Tanzania Nakupenda Lyrics Sung by Acacia Singers, Tanzania
Tanzania Nakupenda Lyrics Sung by Acacia Singers, Tanzania Refrain Tanzania nakupenda nchi yangu nakupenda sana Bara pia visiwani sisi sote tupendane sana 1. Tanzania yetu twakupenda kwa hakika Uumbaji wake Mungu wetu ndio twausifu milele Bahari zake alizotupa ndizo twajivunie leo Bahari zake alizotupa ndizo twajivunie leo 2. Maziwa na vito nazo mbuga za wanyama Mlima mrefu Kilimanjaro upitao yote Afrika Makumbusho yetu ya taifa, ni vivutio kwa wageni Makumbusho yetu ya taifa, ni vivutio kwa wageni 3. Taifa la amani na upendo kwa hao wote Dumisha umoja Mungu Baba, na utuepushe na vita Tupe ulinzi toka kwako Afrika yetu iwe moja Tupe ulinzi toka kwako Afrika yetu iwe moja Acacia Singers, Tz.