Leo Naukana Utu Wangu Lyrics sung by Kurasini SDA Choir
1. “Leo naukana utu wangu wa kale,
Naanza maisha mapya katika Kristo
Nimejifunza habari zako, Eh Bwana,”
Hivi leo najitoa kwake
Refrain(1)
Mambo ya dunia ni hasara,
Fahari zake hazidumu
Refrain (2)
Maisha kwa Yesu ni salama
Aah, Nimejifunza kumfuata Yesu,
Maisha kwa Yesu ni salama
2. “Leo Yesu andika upya jina langu,
Kwenye kitabu cha uzima wa milele
Ya kale yote ninayaacha Bwana,”
Hivi leo najitoa kwake.
Kurasini SDA Choir, Kurasini Vol 32, Bedi Score, Bedi Lyrics