Je Ulibatizwa (Ubatizo Wa Kweli) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir
1. Je, ulibatizwa ubatizo gani?
Ulipomwamini Yesu kuwa Bwana wako.
Refrain
Ubatizo wa kuruka moto, huu si ubatizo
Na kupita chini ya bendera, huu si ubatizo
Kunyunyuziwa maji kichwani, huu si ubatizo
Kupepeshwa mizigo mizito, huu si ubatizo
Ubatizo wa kweli, ni ule ambao Yesu alibatizwa,
Ya kuzamishwa ndani ya maji, Ya maji yalo mengi.
2. Ndugu ‘sidanganywe soma maandiko
Yesu alivyobatizwa mtoni Yordani.
3. Wengi wetu leo wamedanganyika
Wamefungua macho yao pasipo kujua.
Kurasini SDA Choir.
Kurasini SDA Choir Assorted, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics