Saturday, 25 April 2026

Katikati Ya Washtakiwa Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Katikati Ya Washtakiwa Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Katikati ya washtakiwa, Waliosimama hukumuni

Nilikuwa mmoja wao, Hukumu ilisomwa kwetu

Sikuamini kusikia, Kwamba nimehukumiwa kifo

Faraja ingetoka wapi? Moyoni nikakata tamaa


Refrain

Nyuma yangu nikasikia, Sauti ikisema kwangu

Mkombozi yuko mlangoni, Kashuka toka juu

Ameshindwa kuvumilia, Kachukua nafasi yangu

Nimekuwa mtumwa huru, Hakika niko huru


2. Katikati ya washtakiwa, Waliotafutwa kwa bidii

Nilikuwa mmoja wao, Sababu nilimwacha Bwana

Nikatambua mbele yangu, Sina jinsi mimi ni wa kufa

Faraja ingetoka wapi? Moyoni nikasononeka.


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Kurasini Vol 32, Bedi Score, Bedi Lyrics

Wewe Ni Baba (Jenga Boma) Lyrics sung by Majaoni AY Kilifi, Kenya

Wewe Ni Baba (Jenga Boma) Lyrics sung by Majaoni AY Kilifi, Kenya 1. Wewe ni Baba wa kinilinda We ndiye shina anipendaye Marafiki wataponia...