Kichuguu Kilicho Moyoni Mwangu (Bwana Chimba Kichuguu) Lyrics sung by Embakasi Central Church Choir
1. Kichuguu kilicho moyoni mwangu, Kitanizuia kuona ufalme wako
Malkia ambaye yu ndani yangu, Ni tisho kubwa kwa maisha yangu Bwana
Lakini najua nikijitolea nitasonga karibu na Bwana wangu.
Refrain
Bwana chimba kichuguu kichuguu ya dhambi,
Uondoe malkia moyoni mwangu
Unitayarishe kwa kazi yako, niwaletee wote waliopotea
Kazi itakamilika vipi? Iwapo mimi hapa sijakuwa bora.
2. Kichuguu ni siasa za kanisa, zimetufanya tusahau njia ya kweli
Malkia ni chuki na kiburi, wana wa Mungu wamepoteza mwelekeo
Kichuguu ni siasa za kanisa, zimetufanya tusahau njia ya kweli
Malkia ni chuki na kiburi, wana wa Mungu wamepoteza mwelekeo
Kila mtu kanisani twajipenda, hata ushirika hauna maana (with hums)
Tujihadhari sababu muda waisha, tusimsulubishe mara ya pili
Kila mtu kanisani twajipenda, hata ushirika hauna maana (with hums)
Tujihadhari sababu muda waisha, tusimsulubishe mara ya pili.
Embakasi Central Church Choir.
Embakasi Central Church Choir, SDA Kiswahili Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics
Link: https://youtu.be/N568hGq5PIY?list=RDN568hGq5PIY