Najua Ananipenda Lyrics sung by Kurasini SDA Choir
1. Najua ananipenda mimi mdhambi
Najua aliteseka niokoke (niokolewe)
Nina sababu ya kuelezea
Nilivyokombolewa na damu ya Yesu
Najiandaa kumuona Mwokozi
Nikaishi naye huko juu
Pre-Chorus
Utafakari upendo wa Mungu,
Anavyotupenda sisi wenye dhambi
Nani aweza kuokoa nafsi yake?
(Dhidi ya Bwana, - Nafsi)
Pasipo kutegemea huruma zake
Chorus
Ni kwa huruma zake kwetu
(Kwa huruma zake)
Kwa huruma zake wanadamu tumekombolewa (Kombolewa)
2. Najua alivyo mwema kwa wenye shida
Ninatamani niwe kama alivyo (Ninatamani)
Mahangaiko ya maisha haya
Yote ni bure bila msaada wake
Wema wa Mungu wanipa faraja
Tafuteni wema wa Mwokozi.
Kurasini SDA Choir.
Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Kurasini Vol 31, Bedi Score, Bedi Lyrics