Wednesday, 10 June 2026

Mbingu Zilikaa Kimya (Kutafuta Mkombozi) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Mbingu Zilikaa Kimya (Kutafuta Mkombozi) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Mbingu zilikaa kimya kwa masikitiko makubwa,

Kutafuta Mkombozi wetu atakayetuokoa (kwani)

Kwani tulipotea bila tumaini la Wokovu

Hakuna aliyejibu, “Nipo Bwana wangu unitume.”


Refrain

Tumepata Mkombozi, Yesu mwana pekee, Kutoka kwa Baba yake

Kamwe tusiwe na hofu, Mkombozi wetu ni Yesu Kristo

Kamwe tusiwe na hofu, Mkombozi wetu ni Yesu Kristo.


2. Ndipo Yesu akasema, “Nipo Bwana wangu nitume

Ntaondoka niende nikawatafuta walopotea

Na wakilia wote wenye dhambi wapate uzima,"

Kwa pendo la agape Yesu kajitoa kutufilia.


3. Tutalipa nini kwa pendo la Yesu, juu Msalabani?

Kwa damu aliyomwaga, watu wote tuokolewe

Sisi, hatuna cha kulipa bali kulifuata neno lake

Ndipo Mbingu zitafurahi mwanadamu kuokolewa.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Assorted, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Acheni Kristo Aitwe Kristo Lyrics Sung by Kurasini SDA Choir

Acheni Kristo Aitwe Kristo Lyrics Sung by Kurasini SDA Choir 1. Acheni Kristo, aitwe Kristo; Ni mfalme, Yule wa zamani, Kristo wa leo hii; ...