Umekwisha Sikia Lyrics sung by Kurasini SDA Choir
1. Umekwisha sikia kisa cha Musa,
Habari za Daudi na Kombeo,
Kisa cha Yusufu na ndoto zake,
Na Yona ndani ya tumbo la samaki,
Pamoja na wengi wa siku za kale
Ninatamani kuonana nao,
Kwa uwezo wa Bwana nitawaona, siku ile ajapo.
Refrain
Kutakuwa na mkutano juu angani, Bwana anaporudi
Tutakutana kule pamoja nyumbani juu angani
Tutaimba wimbo wa Musa na Mwanakondoo,
Siku ile ya utukufu
Naye Yesu atatuongoza, tukikutana sote.
2. Mambo mengi yatakosekana pale,
Hakutakuwepo maombolezo,
Hakuna tena Wokovu kwa wadhambi,
Wito wa Yesu waliukataa
Hakuna huzuni hakuna upweke
Hakuna mizigo tena mioyoni
Hayo yote Bwana Yesu atafuta, siku ile ajapo.
Kurasini SDA Choir.
Kurasini SDA Choir Vol 27, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics