Sikuja Na Kitu Hapa Duniani Lyrics sung by Kurasini SDA Choir
1. Sikuja na kitu hapa ulimwenguni,
Hilo nalitambua sababu niliumbwa,
Nitarudi tena huko nilikotoka,
Bila kuwa na kitu, vyote ni vya Bwana
Nikumbushe nikutumikie,
Hadi mwisho wa safari yangu, hapa duniani.
Refrain
Sikuja na kitu hapa duniani,
Na vyote nitaviacha duniani
Moyo wangu watosha kwa Bwana aliyenipa vyote
Jambo moja yangu sasa liko mbele yangu
Ni kutangaza marejeo ya Bwana,
Hadi mwisho wa safari yangu, nione utukufu.
2. Wakati mwingine Bwana najisahau,
Huku nikijikweza kwa mambo ya dunia,
Bwana nikumbushe niweze kujishusha,
Kwenye miguu yako nikutumikie,
Bwana wangu mimi sina dhamani
Nikumbushe nikutumikie,
Hadi mwisho wa safari yangu, hapa duniani.
Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Kurasini Vol 29, Bedi Score, Bedi Lyrics