Tangu Nimjue Yesu Lyrics sung by Kurasini SDA Choir
1. Tangu nimjue Yesu, Na kumkaribisha moyoni mwangu
Yalopita yamepita, Na kuvaa utu upya ndani yangu
Sijiitaabishi tena, Ya kale hayana nafasi kwangu
Nimevikwa utu upya, Nimekuwa kiumbe ndani ya Yesu.
Refrain
Utu wangu wa zamani, Umezikwa na kuvaa utu upya
Sikumbuki ya zamani, Yesu yu ndani yangu
Nakimbilia Wokovu, Kwa sasa yalopita yamepita
Dunia kwaheri, Yalopita yamepita.
2. Maisha ndani ya Yesu, Ni raha isiyokuwa kifani
Magumu hurahisishwa, Yatoweka kwa jinsi usiyojua
Mambo yote ya zamani, Hayakumbukwi tena maishani
Mpe Yesu moyo wako, Utaona yote yawezekana.
Kurasini SDA Choir.
Kurasini SDA Choir Vol 26, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics