Monday, 8 June 2026

Ni Takatifu Sana (Ndoa) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Ni Takatifu Sana (Ndoa) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


Pre-Verse

Ni takatifu sana kwake Mungu,

Ndoa ya leo sikiliza.


1.Mungu aliona si vyema,

Mtu kuishi akiwa pekee yake

Akampa msaidizi,

Hata leo twashuhudia (Mungu).


Refrain

(Ndoa) Ndoa ni agizo toka kwake Mungu,

Ipewe heshima na watu wote

Maarusi wetu Bwana awe nanyi,

Muyaanzapo maisha mapya.


2. Bwana harusi na bi harusi

Sio wawili bali ni mwili moja

Tendeeni yote kwa pamoja

Bwana Yesu awaongoze (Bwana).


3. Vumilianeni daima,

Uaminifu ni kitu cha maana

Msimruhusu Shetani,

Atawale nyumbani mwenu (Maarusi).


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Assorted, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Nikitazama Dunia (Ukimwi) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Nikitazama Dunia ( Ukimwi ) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir 1. Nikitazama dunia, Inaombolezayo waya waya Magonjwa yenye kutisha, Yanavyowa...