Saturday, 25 April 2026

Ole Ole Inakuja Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Ole Ole Inakuja Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Ole! Ole! Inakuja, Ole kutoka mbinguni

Changamkeni wokovu u mlangoni

Dunia itaachwa ukiwa siku inakujaa kilio kusaga meno

Mambo yote tunayoyaona yale tunayoyapenda yote tutayasahau

Ndio sababu ninasimama njia panda nikipaza sauti (Ooh-Ooh)

Ndio sababu ninasimama njia panda nikipaza sauti



(Kwenye) Nasimama kwenye njia panda

Ninasimama nikipaza sauti (Ooh-Ooh)

Waendao wasikie kotekote

Wasikie habari za wokovu

Kama Yona alivyopiga kelele

Watu wa Ninawi wakamsikia

Hizi ni habari za wokovu (Ooh-Ooh)


2. Kwa ujasiri nasimama njia panda

Natangaza kotekote injili ya marejeo

Kabla lango la rehema halijafungwa kwa wote waliodharau wito

Nafasi kwa watu wote bado ii wazi fanya matengenezo sasa harakisha

Ndio sababu ninasimama njia panda nikipaza sauti (Ooh-Ooh)

Ndio sababu ninasimama njia panda nikipaza sauti


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Kurasini Vol 31, Bedi Score, Bedi Lyrics

Wewe Ni Baba (Jenga Boma) Lyrics sung by Majaoni AY Kilifi, Kenya

Wewe Ni Baba (Jenga Boma) Lyrics sung by Majaoni AY Kilifi, Kenya 1. Wewe ni Baba wa kinilinda We ndiye shina anipendaye Marafiki wataponia...