Thursday, 30 April 2026

Siku Ya Mwisho Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Siku Ya Mwisho Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Siku ya mwisho tutakapoiona wingu angani (angani)

Yesu yuaja kutuchukua twende nyumbani (nyumbani)

Atupeleke mbinguni kwake Baba tupumzike (pumzike)

Yesu yuaja kutuchukua twende nyumbani (nyumbani)


Shida tulizoziona duniani tutasahau (Yesu)

Yesu yuaja kutuchukua Twende nyumbani (nyumbani)


2. Mwandame Bwana siku ya kuja kwake iko karibu (Yesu)

Yesu yuaja kutuchukua Twende nyumbani kwake

Makovu yote ya dhambi za dunia tutasahau (Yesu)

Yesu yuaja kutuchukua Twende nyumbani (nyumbani)


3. Rafiki zetu tulotengana nao tutawaona (Yesu)

Yesu yuaja kutuchukua Twende nyumbani kwake

Muda waisha jitayarishe sasa umwone Yesu (Yesu)

Yesu yuaja kutuchukua Twende nyumbani (nyumbani)


Ungali hai sahihisha mwenendo uokolewe (Yesu)

Yesu yuaja kutuchukua twende nyumbani kwake


4. Siku ya mwisho arejeapo Yesu tutasahau shida

Wote waliolala katika Bwana wataamshwa tena

Siku ya mwisho arejeapo Yesu tutasahau shida

Wote waliolala katika Bwana wataamshwa tena


Outro

Yesu; Yesu yuaja kutuchukua

Yesu; Yesu yuaja kutuchukua

Uwe tayari; Kuenda naye…


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Kurasini Vol 32, Bedi Score, Bedi Lyrics

Wewe Ni Baba (Jenga Boma) Lyrics sung by Majaoni AY Kilifi, Kenya

Wewe Ni Baba (Jenga Boma) Lyrics sung by Majaoni AY Kilifi, Kenya 1. Wewe ni Baba wa kinilinda We ndiye shina anipendaye Marafiki wataponia...