Hapo Kule (Ayubu) Lyrics sung by Acacia Singers
1. Hapo kale kwenye mji wa Usi,
Alikuwepo mtu mmoja, Mkamilifu mtakatifu
Ndiye Ayubu mchaji wa Mungu,
Alikumbwa nayo majaribu, Akapoteza watoto wote
Mali nazo zikateketea,
Ndugu zake wakamkeuka, Lakini alisimama imara
Ndugu zake wakamkeuka, Lakini alisimama imara.
2. Ayubu alimtazama Mungu,
Katika saa ya kujaribiwa, Kwani mkewe alimgeuka
Akataka akufuru afe
Lakini Ayubu hakujali, Hata alipopoteza vyote
Akadumu kumwamini Mungu,
Mwisho Mungu akamwinua, Na kumzidishia tele
Mwisho Mungu akamwinua, Na kumzidishia tele
3. Je ndugu unasumbuka sana?
Na kulemewa na ya dunia, Maradhi vifo, njaa, mateso,
Vyakuandama kila wakati?
Ndugu jamaa wakukimbia? Hata wapoteza tumaini?
Sikia sasa habari njema,
Mtazame Yesu Mwokozi, Atakushindia yote
Mtazame Yesu Mwokozi, Atakushindia yote.
Acacia Singers Tz Mwenge, SDA Swahili Songs, Bedi Score, Bedi Lyrics