Wengi Wanatamani Lyrics Sung by Kurasini SDA Choir
1. Wengi wanatamani kumwona Bwana,
Hiyo ni sawa, ni sawa sawa, ni sawa
Lakini neno lasema waziwazi,
Ni kama mtu aliyekimbia simba
Mbele yake akakutana na dubu (dubu mkali),
Siku ya Bwana yawaka kama moto, yatisha.
Refrain
Utavuna kile (kile) ulichokipanda,
Neno la Bwana lasema waziwazi
Uzima milele, au hukumu ya kifo,
Siku ya Bwana yawaka kama moto, yatisha.
2. Siku ya Bwana watu wagawanyika,
Wenye furaha, wenye huzuni, kilio
Kila mtu atabeba furushi lake,
Vilio vingi ndivyo vitavyosikika,
Fanya matengenezo una nafasi, ndugu yangu
Mlango wa rehema ungali wazi, rafiki.
Kurasini SDA Choir Assorted 2, Kurasini Classics, Bedi Score, Bedi Lyrics