Posts

Showing posts from September, 2025

Kama Ilivyo Kwenye Safari Lyrics sung by Saro's Family

Kama Ilivyo Kwenye Safari Lyrics sung by Saro's Family Eh-le lele-lele-lele-lele le-le-leh 1. Kama ilivyo kwenye safari Kuna shida na matatizo Kuna vikwazo dhoruba kali Na majaribu mbalimbali Safari yetu kwenda mbinguni Mambo mengi huvunja moyo Wasafiri hukataa tamaa Refrain 1 Farao yuaja nyuma yetu (Nyuma yetu) Bahari ya Shamu mbele yetu Kunayo milima kandokando yetu Bwana fungua njia (Farao) Eh-le lele-lele-lele-lele le-eh 2. Kama ilivyo kule vitani Jemedari yu mbele yetu Mara jangwani, mara msalaba Mwisho kaburi li wazi Nasi nyumaye twasonga mbele  Twazifuata nyayo zake tu Tusichoke mwisho tutashinda Refrain 2 Farao yuaja nyuma yetu (Nyuma yetu) Bahari ya Shamu mbele yetu Japo kuna shida na majaribu mengi Njia atafungua. (Farao) Saro's Family. Saro’s Family, Bedi Score , Bedi Lyrics

I Am Dreaming Lyrics sung by Saro's Family

I Am Dreaming Lyrics sung by Saro's Family Verse I I am dreaming about that day When the trumpet shall be sound And in my dream, I see the king Coming down for me To take me home (To take me home) CHORUS SESSION 1 Chorus, Part 1 So, he takes me home (He takes me home) Where I belong (Where I belong) The Angels fold (The Angels fold) Their wings for me (Their wings for me) And in my dream (And in my dream) I'm ushered in (I'm ushered in) Chorus, Part 2 Oh, And as I walk to the throne , I see my Lord And as I walk to the throne, I see my Lord Chorus, Part 3 And in his hands (And in his hands) There is my crown (There is my crown) And in his hands (And in his hands) There is my crown (There is my crown) Chorus, Part 4 Come on! Everybody let’s dream big Dream on, Even in the pit of danger Oh Let's dream (big), Dream and dream, Dream on, even in the pit of danger Chorus, Part 5 Everybody say, Dream big Dream on, even in the pit of danger Like Joseph (Joseph), and Steven (...

Tengeneza Nyumba Yako Lyrics sung by Grace and Glory Singers

Tengeneza Nyumba Yako Lyrics sung by Grace and Glory Singers 1. '(Tengeneza wewe) Tengeneza nyumba yako, Weka mambo sawa sawa Na ugawe mali yako (Hakika) Hakika wewe hutaishi tena, Kwa kweli ugonjwa wako utakumaliza’ Hezekia mfalme uliye mkuu, 'Umebaki na siku chache pekee' Refrain (Ombi/+langu Bwana) Ombi langu Bwana nisamehewe Najua nafaa kwa sababu ya dhambi zangu Rehema zako bado zadumu kwangu Kumbuka jinsi nimekufanyia kazi (Eh Bwana) Bwana wangu naomba nafasi nyingine 2. (Japo) Japo twakaribia kuanguka, Mungu wetu kweli ni mwaminifu Tukiomba msamaha kwake (kwake), Atatupa nafasi nyingine. Grace and Glory Singers.

Tafakari Kisa/Kisa Cha Wanaisiraeli Lyrics sung by Grace and Glory Singers

Tafakari Kisa/Kisa Cha Wanaisiraeli Lyrics sung by Grace and Glory Singers 1. Tafakari kisa cha wanaisiraeli Walipozunguka zunguka kuta za Yeriko Kuta zikaporomoka Si kwa zana za vita wala bomu Ila kwa vinubi vilivyopulizwa Kwa uwezo wa Mungu (Kwa kweli) kuta zikaporomoka Refrain Waimbaji tupaze sauti zetu Tuvunje ila zote za mwovu Wahubiri tangazeni neno Watu watambue Mungu ni muweza 2. Tumepewa mamlaka naye Mungu wetu Juu ya vitu – vitu vyote ulimwenguni Tusiwe na hofu tena kwa imani tutayashinda yote Roho wake Mungu yu nasi Katika majaribu yote, Tuamini kwake Mungu. Grace and Glory Singers.

