwana Naomba Roho Wako Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Bwana Naomba Roho Wako Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Bwana naomba roho wako,

Aingie moyoni mwangu, Nami nikutukuze

Unionyeshe wema wako,

Unifundishe pendo lako, Nami nikutukuze.


Refrain

Bwana naomba unisikilize,

Ninahitaji unijaze na roho

Uwashe moto ndani yangu,

Watu wa dunia wajue, Kwamba wewe ni Bwana.


2. Kama wakati wa mitume,

Bwana uliwajaza roho, Na wakashuhudia

Na nguvu kutoka mbinguni,

Watu wengi waliokoka, Bwana ulitukuzwa.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 27, Bedi Score, Bedi Lyrics

Bado Kitambo Kidogo Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Bado Kitambo Kidogo Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Bado kitambo kidogo, Usife moyo (Usife moyo)

Mapambazuko karibu, Usife moyo (Usife moyo).


Refrain

Makao ni mengi, Yamekwisha andaliwa,

Kwa kila familia, Ya karibishwa mbinguni,

Ujipe moyo ndugu, Kamwe usirudi nyuma,

Bado kitambo kidogo, Kuisha mwendo!


2. Bado kitambo kidogo, Tutapumzika

Miguuni pa Mwokozi, Kwenye makao.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 27, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Vumilia Sirudi Nyuma Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Vumilia Sirudi Nyuma Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


Prelude

Vumilia! Sirudi nyuma.


1. Kwa muda mrefu, Wamsubiri Mwokozi

Arudi kutuchukua,

Ahadi ya kuja alisema mwenyewe,

"Msifadhaike mioyo."


Refrain

Vumilia! Sirudi nyuma,

Kaza mwendo jipe moyo

Vumilia! Sirudi nyuma,

Pambazuko liko karibu.


2. Safari ni ngumu, Mapambano makali

Njiani vikwazo vingi,

Pasipo msaada wa Bwana toka juu,

Ni wazi 'tarudi nyuma.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 26, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Hukutambua Uzito Wa Msalaba Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Hukutambua Uzito Wa Msalaba Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Hukutambua uzito wa Msalaba

Wajiuliza huwezi kujua (Kujua)

Jambo moja ninajua Mwokozi,

Uzito ukamlemea.


Refrain

“Sasa ninaona kiu,”

Yesu alia msalabani,

“Kikombe hiki, kiniepuke vipi?”

Yote ni kwa ajili yetu.


2. Hukutambua fedheha za Msalaba,

Wala kujua maumivu yake (Kujua)

Akachomwa misumari mkononi,

Mkuki ubavuni mwake.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 26, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Nipo Bwana Nitume Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Nipo Bwana Nitume Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Nipo Bwana nitume, Ni tayari Kwenda

Ila mbele yangu, Kuna vikwazo vingi


Refrain

Ukutaa huu, Bwana ubomoe,

Na kwa mapenzi yako, Niweze kupita

Ukuta huu, Bwana mpaka lini?

Utatuweka huru, Njia iwe wazi?


3. Sina uwezo Bwana, Juu ya ukuta huu

Umenizuia, Nisiweze kuvuka.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 26, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Aniongozaye Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Aniongozaye Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


Prelude

Aniongozaye, amenipa nguvu

Kuwa na Yesu, Ni Eli.


Refrain

Ninafurahishwa nawe wakati wa raha

Yakiwapo majaribu, hunitia nguvu

Neno lako lanitosha, Uniongoze

Pekee yangu siwezi, Nitaanguka.


1. Uliponitafuta sikutambua

Uliponong’oneza ningejua aje?

Bila wito wa Yesu ningepotea

Nafurahi ni huru namjua Mungu.


Refrain

Ninafurahishwa nawe wakati wa raha

Yakiwapo majaribu, hunitia nguvu

Neno lako lanitosha, Uniongoze

Pekee yangu siwezi, Nitaanguka.


2. Ninapo dhaminia kurudi kwako

Ninapotaabishwa na machafuko

Nakumbuka zilivyo huruma zako

Nafurahi ni huru kuwa na wewe.


