Wednesday, 10 June 2026

Jihoji (Je Unafanana Na Mwokozi) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Jihoji (Je Unafanana Na Mwokozi) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Jihoji kama wafanana,

Na Mwokozi Yesu Bwana wako

Ni balozi mwaminifu?


Dini yako kweli yapendeza,

Watu na Mungu duniani

Uwe barua yake Mungu

Uwe barua yake Mungu.


Refrain

Je unafanana na Mwokozi wako,

Katika maneno na matendo?

Bahasha kwa juu, anwani ya Yesu

Barua kwa ndani, si ya Yesu.


2. Ukristo wako majira,

Wafanana na wafarisayo

Walijipamba kwa nje,


Siku sita ni kwa ulimwengu,

Sabato ni kwake Mungu Muumbaji

Wasomekaje ndugu yangu?

Wasomekaje ndugu yangu?


3. Uwapo ndani ya Kanisa,

Yesu Mwokozi ni Bwana wako

Ukitoka wamuacha,


Mitani pia safarini,

Wafanana nao ulimwengu

Utubu uje kwake Yesu

Utubu uje kwake Yesu.


For Revision (or Affirmation): R3: Bahasha kwa juu, anwani ya Yesu


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Assorted, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Acheni Kristo Aitwe Kristo Lyrics Sung by Kurasini SDA Choir

Acheni Kristo Aitwe Kristo Lyrics Sung by Kurasini SDA Choir 1. Acheni Kristo, aitwe Kristo; Ni mfalme, Yule wa zamani, Kristo wa leo hii; ...