Piga Kelele Binti Israeli Lyrics sung by Grace and Glory Singers

Piga Kelele Binti Israeli Lyrics sung by Grace and Glory Singers 1. Piga e binti Zayuni piga kelele Israeli Furahi na kushangilia kwa moyo wako wote, E binti Yerusalemi, Bwana ameziondoa hukumu zako Mfalme wa Israeli Yu katikati yako hutaogopa uovu tena Furahi na kushangilia kwa moyo wako wote, E binti Yerusalemi, Bwana ameziondoa hukumu zako Mfalme wa Israeli Yu katikati yako hutaogopa uovu tena Refrain Achumaye juani hula kivulini Mvumilivu hula mbivu Tuyavumilie ya dunia japo ni machungu Si kitambo Yesu arudi Na tushike ufalme wake 2. “Nitawakusanya wanaousikitia mkutano wa ibada Nitamponya yeye achechemeaye Nitamkusanya yeye aliyefukuzwa Nami nitawafanya sifa na raha Miongoni mwa watu wote duniani Nitawapa raha,” asema Bwana. Grace and Glory Singers.

Nitachipuka Tena Lyrics sung by Grace and Glory Singers

Nitachipuka Tena Lyrics sung by Grace and Glory Singers 1. Nitachipuka tena na kustawi kwa kuwa nimekita mizizi kwa Yesu Matunda yangu mazuri yalete watu kwa Yesu Refrain Hata nikianguka nitasimama tena Na kuanza safari yangu Kama mti uliokatwa huchipuka tena Na kutoa matawi mapya Na mwishowe huzaa matunda mema 2. Wale wamtumainio Mwokozi Wafananishwa na mlima wa Zayuni Japo pepo na zivume hawatatikiswa kamwe. Grace and Glory Singers.

Msiwape Mbwa Lyrics sung by Grace and Glory Singers

Msiwape Mbwa Lyrics sung by Grace and Glory Singers 1. Msiwape mbwa kilicho kitakatifu Wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe Wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao Wakageuka na kuwararua Omba tafuta bisha, Kwa maana Kila aombaye hupokea, Naye atafutaye huona Abishaaye atafunguliwa, Mambo yatakuwa shwari Kila aombaye hupokea, Naye atafutaye huona Abishaaye atafunguliwa, Mambo yatakuwa shwari Chorus Basi ninyi salini hivi, Baba yetu uliye mbinguni jina lako litukuzwe, ufalme, Ufalme wako uje Mapenzi yako yatimizwe hapa duniani, Kama mbinguni Utupe leo riziki yetu, Utusamehe deni zetu, Kama sisi tuwasameavyo wadeni wetu Usitutie majaribuni 2. Basi msalipo msiwe kama wanafiki Kwa maana wao wapenda kusali Hali wamesimama masinagogi na katika pembe za njia Ili waonekane na watu Bali wewe usalipo ingia katika chumba chako Usali mbele ya Baba yako aliye sirini, Na Baba yako aonaye sirini, Atakujali Bali wewe usalipo ingia katika chumba chako Usali mbele ya Baba yako aliye sirini, Na Baba ya...

Kila Mtu Awapotezea Lyrics sung by Grace and Glory Singers

Kila Mtu Awapotezea Lyrics sung by Grace and Glory Singers 1. Kila mtu awapotezea wenye haki Katika njia mbaya ataanguka Katika rima lake yeye mwenyewe Bali wakamilifu wataridhi mema Yeye aligeuzaye sikio lake Asisikie sheria ya Mungu Hata sala yake ni chukizo, Chukizo kwa Mungu Chorus Basi simameni katika njia kuu, Mkaone, Mkaulize mapito ya zamani Iwapo njia iliyo njema, Mkaenende katika njia, Njia hiyo nzuri Mkatubu dhambi zenu, Mkawe safi Naye ninyi basi-ii, Mtajipatia raha katika nafsi zenu 2. Afichaye dhambi zake Hatafanikiwa Bali yeye aziungamae na kuziacha atapata rehema Aendaye kwa unyofu ataokolewa Ila mkaidi wa njia zake Ataanguka mara. Grace and Glory Singers.

Jaribu Kufuata Lyrics sung by Grace and Glory Singers

Jaribu Kufuata Lyrics sung by Grace and Glory Singers 1. Jaribu kufuata nyayo za Yesu Jaribu kuandama Bwana mfalme Kwa mfano wake atubadilisha Raha furaha nyimbo twaimba Refrain Yapendeza tembea katika nyayo zake (Nuru) Nuru kuongoza Nuru kuongoza Yapendeza tembea katika nyayo zake Twamfuata Yesu 2. Twamkaribia zaidi Mwokozi Twajaribiwapo twate-? njia Twategemea mkono wa hodari Atutetea furaha twaimba 3. Jaribu kufuata nyayo za Yesu Siku hadi siku twapanda juu Hadi tumuone kwa uzuri wake Raha furaha tukiwa naye. Grace and Glory Singers.

Come and Dine/Jesus Has a Table Spread Lyrics sung by Grace and Glory Singers

Come and Dine/Jesus Has a Table Spread Lyrics sung by Grace and Glory Singers 1. Jesus Has a table spread  Where the saints of God are fed, He invites His chosen people, Come and dine; With His manna He doth feed And supplies our every need: O ’tis sweet to sup with Jesus all the time! Refrain Come and dine, the Master calleth, Come and dine; You may feast at Jesus’ table all the time; He who fed the multitude, turned the water into wine, To the hungry calleth now, Come and dine. 2. The disciples came to land, Thus obeying Christ’s command, For the Master called unto them, Come and dine; There they found their heart’s desire, Bread and fish upon the fire; Thus He satisfies the hungry every time 3. Soon the Lamb will take His bride To be ever at His side, All the host of Heaven will assembled be; O ’twill be a glorious sight, All the saints in spotless white; And with Jesus they will feast eternally. Grace and Glory Singers. Music Composition & Words by Charles B. Widmeyer

Apandaye Haba Lyrics sung by Grace and Glory Singers

Apandaye Haba Lyrics sung by Grace and Glory Singers Chorus Apandaye haba atavuna haba Na apandaye kwa ukarimu ni ukarimu Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake Si kwa huzuni wala si kwa lazima Maana Mungu humpenda yeye Atoaye kwa moyo wa ukunjufu Tena ni mwenye heri Verse 1 Leteni zaka kamili ghalani Ili kimo chakula katika nyumba yangu 'Mkanijaribu kwa njia hiyo Asema Bwana wa majeshi' Mjue kama sitawafungulia  Madirisha yote ya mbinguni Na kuwamwagieni baraka za mbingu Hata isiwepo nafasi ya kutosha Chorus Apandaye haba atavuna haba Na apandaye kwa ukarimu ni ukarimu Kila mtu na atende Kama alivyokusudia moyoni mwake Si kwa huzuni wala si kwa lazima Maana Mungu humpenda yeye Atoaye kwa moyo wa ukunjufu Tena ni mwenye heri Verse 2 Yeye asiyemwachilia mwana wake mwenyewe Bali kamtoa kwa ajili yetu si’ sote Atakosaje kutukirimia Na mambo yote, pamoja naye. Chorus Apandaye haba atavuna haba Na apandaye kwa ukarimu ni ukarimu Kila mtu na atende Kama alivyokusudia moyo...

Anasewuok Lyrics sung by Grace and Glory Singers

Anasewuok Lyrics sung by Grace and Glory Singers 1. Anasewuok anadhiye gogo Ayombega-? mond’ alos mwanduna Adieri Petro ene-? wito geno Joyahudi onego taya Yawa Yesu manena ageno kuome, Emano chuadi kendo nogur e bawo Anadong’ kendo adawadawa, Aonge geno kendo aonge teko Anadong’ kendo adawadawa, Aonge geno kendo aonge teko Chorus Seche moko wasewito geno (Wasewito geno) Ne gik matimorenwa e pinyka Apaka mag nembe gi ngeri mag aore nyalo yweyi Chorus Kik iwit geno (Kik iwit geno) kata matin Kata bedni taya mane ngimani nosetho obiro liel kendo 2. Iselemo gi kinda to pod ineno chandruok Bende isepenjori “Nyasaye jo malamigi, Singo mane manisingoni nitimnegi Momiyo pod gineno malit kama?” Singo mane manisingoni nitimnegi Momiyo pod gineno malit kama?” Grace and Glory Singers. For Revision #ForRevision 1. Ayombega-? 2. Adieri Petro ene-? wito geno

Anza Vyote Na Bwana Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Anza Vyote Na Bwana Lyrics sung by Kurasini SDA Choir 1. Anza vyote na Bwana , Tembea na Bwana , Furahi na Bwana ushindi Mchana kutwa shikamana naye Usimwache Bwana rafiki mwema Bila Yesu ni bure, ni bure, Ni bure, ni bure utaanguka Anza vyote na Bwana ushindi daima Anza vyote na Bwana ushindi daima Refrain Anza mambo yako alfajiri Wewe ni wa ahadi Ushindi wako mkononi mwa Bwana Tegemea ushindi Kabla anga halija chafuka, Mpe Yesu nafasi Machungu yako yote mpe Yesu , (Oh) Mpe Yesu nafasi 2. Tegemea ushindi kwa Bwana Amani kwa Bwana , Faraja kwa Bwana Safarini utabarikiwa Ulinzi wa Bwana uko juu yako Usikatishwe tamaa simama imara Pambana ufike mwisho Anza vyote na Bwana ushindi juu yako Anza vyote na Bwana ushindi juu yako. Kurasini SDA Choir. Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics , Ukuta Wa Jeriko Album , Bedi Score , Bedi Lyrics

Kati Ya Vyote (Aliniumba Kwa Mfano Wake) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Kati Ya Vyote (Aliniumba Kwa Mfano Wake) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir 1. Kati ya vyote vilivyoumbwa, Niliumbwa kwa mfano wa Mungu Ni kwa sababu alinifinyanga Kwa mfano wake, Eeeh-Eeeh-Eeeh Nilitoka mikononi mwake, Inapendeza kurudi kwake Aliniumba kwa mfano wake, Kwa mapenzi ya Mungu Refrain Aliniumba kwa mfano wake, Inapendeza nilitoka kwake Ingawa dhambi ilitia waa, Aliniosha nikawa safi Ingawa dhambi ilitia waa, Aliniosha nikawa safi, Safi-ii safi-ii Aliniosha nikawa safi, Safi-ii safi-ii, Aliniosha nikawa safi 2. Kanipulizia pumzi yake, Nipate kuwa kiumbe hai Ni kwa sababu alinifinyanga Kwa mkono wake, Ooh-Ooh-Ooh Ndio sababu ninapendeza, Kuliko vyote vilivyoumbwa Aliniumba kwa mfano wake, Kwa mapenzi ya Mungu. Kurasini SDA Choir. Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Ukuta Wa Jeriko Album , Bedi Score , Bedi Lyrics

Malaika Mbinguni (Sauti Za Shangwe) - Unastahili Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Malaika Mbinguni ( Sauti Za Shangwe ) - Unastahili Lyrics sung by Kurasini SDA Choir I Verse Malaika mbinguni zikiimba kwa furaha Watakuwa watakatifu Watakuwa watakatifu wakiimba Watapendeza watavutia Kwa mavazi meupe watapendeza Verse Utapenda kuwa mmoja Utapenda kuwa mmoja wa watakaoimba Wataimba wimbo mpya Wakizunguka kiti cha enzi Wataimba wimbo mpya Wimbo wa Musa na Mwana kondoo Verse Unastahili Unastahili kuupokea utukufu Unastahili Unastahili uliimwaga damu Kukomboa wengi, Unastahiliiii… II Verse Ulifundisha mitume neno lako Ukawatuma kufundisha wengine Walihubiri na kulitangaza neno Ukawa mwanzo wa injili yako leo Verse Injili yako ikatangazwa Ikafundisha neno lako kwa upendo Walihubiri habari za mbinguni Wakawavuta wengi wakujue wewe Injili yako ikatangazwa kwa upendo III Verse Kazi ni yako Bwana Uliyotuagiza, ‘Nendeni ulimwenguni kuhubiri Mkawafanye wote kuwa wanafunzi Mkiwabatiza kwa jina la Baba, Mwana na roho mtakatifu, Nitakuwa nanyi siku zote Hata ukamilifu na mwisho ...

Tunaukaribia Jerusalem Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Tunaukaribia Jerusalem Lyrics sung by Kurasini SDA Choir 1. Tunaukaribia Jerusalem , Mji mzuri wa Jerusalem Kila mtu atafuta wokovu -Uuhu, Apate ingia Jerusalemu-(…Ooh*) Refrain Wengi twataka kuingia pale, Twajiinua twajawa kiburi Kusema ‘twataka kuingia,’ Kuingia ni jambo jingine Tumeangalia-? ya dunia, Tutawezaje ingia pale? (Ooh*) 2. Tumeugeukia ulimwengu, Ya Mungu tumeyaweka kando Tumetanguliza miungu yetu -Uuhu, Tutawezaje ingia pale?-(…Ooh*) Kurasini SDA Choir. Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics , Ukuta Wa Jeriko Album , For Revision, Bedi Score , Bedi Lyrics (…Ooh*) - An animation on second repeat in verse 1 & 2. For Revision; Tumeangalia-?

Mwisho Wa Safari Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Mwisho Wa Safari Lyrics sung by Kurasini SDA Choir 1. Mwisho wa safari twaona nchi nzuri Ng'ambo ya bahari makao ya washindi Chorus Hujawahi ona mazuri ya mji ule Maziwa na asali (asali) raha ya mji ule Usichoke ndugu pambana hadi mwisho  Mwisho wa safari twaona nchi nzuri 2. Mwisho wa safari sauti zasikika Zikiimba wimbo wa Musa mwana Kondoo . Kurasini SDA Choir. Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Ukuta Wa Jeriko Album , Bedi Score , Bedi Lyrics

Nataka Zaidi (Nataka Kumwona Yesu) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Nataka Zaidi ( Nataka Kumwona Yesu ) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir 1. Nataka, Nataka, Nataka, Nataka zaidi Nataka kumjua Yesu Nataka kujua habari zake Yesu , N'ambie Nataka zaidi, Zaidi na zaidi N’ambie zaidiii Refrain Katika Yesu (Yesu) vipofu wanaona tena Katika Yesu (Yesu) viwete wanashangilia Katika Yesu majibu yapatikana 2. Nataka tena Na tena, Na tena kukaa na Yesu Nataka tena Na tena, Na tena kukaa na Yesu, Zaidiii Outro Nataka, Nataka, Nataka, Nataka Zaidiii Nataka kumjua Yesu. Kurasini SDA Choir. Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics , Ukuta Wa Jeriko Album , Bedi Score , Bedi Lyrics N’ambie = Niambie

En e Yoo Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

En e Yoo Lyrics sung by Kurasini SDA Choir Chorus En e yoo , Yesu en e yoo ×8 [Omiyo awerne Yesu (Yesu) En e yoo Adieri en e yora, (Yesu) En e yoo Omiyo awerne Yesu (Yesu) En e yoo Adieri en e yora, (Yesu) En e yoo En e yoo, Yesu en e yoo, Yesu en e yoo] ×2 Verse En e ler mamenyo yora, Enie ler En e ler mamenyo yora, En e ler En e ler mamenyo yora, Enie ler En e ler mamenyo yora, En e ler Ooh Yesu kalo en e ler Jawar konya kalewo dier ndara En e ler mamenyo yora, En e ler Chorus En e yoo, Yesu en e yoo ×8 [Omiyo awerne Yesu (Yesu) En e yoo Adieri en e yora, (Yesu) En e yoo Omiyo awerne Yesu (Yesu) En e yoo Adieri en e yora, (Yesu) En e yoo En e yoo, Yesu en e yoo, Yesu en e yoo] ×6 Kurasini SDA Choir. Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Ukuta Wa Jeriko Album , Bedi Score , Bedi Lyrics This is a praise song is filled with ululations, whistles that mark celebration of Jesus as the way, light and shield.