Refrain

Ninafurahishwa nawe wakati wa raha

Yakiwapo majaribu, hunitia nguvu

Neno lako lanitosha, Uniongoze

Pekee yangu siwezi, Nitaanguka.


Outro

Aniongozaye, amenipa nguvu

Kuwa na Yesu, Ni Eli.


NOTES

Prelude & Outro: Line 2; Kuwa na Yesu, Ni Eli...


Eli, Eli, lama sabakthani? maana yake; Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 26, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Tangu Nimjue Yesu Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Tangu Nimjue Yesu Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Tangu nimjue Yesu, Na kumkaribisha moyoni mwangu

Yalopita yamepita, Na kuvaa utu upya ndani yangu

Sijiitaabishi tena, Ya kale hayana nafasi kwangu

Nimevikwa utu upya, Nimekuwa kiumbe ndani ya Yesu.


Refrain

Utu wangu wa zamani, Umezikwa na kuvaa utu upya

Sikumbuki ya zamani, Yesu yu ndani yangu

Nakimbilia Wokovu, Kwa sasa yalopita yamepita

Dunia kwaheri, Yalopita yamepita.


2. Maisha ndani ya Yesu, Ni raha isiyokuwa kifani

Magumu hurahisishwa, Yatoweka kwa jinsi usiyojua 

Mambo yote ya zamani, Hayakumbukwi tena maishani

Mpe Yesu moyo wako, Utaona yote yawezekana.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 26, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Nimesikia Wito (Naja Kwako) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Nimesikia Wito (Naja Kwako) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Nimesikia wito wako Bwana,

Ukiniita mdhambi nisafishwe

Kwa damu ya thamani ya Kalvari,

Iliyomwagika kwa watu wote.


Refrain

Naja kwako nisiyestahili,

Naja kwako mimi mdhambi

Naja kwako Bwana nipokee

Miguuni pako ni ngome yangu.


2. Ingawa ninajua mbele yangu,

Mapambano makali yaja kwangu

Kristo ni vyote kwangu sina hofu,

Ni jibu kwa mashaka mbele yangu.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 26, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Makaoni Mbinguni (Njia Iliyo Njema) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Makaoni Mbinguni (Njia Iliyo Njema) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Makaoni Mbinguni,

Tutakaposujudu mbele zake Mungu 

Tutaikumbuka, Njia iliyo njema,

Waliopitia zamani, Wazee wa imani (Imani).


2. Siku yenye mibaraka tele,

Ilibarikiwa na Mungu hapo mwanzo

Ilibarikiwa naye Mungu, Njia iliyo njema,

Waliopitia zamani, Wazee wa imani (Imani).


3. Siku ya saba, ilitakaswa

Ndio ishara, Kati ya Mungu na wamchao

Ilibarikiwa na Mungu hapo mwanzo.


4. Mbinguni

---(Mbinguni pa Mungu juu)

Tutaikumbuka

Ilibarikiwa hapo mwanzoni.


4b. Mbinguni

---(Mbinguni pa Mungu juu)

Tutaikumbuka

Ilibarikiwa hapo mwanzoni.


5. Siku yenye matumaini,

Kwa watu wake Mungu

Njia iliyo njema, Waliopitia zamani,

Waliomwamini, Walitetea imani hata kufa

Ilibarikiwa na Mungu hapo mwanzo.


6. Kwa watu wake Mungu

Njia iliyo njema, Waliopitia zamani,

Waliomwamini, Walitetea imani hata kufa

Ilibarikiwa na Mungu hapo mwanzo.


7. Tukifika Mbinguni, Mbele zake Mungu

Nyuso zenye furaha, Pamoja na Yesu.


Tukifika Mbinguni, Mbele zake Mungu

Nyuso zenye furaha, Pamoja na Yesu.


Njia iliyo njema,

Waliopitia zamani, Wazee wa Imani.


8. Tukifika Mbinguni, Mbele zake Mungu

Nyuso zenye furaha, Pamoja na Yesu.


Tukifika Mbinguni, Mbele zake Mungu

Nyuso zenye furaha, Pamoja na Yesu.


