Sunday, 14 June 2026

Ni Watano (Walibisha Hodi Hodi) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Ni Watano (Walibisha Hodi Hodi) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir


1. Ni watano, Waliokuwa ni wajinga

Na watano, Walikuwa wenye busara

Wote walisubiri, Bwana harusi pamoja

Wote walisubiri, Bwana harusi Pamoja.


Tazama; na wajinga hawakuwa na akiba; mafuta

Na la kushangaza, Bwana harusi kachelewa.

Tazama; na wajinga hawakuwa na akiba; mafuta

Na la kushangaza, Bwana harusi kachelewa.


Wote wakasinzia, wakalala usingizini

Wote wakasinzia, wakalala usingizini.


2. Usiku wa manane, sauti ikasikika

Bwana harusi amefika, Wote wakatoka usingizini

Kumlaki Bwana harusi, Ole wao wale wajinga

Walikosa mafuta, Taa zao zikazimika.


Usiku wa manane, sauti ikasikika

Bwana harusi amefika, Wote wakatoka usingizini

Kumlaki Bwana harusi, Ole wao wale wajinga

Walikosa mafuta, Taa zao zikazimika.


Refrain

Walibisha hodi, hodi (hodi) tufungulieni mlango

Kwani hata sisi, tumekesha tukisubiri

(Huzuni) Na huzuni ni kwamba (kwamba), hau’funguliwa tena

Ni aibu kubwa, kwamba tutafunguliwa nje.


3. Kweli nyinyi ndio taa, ya ulimwengu wa sasa

Tangazeni ujumbe huu, kwa kukesha ombeni msichoke

Msififie kwa imani, imani ndiyo mafuta

Akiba ni kwa Bwana, aliye Mkombozi wetu.


Kweli nyinyi ndio taa, ya ulimwengu wa sasa

Tangazeni ujumbe huu, kwa kukesha ombeni msichoke

Msififie kwa imani, imani ndiyo mafuta

Akiba ni kwa Bwana, aliye Mkombozi wetu.


Refrain

Walibisha hodi, hodi (hodi) tufungulieni mlango

Kwani hata sisi, tumekesha tukisubiri

(Huzuni) Na huzuni ni kwamba (kwamba), hau’funguliwa tena

Ni aibu kubwa, kwamba tutafunguliwa nje.


NOTES

R(Huzuni) Na huzuni ni kwamba (kwamba), hau’funguliwa tena; (Huzuni) La huzuni ni kwamba, hau-ku-funguliwa tena


Kurasini SDA Choir.


Kurasini SDA Choir Assorted, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics

Usiku Wa Manane Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Usiku Wa Manane Lyrics sung by Kurasini SDA Choir Pre-Chorus Usiku wa manane , kelele zikasika, Amini; Usiku wa manane, kelele zikasika. Ref...