Tuseme Nini Bwana Lyrics sung by Kurasini SDA Choir
1. Tuseme nini Bwana (Bwana), Kwa upendo ulio mkuu
Kututoa kwenye shimo, Kwenye giza la dhambi
Sifa zikurudie Mungu Baba na mwana
Uamuzi mliofanya kumuokoa mdhambi
Refrain
Haki ya Bwana, Utakatifu wetu
(Haki ya Bwana---Utakatifu wetu)
Tunaupata kwa njia ya imani
Kila anayemwamini Yesu
Damu ya Yesu inamuokoa
2. Twaokolewa kwa neema (neema), Wala si kwa matendo yetu
Mtu asikudanganye, Ni kwa huruma zake Bwana
Sote tumwangalie Yesu, Ndiye mkuu wa imani yetu
Na mbinguni tutafika tukimtegemea.
Kurasini SDA Choir.
Kurasini SDA Choir, Kurasini Vol 33, Bedi Score, Bedi Lyrics