Njia iliyo njema,

Waliopitia zamani, Wazee wa Imani.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 26, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Itakuwa Siku Ya Ajabu (Tuonane Ng'ambo Ile) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Itakuwa Siku Ya Ajabu (Tuonane Ng'ambo Ile) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Itakuwa siku ya ajabu,

Baada ya kusafiri sana

Pale ng'ambo ya mto Yordani,

Tutaonana kwa furaha.


Refrain

Ni furaha tele siku hiyo,

Jeshi la Mbingu likitulaki (Tulaki)

Kisa cha Wokovu twasimulia (Simulia),

Kwenye Bahari ya kioo (Kioo)


Yeye bado atatufuta machozi,

Hatutazikumbuka tena (Kumbuka)

Tukiwa ni washindi, Kutawala na Yesu

Tuonane ng'ambo ile ndugu (Tuonane).


2. Sasa siwezi sema hakika,

Ninajua siku i karibu

Ninao wito kwako kwa hakika,

Ujiunge tuonane mbinguni.


NOTES

If We Never Meet Again/I Will Meet You On That Beautiful Shore is a gospel made popular by Elvis Presley here sung by Kurasini SDA Choir, a Swahili rendition, "Itakuwa Siku Ya Ajabu (Tuonane Ng'ambo Ile)"


Writer & Composer: Albert E. Brumley

Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 26, Swahili Hymns, Bedi Score, Bedi Lyrics

Nani Wa Kulinganishwa Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Nani Wa Kulinganishwa Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


Prelude

Nani wa kulinganishwa na Yesu?

Ni wa kwanza


1.Muda mwingi nilikaa, Nikiwa gerezani

Nikamkosa mdhamini, Wakunifungulia.


Refrain

Sauti zilisikika, Nani wakunifungulia?

Ni Yesu mwenye huruma, Kaingia gharama.


2. Katika gereza langu, sikupata nafasi

Langoni alisimama wakuniangamiza.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 26, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Jehova, Jehova Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Jehova, Jehova Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


Refrain

Jehova, Jehova, (-aah)

Jehova, Jehova, (-ah)

Jehova, Sikia kilio cha waja wako

Dunia huzuni

Dunia kilio

Iko wapi, amani?

Ndio maana twaja kwako!


Bridge (Hums)

Uh-uh-uh Uh-uh=uh

Uh-uh-uh Uh-uh=uh

Uh-uh Uh-uh, Uh-uh=uh?

Uh-uh Uh-uh Uh-uh Uh-uh.


Verse 1

Maisha ni bure; Maisha

Maisha ni bure

Yamejaa huzuni, taabu, maombolezo


Refrain

Jehova, Jehova, (-aah)

Jehova, Jehova, (-ah)

Jehova, Sikia kilio cha waja wako

Dunia huzuni

Dunia kilio

Iko wapi, amani?

Ndio maana twaja kwako!


Verse 2

Dunia ni kilio; Oh kilio

Hapafai tena

Watu hawaelewani

Majumbani kilio,

Wamechoka maisha,

Wamekosa jibu,

Tunayo habari njema,

Itokaayo kwa Yesu.


Refrain

Jehova, Jehova, (-aah)

Jehova, Jehova, (-ah)

Jehova, Sikia kilio cha waja wako

Dunia huzuni, Dunia kilio

Iko wapi, amani?

Ndio maana twaja kwako!


Bridge (Hums)

Uh-uh-uh Uh-uh=uh

Uh-uh-uh Uh-uh=uh

Uh-uh Uh-uh, Uh-uh=uh?

Uh-uh Uh-uh Uh-uh Uh-uh.


Outro

Ndio maana twaja kwako!

Ndio maana twaja kwako!

Ndio maana twaja kwako!


NOTES

(Humming of the bridges can be done in the same phasing as the melody of Line 1, 2 & 3 of Refrain, or Line 4, 5 & 6 of the Refrain.


Refrain

Jehova, Jehova, (-aah)

Jehova, Jehova, (-ah)

Jehova, Sikia kilio cha waja wako


OR

Dunia huzuni, Dunia kilio

Iko wapi, amani?

Ndio maana twaja kwako!


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 26, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Kwa Imani Eliya Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Kwa Imani Eliya Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Kwa imani Eliya, akapaa juu Mbinguni,

Na watu wakimuona,

Upepo wa kisulisuli ukamchukua,

Akapaa juu.


