Tafakari Maisha Yako Lyrics sung by Kurasini SDA Choir
Verse
Tafakari kama maisha yako
Yamtangaza Yesu,
Kwa watu
Matendo yako yaonekane vyema
Kati ya watu wa mataifa
Utende mema watu (watu wengi)
Watu wengi waokoke
Maishani mwako wamjue Mungu (Wamjue Mungu)
Utende mema watu (watu wengi)
Watu wengi waokoke
"Beba msalaba wako, nimfuate"
verse
"Yeye anipendaye atazishika,
Amri na kurithi ufalme"
Bwana ahadi zake hazibadiliki kamwe
Tangu zamani hajabadilika
Atawapa baraka tele,
Wamwaminio atawabariki
Baraka tele asema, "Nitawainua,"
Mtainuliwa ameahidi
Matendo yenu kwao wa mataifa,
Yatawavuta wasiomjua
Neno la Mungu lasema,
"Mnifuate, Mimi nimeshinda ulimwengu
Nimepewa mamlaka yote,
Mkinifuata nitawainua juu muwe washindi."
Verse
"Anipendaye atashika amri (zangu)
Anipendaye atainuliwa
Matendo yenu yatawavuta kwangu
Anipendaye anifuate."
"Anipendaye atashika amri (zangu)
Anipendaye atainuliwa
Matendo yenu yatawavuta kwangu
Anipendaye anifuate."
Kurasini SDA Choir.
Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Kurasini Vol 31, Bedi Score, Bedi Lyrics