Kisha Nikaona Mbingu Lyrics sung by Kurasini SDA Choir
1. Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya
Mara mbingu za kwanza nchi vyote vimeshapita
Nami nikaona Yerusalemi ukishuka
Ukishuka toka kwa Mungu kama bibi harusi
Ukishuka toka kwa Mungu kama bibi harusi
Refrain
Tazama maskani ya Mungu, Pamoja na wanadamu
Mungu ataishi na watu wake, Naye atafuta machozi yote
Maombolezo na maumivu vyote vimekwisha toweka
Maombolezo na maumivu vyote vimekwisha toweka
2. Yeye ashindaye atayaridhi haya milele
Mikono ya Bwana imenyoshwa kwetu atuita
Tuwezeshe Bwana tupokee neema ya Yesu
Tuvishwe utakatifu wake sote kwa imani
Tuvishwe utakatifu wake sote kwa imani.
Kurasini SDA Choir.
Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Kurasini Vol 32, Bedi Score, Bedi Lyrics