Refrain I

(Akapaa), Akapaa juu, Paa juu

Katika gari la moto

Tukiwa na imani (Imani),

Tutapaa juu.


2. Ijapo iwe ndogo, imani katika Bwana,

Yatosha kwenye vita,

Vyote vitawezekana katika imani,

Tutapaa juu.


Refrain II

(Tutapaa), Tutapaa juu, Kwa imani,

Tukiruka juu angani,

Tukiwa na imani (Imani),

Tutapaa juu.


Outro

Tutapaa juu.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 26, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Ungeimba Wimbo Wa Sifa Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Ungeimba Wimbo Wa Sifa Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Ungeimba wimbo wa sifa, ukimsifu Mungu wetu

Lakini bado hujaimba wa Mwanakondoo,

Ukimsifu Mkombozi ukiwa naye

Lakini bado hujaimba wa Mwanakondoo,

Ukimsifu Mkombozi ukiwa naye.


Refrain

Nitapiga tarumbeta (Tarumbeta)

Nitapiga na kinubi (Na kinubi)

Nitapiga zeze langu,

Kuimba wimbo mpya (Oh Haleluya)

Tulia eh moyo wangu (Moyo wangu)

Tulia katika Bwana (Tulia kwa Bwana)

Tulia moyo wangu, Miguuni pa Yesu.


2. Kinyonge hakitaingia, kuimba wimbo ule mpya

Utengeneza mambo yako, una nafasi

Mapambazuko ni karibu, mfalme aja

Utengeneza mambo yako, una nafasi

Mapambazuko ni karibu, mfalme aja.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 26, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Tukaribie Msalaba Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Tukaribie Msalaba Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


Refrain

Tukaribie msalaba, Mti uletao uzima,

Msalaba, Msalaba wa Kalvari

Damu yake inatakasa.


1. Mliosumbuka kwa miaka mingi; Damu yake inatakasa

Yesu anawaita wote; Damu yake inatasa

Mliosumbuka na kulemewa; Damu yake inatakasa

Yesu anawaita wote; Damu yake inatakasa.


Refrain

Tukaribie msalaba, Mti uletao uzima,

Msalaba, Msalaba wa Kalvari

Damu yake inatakasa.


2. Mbona mnasita kuja kwa Yesu? Damu yake inatakasa

Kwa huruma anakuita; Damu yake inatakasa

Masumbuko yako umtwishe leo; Damu yake inatakasa

Yesu anawaita wote; Damu yake inatakasa.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 26, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Ninapofikiria Bustani Ya Edeni Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Ninapofikiria Bustani Ya Edeni Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


Refrain

Ninapofikiria Bustani ya Edeni,

Ilivyopambwa vizuri, Yapendeza macho,

Mito yatiririka, Mambo yote ni mazuri

Mungu akiwapo kati yao kila siku.


Verse

Dhambi ikapendeza na kuharibu Edeni

Utukufu wa Mungu ukatoweka kabisa,

Hofu ikatawala, uovu ukazidi

Ulinzi ukatoweka, bustanini.


Refrain

Ninapofikiria Bustani ya Edeni,

Ilivyopambwa vizuri, Yapendeza macho,

Mito yatiririka, Mambo yote ni mazuri

Mungu akiwapo kati yao kila siku.


Verse (Outro)

Lakini jambo moja niwaambieni mjue

Tutaiona tena Bustani hiyo nzuri,

Iliyojawa na nuru (Ya mbinguni) siku zote


Tutaiona tena Bustani hiyo nzuri,

Iliyojawa na nuru (Ya Mbingu) siku zote.


Tutaiona tena Bustani hiyo nzuri,

Iliyojawa na nuru (Ya mbinguni) siku zote

Tutaiona tena Bustani hiyo nzuri,

Iliyojawa na nuru (Ya mbinguni) siku zote.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Vol 26, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Ndoa Ilibarikiwa Lyrics sung by Diana Gesare

Ndoa Ilibarikiwa Lyrics sung by Diana Gesare 1. Ndoa ilibarikiwa na Mungu , Ilianza pale Edeni Kwani Mungu aliona, si vyema Adamu , Awe pek...