Wataka Kujua (Yesu Akanigusa) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Wataka Kujua ( Yesu Akanigusa) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir 1. Wataka kujua habari zangu (habari zangu) Nilikuwa kipofu sasa naona Sijui ni kwa vipi ninalojua (Eeh) Nilikuwa kipofu sasa naona Refrain Yesu akanigusa nikaona (Haleluya) Ninaona (nami) amenigusa (na-we we-we) Nilikuwa kipofu ninaona (Haleluya) Ninaona (nami) amenigusa 2. Nilipaza sauti nipate ona (nipate ona) Baada ya kusikia Yesu apita Bwana unirehemu akasikia (Aah) Nilikuwa kipofu sasa naona. Kurasini SDA Choir. Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Ukuta Wa Jeriko Album , Bedi Score , Bedi Lyrics

Nitasimulia Kisa Cha Yesu Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Nitasimulia Kisa Cha Yesu Lyrics sung by Kurasini SDA Choir 1. Nitasimulia kisa cha Yesu, Kwa matendo makuu aliyotenda Kwa rehema zake nitasimulia, Amebadilisha maisha yangu Sasa natambua kwamba anipenda, Nitasimulia habari zake Kamwe sitaacha kunena habari, Habari za Yesu tamu kwangu Pre-Chorus Nitasimulia habari zake, Amebadilisha maisha yangu Nilikuwa vile leo niko hivi, Amebadilisha maisha yangu Nitasimulia habari zake Chorus Mashariki (wote) kusini, wasikie Kaskazini (wote) magharibi, wasikie (wasikie) Vilindini (wote) na bahari, wasikie Juu angani viumbe viseme ya kwamba Yesu; Mfalme wa utukufu 2. Katika tanuru amenilinda, Tunduni mwa simba kashuka kwangu Amenikingia mauti juu yangu, Hukumu ya kifo aliibeba Sasa natambua kwamba anipenda, Nitasimulia habari zake Kamwe sitaacha kunena habari, Habari za Yesu tamu kwangu. Kurasini SDA Choir. #RepeatPostedLyrics Second Time Posting.

Katikati Ya Mafarao (Amini) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Katikati Ya Mafarao (Amini) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir 1. Katikati ya mafarao wasiomjua Yusufu Yuko Mungu atakae simama kwa ajili yako Immanueli Mungu yupo nasi Ebeneza Mungu wa maajabu Atakuinulia uso wake Akufadhili akulinde Katika tundu la simba Kati ya watesi atakuona Malaika wakuzunguka kote Uko mikononi mwake Refrain Amini, (Amini) na tena uamini Anashughulikia maisha yako Amini, (Amini) na tena uamini Rehema zake kwako ni za ajabu Uamini na tena uamini Maisha yako mikononi mwake Uamini na tena uamini Roho anaugua kwa ajili yako 2. Katikati ya masumbuko yako Yuko anayeweza kukuonyesha Upendo uliokwisha toweka Faraja kwa wanaoteseka Yuko Mungu anayejali leo Atakuwa mfariji kwa waliokataa tamaa Waliosongwa na dunia hii Walimwengu watakapokushusha Atakufunika mbawani mwake Ujisalimishe kwake. Kurasini SDA Choir. Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics , Ukuta Wa Jeriko Album , Bedi Score , Bedi Lyrics

