Kama Ilivyo Kwenye Safari Lyrics sung by Saro's Family
Kama Ilivyo Kwenye Safari Lyrics sung by Saro's Family Eh-le lele-lele-lele-lele le-le-leh 1. Kama ilivyo kwenye safari Kuna shida na matatizo Kuna vikwazo dhoruba kali Na majaribu mbalimbali Safari yetu kwenda mbinguni Mambo mengi huvunja moyo Wasafiri hukataa tamaa Refrain 1 Farao yuaja nyuma yetu (Nyuma yetu) Bahari ya Shamu mbele yetu Kunayo milima kandokando yetu Bwana fungua njia (Farao) Eh-le lele-lele-lele-lele le-eh 2. Kama ilivyo kule vitani Jemedari yu mbele yetu Mara jangwani, mara msalaba Mwisho kaburi li wazi Nasi nyumaye twasonga mbele Twazifuata nyayo zake tu Tusichoke mwisho tutashinda Refrain 2 Farao yuaja nyuma yetu (Nyuma yetu) Bahari ya Shamu mbele yetu Japo kuna shida na majaribu mengi Njia atafungua. (Farao) Saro's Family. Saro’s Family, Bedi Score , Bedi Lyrics