Watu Wengi Walikuja (Waliofika Kwake) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Watu Wengi Walikuja (Waliofika Kwake) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir 1. Watu wengi walikuja kwa Yesu Hawakubakia kama mwanzo Walibadilika wakazaliwa upya Jaribu leo utabadilika Refrain Waliofika kwake (fika kwake) Wakiwa ni vipofu (vipofu) Walifanyika wana (wana wana) Wana wa kifalme Waliofika kwake (fika kwake) Wakiwa ni viwete (viwete) Wakatupa magongo (yao, yao) Wakaenda zao 2. Namtafuta atakayenitoa hapa, yuko wapi? Nimezungukwa na adui kotekote, n’ende wapi? Namtafuta Yesu Ni Yesu pekee wa kunitoa hapa Namtafuta atakayenitoa hapa, Yesu pekee. 3. Nimezunguka kotekote Ili nimuone Yesu Kama Zakayo alitamani kumuona Yesu Akagundua ufupi wake Akapanda juu ya mkuyu Yesu akamuona kamwambia, ‘Shuka, Wokovu umefika kwako.’ Kurasini SDA Choir. Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics , Ukuta Wa Jeriko Album , Bedi Score , Bedi Lyrics

Bwana Twataka Njia (Ukuta Wa Jeriko) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Bwana Twataka Njia ( Ukuta Wa Jeriko ) Lyrics sung by Kurasini SDA Choir 1. Bwana twataka njia kwenda ng’ambo Mbele yetu kuna vikwazo vingi Jeshi la Bwana limeshapanga vita Lataka kuvuka Makedonia Kama Paulo na Sila waliomba Lango la gereza likafunguka Refrain Ukuta wa Jeriko (Jeriko) Ulibomoka kwa nguvu za Mungu Tutakaa kimya Bwana atapigana Ukuta utasambaratika Nahodha wetu ni Yesu yuko mbele Njia nyeupe tupite Jina la Yesu ni kama ngao kwenye vita Twataka kuvuka watu wanaangamia 2. Mbiu imelia jeshi vitani Uria amerudishwa nyumbani Uria kwa kinywa chake akasema, ‘Talalaje jeshi liko vitani (Bwana) Fungua njia Bwana tusonge mbele Yowe limelia kwapambazuka. Kurasini SDA Choir. Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics , Ukuta Wa Jeriko Album , Bedi Score , Bedi Lyrics

Giza Nene Limetanda Lyrics sung by Kurasini SDA Choir

Giza Nene Limetanda Lyrics sung by Kurasini SDA Choir 1. Giza nene limetanda usoni Napapasa sioni pa kushika Msaada wangu ‘tatoka wapi? Natafuta uso wa Bwana wangu Anishike mkono nifike kwake Refrain Sauti ikasema mimi ni Mungu wako Ni Alfa na Omega Mwanzo mwisho Niite wakati wa shida, Mimi nitajibu, (Kwa kweli nitajibu) ‘Katika mambo magumu niite (Mimi) Tangu mwanzo nilikuwepo (Mimi nipo) Leo nipo (Leo nipo) kesho nipo (Kesho nipo) niite kwako Mambo magumu kwako Nitajibu Niite nitaitika, Mambo magumu kwako Nitajibu Niite nitaitika’ 2. Majaribu yaliyo mbele yangu Kila siku ninapanda kushuka Kila siku ninayaona mapya Msaada wangu ‘tatoka wapi? Natafuta uso wa Bwana wangu. Kurasini SDA Choir. Kurasini SDA Choir, Kurasini Classics, Ukuta Wa Jeriko Album , Bedi Score , Bedi Lyrics

Kama Wanaisiraeli Lyrics sung by Grace and Glory Singers

Kama Wanaisiraeli Lyrics sung by Grace and Glory Singers 1. Kama Wanaisiraeli Katika safari yao Safari ya siku chache jangwani Ikawa ya miaka mingi Wengi walikata tamaa Wengi walifia njiani Ni wachache walifika Nchi ya ahadi Ni wachache walifika Nchi ya ahadi Refrain Tutembee kwa ujasiri Kwenye safari ya Kaanani Yesu nahodha wetu ‘tatuvusha salama Bila mwongozo wake Hatuwezi vuka mto Yordani Tujipe moyo tutafika 2. Nasi tunapiga hatua Moja mbele mbili nyuma Katika safari yetu ya mbingu Tupatapo majaribu Tukazeni mioyo yetu sasa Tufikie ng'ambo ya pili Kwani Pwani sio mbali Mwisho tutafika Kwani Pwani sio mbali Mwisho tutafika. Grace and Glory Singers.